Sababu za kushuka surat al humazah

Sura hii inaonya vikali tabia ya kusengenya na kusambaza habari za uongo. Wameonywa vikali wenye tabia ya kujisifu kwa mali, kukusanya mali bila ya kuitolea zaka.

Surat Al-Humazah

SURAT ALHUMAZAH
Sura hii imeteremshwa Maka na ina aya 10 pamoja na bismillah.


Wafasiri wengi wanakubaliana ya kuwa sura hii ilishuka Makka. Hali ya watu wa siku za Mtume s.a.w. waliokuwa wakiwaudhi Waislamu na wakijivuna kwa mali zao, imeelezwa katika sura hii.


 

Humazah, "Msingiziaji." Neno hili limetoka katika neno hamazah lenye maana ya
kusingizia; kukoneka; kupiga kwa kidole; kusukumu; kupiga; kuuma; kusengenya; kuvunja; kutia wasiwasi.


 

Lumazah (Msingiziaji) ni neno lililotoka katika lamazah, yaani kusingizia, kuaibisha; na ku- koneka.


 

Masahaba na watu wa baadaye wamehitilafiana katika maana ya Aya hii, na hakuna sababu yake nyingine isipokuwa ya kwamba maneno haya mawili humazah na lumazah yanakaribiana sana katika maana. Inasemekana ya kuwa Mughira, A'as bin Wail na Sharik walikuwa wakishughulika kila mara kumwudhi Mtume s.a.w. na masahaba kwa kuwasingizia na kuwaaibisha; basi Mwenyezi Mungu katika sura hii akawaonya ya kuwa waache mwendo wao huo waila wataangamizwa.


 

Lakini hakuna haki ya kusema ya kuwa watu hawa watatu tu ndio walioonywa, maana
wangekuwa ni hao watatu tu, basi wangetajwa majina yao. Lakini badala ya kutajwa majina yao Mwenyezi Mungu amesema, Maangamizo kwa kila msingiziaji, msengenyaji. Hili laonyesha ya kuwa watu wote wenye ada na mwendo wa namna hiyo wameonywa - wawe watu wa zamani, wa leo, hata na wa baadaye - wote watapata adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa dhambi zao za kuwasingizia, kuwaaibisha, kuwasengenya na kuwateta watu. Hivyo, Mwenyezi Mungu amewaonya
watu wote wa siku zote ili wasishike njia ya namna hii inayoleta machafuko makubwa kati ya jamii za watu na makabila, na watu wanatenguka nguvu zao na kuangamia kabisa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2331

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat Al-Humazah

Zijuwe sababu kuu za kushuka surat Al-Humazah katika quran

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka kwa surat An-Nasr (idhaa jaa)

SURATUN-NASR Sura hii imeteremka wakati Mtume (s.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hukumu za mim sakina na tanwinkwenye hukumu za tajwid

Hukumu za kim sakina na tanwin ni idgham shafawiy, idh-har shafawiy, na Ikhfau shafawiy

Soma Zaidi...