Zijue kazi za madini ya chuma mwilini

Posti hii inahusu zaidi kazi za madini ya chuma mwilini,Ni madini ambayo ufanya kazi mbalimbali mwilini na pia utokana na vyakula mbalimbali ambavyo upatikana kwenye wanyama na mimea. Zifuatazo ni kazi za madini ya chuma.

1. Madini ya chuma usaidia kusafilisha gasi ya oxygeni kutoka sehemu mbalimbali za mwili na kwenda sehemu nyingine za mwili ambapo oxgeni inahitajika.

 

2. Madini ya chuma usaidia katika kazi za haemoglobini ambayo ubeba gasi ya oxygeni kutoka kwenye mapafu kwenda sehemu mbalimbali za mwili na pia haemoglobini hiyo ubeba carbon dioxide kutoka kutoka kwenye sehemu mbalimbali za mwili mpaka kwenye mapafu kwa ajili ya kutafuta oxgeni kwa hiyo kazi ya kusafilisha hizi gasi mbili usaidia na madini ya chuma.

 

3. Madini ya chuma usaidia kusafilisha damu ya oxgeni kwenye misuli ambapo kitendo hiki kwa kitaalamu huitwa myoglobin ambayo ni sehemu ya protein kwenye misuli,kwa hiyo myoglobini asili yake ni protini ambayo inaweza kusafilisha gasi ya oksijeni kwenye misuli, hii kazi usaidiwa na madini ya chuma.

 

4. Madini ya chuma yanasaidia katika upumuaji kwa sababu ya kuwepo kwa cytochrome ambayo ni sehemu ya madini ya chuma, cytochrome usaidia katika kusafirisha hewa wakati wa kupumua, kwa sababu cytochrome imetengenezwa na madini ya chuma, ndo maana tunaaweza kusema kuwa madini ya chuma usaidia katika upumuaji.

 

5. Madini ya chuma usaidia katika kuzalisha protini hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa baadhi ya vitu ambavyo vimetengenezwa kwa madini ya chuma ambayo usaidia kutengeneza protein kwa kitaalamu huitwa xanthine oxidase - enzyme ambayo ni sehemu ya madini ya chuma.

 

6.Madini ya chuma ni sehemu ya enzyme, tunajua kuwa enzyme ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili, kwa hiyo madini ya chuma ni sehemu ya enzyme ambazo kwa kitaalamu huitwa peroxide, catalase na enzyme nyingine nyingi ambazo ufanya kazi mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.

 

7.Madini ya chuma usaidia katika kuzalisha homoni ambazo utumika kufanya kazi mbalimbali kwenye mwili kama vile kuhakikisha kiwango Cha sukari kipo sawa kwenye mwili, kutengeneza protini kwenye mwili, kukua na kuzaliana na kazi zote mwilini ambazo utengenezwa na homoni.

 

Wapi tunaaweza kupata madini ya chuma?

1. Madini ya chuma tunaaweza kuyapata katika sehemu mbalimbali kama vile nyama, samaki, vyakula kama vile njegere, maharage,soya beans, njugu Mawe na vyakula vyote ambavyo ni jamii ya kuunde hivi vyote tunaviita kwa kitaalamu heme - iron .Kuna vyakula vingine ambavyo tunaviita non- heme iron kama vile vyakula vinavyopatikans kwenye mboga za majani, mayai na maziwa.

 

Nini madhara ya kukosa madini ya chuma mwilini.

1. Madini ya chuma yakikosa mwilini mtu anaweza kupata upungufu wa damu mwilini ambapo kwa kitaalamu huitwa Anaemia, ambayo upelekea mwili kuchoka, kizunguzungu, kichwa kuuma na mwili una kiss kinga mwilini  kwa hiyo unaweza kupata magonjwa nyemelezi .

 

2. Madini ya chuma yakikosa mwilini mtu anaweza kupata ugonjwa wa kuvimba matezi ambao kwa kitaamu huitwa goitre yaani ni kuvimba kwenye shingo ambapo ugonjwa huu usababisha madhara makubwa kwa watu wengi, kwa hiyo tunapaswa kula vyakula vyenye wingi wa madini ya chuma usaidia sana katika shughuli mbalimbali kwenye mwili wa binadamu.

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 4331

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula maboga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
vyakula vya kuongeza damu, dalili zake na sababu za upungufu wa damu

Zijuwe sababu za upungufu wa damu, dalili za upungufu wa damu na kazi za damu mwilini,n avyakula vya kuongeza damu

Soma Zaidi...
Vyakula na ugonjwa wa kisukari

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya vyakula vimpasavyo mgonjwa wa kisukari

Soma Zaidi...
Faida za kula papai

Posti hii inaonyesha Faida za kula papai.papai Ni tunda na Lina leta afya,nguvu na kuujenga mwili.

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula spinach

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula spinach

Soma Zaidi...
Faida za kula Ndizi

Kuna faida kubwa za kiafya kwa kula ndizi, soma makala hii mpaka mwisho

Soma Zaidi...
Majani ya mstafeli dhidi ya bakteria na fangasi

Posti hii inahusu zaidi kazi ya majani ya mstafeli dhidi ya bakteria na fangasi, pamoja na kutibu saratani mbalimbali na upambana na fangasi na bakteria kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Faida za kunywa maziwa

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kunywa maziwa kiafya

Soma Zaidi...