picha

Lishe salama kwa mjamzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu lishe salama kwa mjamzito

LISHE SALAMA KWA MJAMZITO:Kwa ufupi ni kuwa mjamzito na anayenyonyesha wanatakiwa wapewe lishe kamili iliyokuwa na virutubisho vyote. Haata hivyo ni vyema kuzingatia nukuu za hapo chini. Wanaonyonyesha na wajawazito wanahitaji kupata vyakula vyenye viinilishe vya kutosha ili kuwezesha ukuaji wa mtoto tumboni , utengenezwaji wa maziwa na kwa ajili ya afya zao wenyewe.

 

Vyakula vya protini vinahitajika kwa mkiwango kikubwa ili kuwezesha mwili wa mama kujenga misuli vizuri , tishu katika mwili wake na mwili wa mtoto aliye tumboni. Utengenezwaji wa maziwa , usafirishwaji wa damu na ukuaji wa viungo vya mama na mtoto unahitaji protini. Hivyo wamama hawa wapewe protini kwa wingi.vyakula vya protini ni kama:-A.NyamaB.MayaiC.MaharagweD.SamakiE.MaziwaF.Pia kwenye nafaka na baadhi ya mboga za majani na matunda.

 

Vyakila vya folic asid na vitamini B vinahitajika kwa ajili ya kuwezesha kupunguza tatizo la kushindwa kujifunguwa kwa njia ya kawaida. Vyakula vya madini ya kashiam(calcium) ni muhimu kwa ukuwji wa mifupa ya mtoto aliye tumboni na kuimarika mwili wa mama pia. Kwani mjamzito asipopewa madini haya mtoto atatumia madini yaliyomo kwa mama na kumfanya mama awe na mifupa dhaifu katika kipindi hiki.

 

Madini ya chuma ni muhimu katika utengenezwaji wa damu, halikadhalika mtoto anahitaji madini haya ili ayatumie katika wiki ya kwanza ya kuzaliwa. Madini ya zink ni muhimu katika kuwezesha kujifunguwa.(progression of labour) na ukuaji salama wa mtoto aliyoko tumboni.

 

Wamama wajawazito wapewe vyakula vyenye kambakamba (dietary fiber}. Hivi vitamuwezesha kutopata tatizo la kukosa choo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-10-29 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1889

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 ai web app    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Faida za ukwaju (tamarind)

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za ukwaju

Soma Zaidi...
Vyakula vya vitamin E

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya vitamin E

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula pera

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula pera

Soma Zaidi...
Athari za kula vitamin C kupitiliza

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu athari za kula vitamini C kupitiliza

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Soma Zaidi...
Faida za muarobaini

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za muarobaini

Soma Zaidi...
Matunda yenye vitamin C kwa wingi

Somo hili linakwenda kukuletea matunda yenye vitamin C kwa wingi

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula karanga

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula karanga

Soma Zaidi...
Zijuwe faida za kula njegere

zijuwe faida za kula njegere kiafya na umuhimu wa kula jegere pia jifunze njegere zina kazi gani mwilini?

Soma Zaidi...