Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii

Download Post hii hapa

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr

Surat Al-Asr

SURAT AL-ARS
Wafasiri wengi wanasema sura hii ilishuka Makka.
Imam Shafii anasema, Sura hii ina maana nyingi na pana. Na kama mtu aifikiri, haja zake zote za dini zinaweza kutimizwa. Imesimuliwa katika Hadithi ya kuwa masahaba wawili kila mara walipokuwa wanakutana wakati wa kuagana walikuwa wakisomeana sura hii.




Neno hili maana yake ni wakati, wakati wa alasiri, na pia maana yake ni kukamua. Katika Aya hii Mwenyezi Mungu analeta ushahidi wa wakati kuonyesha ya kwamba kadiri wakati unavyopita umri wa kila mtu unapungua na kuingia katika hasara maana kila kitu kinasogelea mwisho wake na kitakufa. Lakini watu wanaweza kujiepusha na hasara hiyo kwa kuamini na kutenda mema na kuusiana kushika haki na subira, maana mambo haya yatafanya roho zao ziendelee katika maisha ya raha huko Akhera.



Katika sura hii habari za watu wa namna mbili zimeelezwa. Ya kwanza ni wale ambao wamo hasarani, na pili ni wale ambao wameamini na kufanya vitendo vizuri. Ni dhahiri ya kuwa wasioamini wala hawafanyi vitendo vizuri wao ndio watakaokuwa katika hasara. Lakini wanaoamini kwa moyo wote, tena wanaionyesha imani yao kwa viungo vyao, kwa kutenda sawa na walivyoamini, bila shaka wao watalindwa na hasara. Tena ikumbukwe ya kuwa Mwenyezi Mungu aliposema "walioamini" kwa hakika ameashiria kwenye ukamilifu wa elimu; maana imani haiwezi kupatikana bila elimu, Basi mtu anapopata ukamilifu katika elimu, anakuwa mwenye imani hasa. Na Mwenyezi Mungu aliposema "kufanya vitendo vizuri" ameelekeza kwenye ukamilifu wa amali, yaani matendo. Hivyo Mwenyezi Mungu amesema ya kuwa watu wanaokamilika katika elimu, na wanaokamilika katika vitendo, wao wanasalimika katika hasara na wanaokoka.



Hakuna sababu maalumu yenye kuaminika juu ya kushuka kwa sura hii.



UMUHIMU WA SURA HII
Sura hii inachukuliwa kama muhtasari wa Qur'ani nzima na karibu wasomi wote mashuhuri wa kitamaduni na wa kisasa wa Kiislam wakiwemo Imam Shafi, Ibn Kathir, Israr Ahmed na Farhat Hashmi.



Ibn Kathir, mfasiri wa Quran anashikilia kwamba sura hii, kama onyo kwa waumini kutopoteza wakati au wangeweza kudhalilishwa au hata kuharibiwa.



Imam Shafi, alishikilia-kwamba ikiwa Mungu angefunua tu surah hii ingetosha kwa mwongozo wa wanadamu wote. Ilielezea kwa muhtasari kiini cha ujumbe wa Kurani. Kwa hivyo, Imam Shafi'i anasisitiza kwamba ikiwa mtu angefuata ushauri wake, ilitosha kwa wanadamu kupata mafanikio maishani.



Sayyid Qutb, Mfasiri wa Quran, anathibitisha kwamba surah hii inaelezea mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu kulingana na maoni ya Kiisilamu. Anasema kuwa inafafanua, kwa njia iliyo wazi na fupi zaidi, dhana ya kimsingi ya imani katika muktadha wa ukweli wake kamili.



Al-Tabarani: wakati wanadamu wanajikuta wamepotea; inaweza kujihuisha kwa kurudi kwenye fomula iliyotolewa na aya ya tatu na kanuni / masharti manne, ambayo yanazingatiwa kama msingi.






                   





Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1010

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Amri ya Kuchinja Ng'ombe

Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al adiyat
Sababu za kushuka surat al adiyat

Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.

Soma Zaidi...
KISA CHA TEMBO KATIKA QURAN, KUHUSU ABRAHA KUTAKA KUVUNJA AL-KABA NYUMBBA YA aLLAH
KISA CHA TEMBO KATIKA QURAN, KUHUSU ABRAHA KUTAKA KUVUNJA AL-KABA NYUMBBA YA aLLAH

KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat al-Fiyl
Sababu za kushuka surat al-Fiyl

Al fiyl ni neno la Kiarabu lenye maana ya tembo. Sura hii inazungumziakisa cha jeshi lenye tembo. Jeshi hili lilikuwa na nia ya kuvunja al qaaba

Soma Zaidi...
sura ya 11
sura ya 11

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...