Vyakula vya kupunguza presha ya kupanda

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula ambavyo vinaweza kupunguza presha ya kupanda

VYAKULA AMBAVYO HUSAIDIA KUPUNGUZA PRESHA YA KUPANDA AMA HULINDA MWILI DHIDI YA PRESHA YA KUPANDA.

Presha ya kupanda inaweza kupelekea athari kubwa na mbaya sana kwenye afya ya mtu. Presha ya kupanda isipotibiwa ama mtu asipofuata masharti ya kuishi na ugonjwa huu madhara makubwa yanaweza kutokea. Kifo, kupasuka kwa mishipa ya damu, kupalalaizi, kuharibika kwa figo na moyo kushindwa kufanya kazi na kupata shambulio la moyo yote haya yanaweza kuwa ni matokeo ya presha ya kupanda pindi isipotibiwa ama mtu asipofata masharti.:-

 

Unaweza kupamana na presha kwa kufuata mashari kama kufanya mazoezi, kula vyakula salama kwa presha, kupunguza misongo ya mawazo, kupunguza kula chumvi, kupunguza uzito, kupunguza ama kuacha sigara na pombe. Miongoni mwa vyakula salama kwa presha ni kama

1.Mboga za majani ambazo zina madini ya potassium kwa wingi. Madini haya ni mujarabu sana katika kulinda na kuimarisha afya ya moyo. Ulaji wa mboga hizi unaweza kuwa ni njia ya kujilinda na presha ya kupanda. Miongoni mwa mboga hizi ni kama spinachi

2.Maziwa: maziwa ni katika vyakula vyenye madini ya calcium kwa wingi na pia yana mafuta kwa uchache. Hali zote mbili hizi ni muhimu kwa afya ya moyo.

3.Ndizi; ndizi ni katika matunda yenye madini ya potassium kwa wingi. Ulaji wa ndizi unaweza kuwa ni msaada mzuri kwa kulinda mwili dhidi ya presha ya kupamda.

4.Mayai

5.Samaki aina ya salmon na wanaofanana nao.

6.Ulaji wa mbegu za mimea kama maboga na alizeti

7.Kitunduu thaumu: unaweza kutumia vitunguu thaumu kwa kula ama kutafuna, ni vyema kufunga mdomo wakati unapotafuna.

8.Makomamanga; unaweza kula atunda hili kama juisi ama kula kawaida.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 2957

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula miwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula miwa

Soma Zaidi...
Faida za ubuyu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula ubuyu

Soma Zaidi...
Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo, na vyakula salama kwa vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Faida za kula papai

Posti hii inaonyesha Faida za kula papai.papai Ni tunda na Lina leta afya,nguvu na kuujenga mwili.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu maji, kazizake mwilini na athari za upungufu wake mwilini

Hpa utafahamu faida za maji mwilini pamoja na athari za upungufu wa maji mwilini na dalili zake

Soma Zaidi...
Dalili za ukosefu wa madini ya iodini (goiter)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili za upungufu wa iodini ambapo kitaalamu hujulikana Kama goiter. Goiter Ni Sababu ya kawaida ya goiter duniani kote ni ukosefu wa iodini katika chakula. Nchini Marekani, ambako utumiaji wa chumvi yenye iodini ni j

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula bamia

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia

Soma Zaidi...
Vyakula vilivyo hatari kwa afya ya meno

Vyakula hivi vinaweza kuwa na hatai kwenye afya ya meno ama kuharibu kabisa meno.

Soma Zaidi...