HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

SURA YA SABA
HUKUMU ZA TAFKHIM NA TARQIQ AT-TAFKHIYM NA AT-TARQIYQ
1.At-Tarqiyq - Kufanya Nyembamba au Nyepesi
Ni kuitamka herufi kwa kuifanya nyembaba au nyepesi. Hali hii hutokea wakati ulimi uanapokuwa mbali na sakafu la kinywa yaani ulimu unakuwa chini. Tarqiyq hutokea katika herufi za chini yaani إسْتِفال (isfal-herufi za kuinamisha) isipokuwa isipokuwa herufi mbili ر na ل.
2.At-Tafkhiym - Kufanya Nene Au Nzito
Hutokea pale inapotamkwa herufi kwa kuifanya kuwa nene au nzito. Hukumu hii hutokea kwa zile hurufi za اٌلإسْتِعْلاء al-isti’ala yaani herufi za kupanda. Herufi hizi hutamkwa wakati ulimu unapokuwa juu ya sakafu la kinywa.
TAFKHEEM

3.Baina ya Tafkhiym na Tarqiyq
Kuna baadhi ya herufi zinaweza kubeba hukumu zote mbili zilizotajwa hapo juu. Yaani wakati mwingine huwa taeqitq na wakati mwingine huwa tafkheem. Herufi hizo ni kama;-
i) Alif ( ا ) ya madd
ii) Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah ( (لله
iii) Raa ( ر)
Laam ( ل ) ya Lafdhw Al-Jalaalah
Kawaida herufi ya ل ni nyepesi ila inapotokea katika jina la Allaah ( ,(سبحانه وتعالى hapo huwa ima ni tafkhiym au tarqiyq kutegemea na i’raab inayotangulia. Ikiwa jina la Allaah ( سبحانه وتعالى ) Limetanguliwa na herufi ya kasrah au ي (yaa) saakinah, hutamkwa kwa tarqiyq. Ama jina la Allaah ( (سبحانه وتعالى Linapotanguliwa na fat-hah, dhwammah au و (waaw) saakinah linatamkwa kwa tafkhiym.
TAFKHEEM

At-Tafkhiym na At-Tarqiyq katika ( ر ) Raa
Halikadhalika herufi hii raa inaweza kuwa nzito au nyepesi, nene au nyembamba kulingana na kanuni za tajweed. Hivyo basi itakuwa tafkhiym katika hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa ina fataha au dhummah
2.Inakapokuwa na sakinah na nyuma yake kuna herufi yenye fataha au dhumah
3.Itakapokuwa na sakinah na nyuma yake kukawa na kasra na mbele yake kukawa na herufi za isti’laa
4.Itakapokuwa ina sakina na nyuma yake kukawa na hamzatul-waswl yaani hamza ya kuungia.
5.Itakaposimamiwa kwa sakina halafu nyuma yake kukawa na sakina na nyuma ya hiyo sakina kukawa na fataha au dhumah.

Pia itakuwa nyepezi au nyembaba itakapokutana na hali zifuatazo;-
1.itakapokuwa na kasra
2.Itakapokuwa na sakina na nyuma yake kuna fataha
3.Itakaposimamiwa na sakina na kukawa nyuma yake kuna sakina iliyotanguliwa na kasra.
4.- 5 Inayoitwa الراء الممالة (ar-raa al-mumaalah) ambayo inasomwa kwa vokali ya ‘e’ badala ya kasrah. Hii ni kutokana na riwaayah ya Hafsw ‘an Aaswim. Nayo ni katika neno la pekee katika Qur-aan, na huwa ni ya tarqiyq inapatikana katika surat hud aya ya 41 (11:41)


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2355

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 web hosting    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Je, mtu anaweza kusoma quran akiwa amelala?

Kusoma Qur'an kuna faida kubwa kwa Muislamu, kwanza kunampatia thawabu, kunatoa nuru maisha yake, mwili wake na kumlinda na mashetani na watu wabaya. Quran ni dawa na pozo kwa magonjwa. Thawabu za Qur-an hulipwa kwa kila herufi. Quran pia huja kutet

Soma Zaidi...
Faida za kujuwa Quran tajwid

Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.

Soma Zaidi...
Maisha ya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 19. Hapa utajifunza maisha ya Mtume kabla ya utume.

Soma Zaidi...
Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.w)

(ii)Qur-an Yenyewe Inajieleza kuwa ni Ufunuo Kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Idh-har katika usomaji wa Quran

Hapa utajifunza kuhusu hukumu ya Idh-har katika usomaji wa Quran.

Soma Zaidi...
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...