picha

Saratul-humaza

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.

  1. Adhabu kali itamthubutikia kila mwenye kuramba kisogo, asengenyaye, msengenyaji.
  2. Ambaye amekusanya mali na kuihesabu (tu bila ya kuitumia katika njia za kheri).
  3. Anadhania kuwa mali yake itambakisha milele.
  4. Hasha! Bila shaka atavurumishwa katika (moto unaoitwa) Huttama.
  5. Na ni jambo gani litakalokujulisha (hata ukajua) ni nini (huo moto unaoitwa) Huttama?
  6. (Huo ni) moto wa Mwenyezi Mungu uliowashwa (kwa ukali bara bara).
  7. Ambao unapanda (mpaka) nyoyoni.
  8. Hakika watafungiwa ndani ya moto huo.
  9. Kwa manguzo marefu (ili wasiweze kutoka).

 

Mafunzo kwa Ufupi.

  1. Kusengenya ni katika makosa makubwa kabisa.
  2. Ni makosa makubwa kukusanya mali bila kuitumia katika njia za kheri.
  3. Matumizi mabaya ya ulimi na neema zingine hupelekea kwenye maangamizi na adhabu.
  4.  Matumizi mabaya ya ulimi kama fitna, uongo, usengenyi, n.k. huleta chuki, husda na mtafaruku katika jamii.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Views 2650

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 web hosting     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al qadir

Asbab nuzul surat al qadi. Hii ni sura ya 97 katika mpangilio wa mashaf. Surat al qadir imeteremshwa Madina na ina aya 5.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Ikhlas

Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa Surat al-Kawthar na fadhila zake

SURATUL-KAUTHAR Imeteremshwa maka, na sura hii imeshuka kwa sababu al-aAs ibn Waail.

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...