picha

Vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo

VYAKULA HATARI NA VYAKULA SALAMA KWA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni moja kati ya maradhi yanayosumbuwa watu kutokana na kuchelewa kwake kupona hata baada ya kutumia dawa nyingi. Hali hii husababishwa kutokana na kutofata masharti ya vidonda vya tumbo vyema. Mgonjwa anatakiwa kufata masharti, ajuwa ni vyakula vipi atumie na vipi asitumie. Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

 

Pia makala hii itakwenda kukufundisha vyakula ambavyo hutumuka kama dawa kwa ajili ya kutibu maradhi hususan vidonda vya tumbo. Mwisho wa makala hii utaweza kujifyunza ni kwa nini vidonda vingine haviponi, na vidonda sugu vinatokeaje.

 

Vyakula salama kwa wenye vidonda vya tumbo

1. Kabichi

2. Maepo

3. Karoti

4. Mboga za kijani

5. Asali

6. Kitunguu thaumu

 

Vyakula salama kwa vidonda vya tumbo pia ni dawa

1. Juisi ya kabichi

Kabihi ni katika mboga ambazo zina vitamini C. vitamini hii pia ni katika antioxidant ambayo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.

 

2. Asali

Asali nikatika baadhi ya vyakula ambavyo huhusishwa na matibabu mbalimbali. Asali husaidia kuimarisha afya ya moyo, pia hutumika kama dawa kwenye majeraha na majeraha ya moto ili kuzuia bakteria. Asali inaweza pia kupambana na bakteria wa kusababisha vidonda vya tumbo

 

3. Kitunguu thaumu.

ni katika viungo vya mboga kama kinavyotumika.lakini pia ni katika tiba za asili ambazo hutumiwa maeneo mengi duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa katika kitunguu thaumu kuna chembechembe ambazo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.

 

4. Shubiri

Shubiri si katika vyakula ila hutumika sana katika viwanda vya vyakula, urembo na viwanda vya kutengeneza madawa. Shubiri ni katika tiba asili ambazo hutumiwa maeneo mbalimbali duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa shubiri lina uwezo wa kuzuia mashambulizi ya bakteria kwenye ngozi. Pia shubiri limeonekana kuwa na uwezo wa kutibu vidonda vya tumbo.

 

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:

1. Maziwa.

Wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanatambuwa kuwa akinywa maziwa maumivu yanapunguwa. Hii ni faida, lakini tafiti zinaonyesha kuwa maziwa yanaongeza uzalishwaji na utaji wa tindikali za tumboni. Tindikali hizi zina mchango sana katika kusababisha vidonda vya tumbo

2. Pombe

Unywaji wa pombe unaweza kuathiri na kuharibu kuta za tumbo na utumbo. Hali hii inaweza kuongeza hatari ya kuweza kupata vidonda vya tumbo. Ama inaweza kusababisha hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

3. Kahawa;

Kahawa inaweza kusababisha kuongezeka kwa uzalishwaji wa tindikali za tumboni (stomach acid). tindikal hizi zikizalishwa kwa wingi tumboni zinaweza kuchubuwa ukuta wa tumbo na hatimaye kusababisha vidonda vya tumbo

4. Vyakula vyenye mafuta na fati kwa wingi.

5. Pilipili kali vyema kupunguza kuzitumia

6. Vyakula vyenye chumvi nyingi

7. Vyakula vya kuoka

8. Vyakula vyenye uchachu

9. Wacha kuvuta sigara

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Vyakula Main: Post File: Download PDF Views 2481

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 web hosting     👉4 ai web app     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Vyakula vinavyoondoa sumu mwilini

Katika somo hili tutajifunza Mifumo ya mwili inayotoa sumu. Ushahidi wa kitaaluma kuhusu nafasi ya matunda na mboga kwenye detox. Aina za matunda na mboga zenye ufanisi. Kanuni za matumizi salama.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuoambana na mafua

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula vya kuoambana na mafua

Soma Zaidi...
Kazi za protini mwilini ni zipi?

Virutubisho vya protini vina kazi nyingi mwilini. Zifuatazo ndio kazi protini mwilini

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kufunga (Intermittent Fasting).

​Kufunga kwa vipindi (Intermittent Fasting) sio mlo maalumu, bali ni mtindo wa maisha unaohusu kubadili nyakati unazokula badala ya aina ya chakula unachokula. Mbinu hii imepata umaarufu mkubwa ulimwenguni kwa ahadi yake ya kupunguza uzito na kuboresha afya ya jumla. Makala haya yanachambua nini hasa hufanyika mwilini unapotumia mtindo huu ili uweze kufanya uamuzi sahihi.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mara moja

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya matiti yanayopaswa kutolewa taarifa mapema, kwa sababu ya kuwepo kwa saratani ya matiti, kuna dalili ambazo zikijitokeza zinapaswa kutolewa taarifa mara moja bila kuchelewa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...