Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao

Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao

Madai ya Makafiri dhidi ya Qur-an



Waislamu wanaamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an ni kitabu cha Allah (s.w) neno kwa neno kama mwenyewe anavyothibitisha:


"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (2:2)
Pamoja na uthibitisho huu, makafiri wa zama za kale na za sasa wameibuka na upinzani dhidi ya Qur-an na kudai kuwa kitabu hiki amekitunga mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w):



"Au ndio wanasema kuwa hii Qur-an ameitunga (Muhammad)? Bali wao hawaamini lolote." (52:33)
Dai hili la kumpa Mtume (s.a.w) utunzi wa Qur-an limewakilishwa katika sura mbali mbali na makafiri wa zama mbali mbali. Kwa ujumla makafiri wamedai kuwa Qur-an ni:


1. Mashairi aliyotunga Mtume Muhammad (s.a.w).
2. Zao la njozi za Muhammad (s.a.w) zilizovurugika
3. Zao la mwenye kujidhania kupata ufunuo
4. Zao la mwenye kifafa na aliyepagawa na shetani.
5. Aya za shetani
6. Uandishi wa Muhammad (s.a.w) kwa msaada wa Mayahudi na Wakristo.
7. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuleta umoja na ukombozi wa Waarabu.
8. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kurekebisha tabia ya Waarabu.
9. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili ajinufaishe kiuchumi.
10. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuwania madaraka na ukubwa.



Qur-an yenyewe inakanusha madai haya katika aya mbali mbali kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


Basi naapa kwa mnavyoviona. Na msivyoviona. Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe (wa Mwenyezi Mungu) mwenye hishima (kubwa). Wala si kauli ya mtunga mashairi (kama mnavyosema).Ni machache sana mnayoyaamini. Wala si kauli ya mchawi (kama mnavyodai). Ni kidogo kabisa kuwaidhika kwenu. Ni mteremsho utokao kwa Mola wa viumbe vyote. Na kama


(Mtume) angelizua juu yetu baadhi ya maneno tu, bila shaka tungalimshika kwa mkono wa kuume, (wa kulia). Kisha kwa hakika tungalimkata mshipa mkubwa wa moyo (69:38-46).


Na hapana yeyote katika nyie angeweza kutuzuia naye. Kwa hakika hii (Qur-an) ni mawaidha kwa wanaomcha Mwenyezi Mungu. Na kwa yakini tunajua kuwa miongoni mwenu wamo wanaokadhibisha. Na itakuwa ni sikitiko, (m ajut o) juu ya wanaokanusha. Na hakika hii ni haki ya yakini. Basi litukuze jina la Mola wako aliye Mkuu. (69:47-52)
Pamoja na aya hizi na nyingine nyingi zinazokanusha madai ya makafiri dhidi ya utunzi wa Qur-an bado Allah (s.w) ametoa changa moto kwa makafiri wa zama zote tangu ianze kushuka Qur-an hadi leo, kuwa:


"Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia Mtumwa Wetu (kuwa hakuteremshiwa na Mwenyezi Mungu) basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliye mfano wake, na muwaite waungu wenu bighairi ya Mwenyezi Mungu (wakusaidieni), ikiwa mnasema kweli." (2:23)
Pamoja na changamoto hii ya Qur-an, hebu tuangalie kwa undani kidogo udhaifu wa hizi hoja kumi za makafiri dhidi ya Qur-an:




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1565

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
HIKUMU YA BASMALLAH YAANI KUSOMA BISMILLAH

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al bayyinah

Asbab nuzul surat al bayyinh. Sura hii imeteremka Madina na ina aya nane.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)

HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
namna quran inavyogawanya mirathi na wanaorithi pamoja na mafungu yao

Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.

Soma Zaidi...