Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad

(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.

Quran si njozi za mvurugano alizoota Mtume Muhammad

(ii)Dai kuwa Qur-an ni zao la njozi za Mtume (s.a.w) zilizovurugika:



Katika miaka ya 1960 waandishi wawili, Anderson na Watt, walikuja na dai kuwa Qur-an ni zao la dhana (Wishful Thinking).


Walidai kuwa maneno na maelezo ya habari mbalimbali yaliyomo katika Qur-an yametokana na mawazo ya Mtume (s.a.w) aliyoyatoa kwa dhana tu. Watt, kwa kutumia njia za kisasa za kuchunguza fasihi alihitimisha kuwa angelifanya makosa makubwa sana kama angeliamini kuwa Qur-an ni ujumbe wa Allah (s.w) kwani: "Kila kinachoonekana kinatoka nje ya fikra za mwanaadamu, kwa kweli hutokana na mawazo yake ya kinjozi ambayo hutokea bila ya kufikiri." Kwa hiyo alieleza Watt kuwa Qur-an ni zao la dhana (Creative Imagination)



Udhaifu wa Dai hili:
Nadharia ya Anderson na Watt haina nguvu yoyote kwa sababu katika historia nzima ya mwanaadamu hapajatokea mawazo ya kinjozi hata yawe yamebuniwa kwa uhodari kiasi gani yakaunda kitabu mithili ya Qur-an au hata angalau sura moja iliyo mithili na sura yoyote ya Qur-an. Hata hivyo, jambo la kukumbuka ni kwamba dai hili la Anderson na Watt na makafiri wengine wa kisasa wenye mawazo kama hayo, si geni bali ni dai kongwe lililotolewa na jamii ya Mtume (s.a.w) mwenyewe kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:


"Lakini (Makafiri) walisema: "(Hayo anayosimulia) ni ndoto zilizovurugika. Bali ameyabuni (mwenyewe). Bali huyu ni mtunga mashairi tu.Basi atuletee Muujiza kama walivyotumwa (Mitume) wa kwanza." (21:5)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1025

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Hukumu za mim sakina na tanwinkwenye hukumu za tajwid

Hukumu za kim sakina na tanwin ni idgham shafawiy, idh-har shafawiy, na Ikhfau shafawiy

Soma Zaidi...
Maswali yanayohusu quran

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
Saratul-asr 103

Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka Surat al fatiha (Alhamdu)

Kwa kuwa hakuna sababu mwalumu ikiyonukuliwa kuwa ndio chanzo cha kushushwa suravhii. Basi post hii itakujuza mambo ambayo huwenda hukuyajuwa kuhusu fadhika za surabhii na mengineyo.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA (MIIM SAKINA)

HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA : Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...