Madai ya Makafiri dhidi ya Qur-an
Waislamu wanaamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an ni kitabu cha Allah (s.w) neno kwa neno kama mwenyewe anavyothibitisha:
"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (2:2)
Pamoja na uthibitisho huu, makafiri wa zama za kale na za sasa wameibuka na upinzani dhidi ya Qur-an na kudai kuwa kitabu hiki amekitunga mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w):
"Au ndio wanasema kuwa hii Qur-an ameitunga (Muhammad)? Bali wao hawaamini lolote." (52:33)
Dai hili la kumpa Mtume (s.a.w) utunzi wa Qur-an limewakilishwa katika sura mbali mbali na makafiri wa zama mbali mbali. Kwa ujumla makafiri wamedai kuwa Qur-an ni:
1. Mashairi aliyotunga Mtume Muhammad (s.a.w).
2. Zao la njozi za Muhammad (s.a.w) zilizovurugika
3. Zao la mwenye kujidhania kupata ufunuo
4. Zao la mwenye kifafa na aliyepagawa na shetani.
5. Aya za shetani
6. Uandishi wa Muhammad (s.a.w) kwa msaada wa Mayahudi na Wakristo.
7. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuleta umoja na ukombozi wa Waarabu.
8. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kurekebisha tabia ya Waarabu.
9. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili ajinufaishe kiuchumi.
10. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuwania madaraka na ukubwa.
Qur-an yenyewe inakanusha madai haya katika aya mbali mbali kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
Basi naapa kwa mnavyoviona. Na msivyoviona. Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe (wa Mwenyezi Mungu) mwenye hishima (kubwa). Wala si kauli ya mtunga mashairi (kama mnavyosema).Ni machache sana mnayoyaamini. Wala si kauli ya mchawi (kama mnavyodai). Ni kidogo kabisa kuwaidhika kwenu. Ni mteremsho utokao kwa Mola wa viumbe vyote. Na kama
(Mtume) angelizua juu yetu baadhi ya maneno tu, bila shaka tungalimshika kwa mkono wa kuume, (wa kulia). Kisha kwa hakika tungalimkata mshipa mkubwa wa moyo (69:38-46).
Na hapana yeyote katika nyie angeweza kutuzuia naye. Kwa hakika hii (Qur-an) ni mawaidha kwa wanaomcha Mwenyezi Mungu. Na kwa yakini tunajua kuwa miongoni mwenu wamo wanaokadhibisha. Na itakuwa ni sikitiko, (m ajut o) juu ya wanaokanusha. Na hakika hii ni haki ya yakini. Basi litukuze jina la Mola wako aliye Mkuu. (69:47-52)
Pamoja na aya hizi na nyingine nyingi zinazokanusha madai ya makafiri dhidi ya utunzi wa Qur-an bado Allah (s.w) ametoa changa moto kwa makafiri wa zama zote tangu ianze kushuka Qur-an hadi leo, kuwa:
"Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia Mtumwa Wetu (kuwa hakuteremshiwa na Mwenyezi Mungu) basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliye mfano wake, na muwaite waungu wenu bighairi ya Mwenyezi Mungu (wakusaidieni), ikiwa mnasema kweli." (2:23)
Pamoja na changamoto hii ya Qur-an, hebu tuangalie kwa undani kidogo udhaifu wa hizi hoja kumi za makafiri dhidi ya Qur-an:
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa
Soma Zaidi...Sura hii iliposhuka ilikuwa kama imekuja kuwasuta Wanafiki waliokuwa wakizungumzahabari za uongo kuhusu jeshi alilolituma Mtume wa Allah.
Soma Zaidi...2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA
Soma Zaidi...Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.
Soma Zaidi...Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.
Soma Zaidi...Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kufundisha fadhila na faida za kusoma Alhamdu.
Soma Zaidi...Je Qur-an ilikusanywa na kuandikwa katika msahafu wakati wa uongozi wa Abu-Bakr(r.
Soma Zaidi...