picha

Vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya vyakula hatari na salama kwa vidonda vya tumbo

VYAKULA HATARI NA VYAKULA SALAMA KWA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni moja kati ya maradhi yanayosumbuwa watu kutokana na kuchelewa kwake kupona hata baada ya kutumia dawa nyingi. Hali hii husababishwa kutokana na kutofata masharti ya vidonda vya tumbo vyema. Mgonjwa anatakiwa kufata masharti, ajuwa ni vyakula vipi atumie na vipi asitumie. Makala hii inakwenda kufundisha vyakuna na vinjwaji salama anavyopaswa kutumia mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Pia utajifunza vyakula na vinywaji hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

 

Pia makala hii itakwenda kukufundisha vyakula ambavyo hutumuka kama dawa kwa ajili ya kutibu maradhi hususan vidonda vya tumbo. Mwisho wa makala hii utaweza kujifyunza ni kwa nini vidonda vingine haviponi, na vidonda sugu vinatokeaje.

 

Vyakula salama kwa wenye vidonda vya tumbo

1. Kabichi

2. Maepo

3. Karoti

4. Mboga za kijani

5. Asali

6. Kitunguu thaumu

 

Vyakula salama kwa vidonda vya tumbo pia ni dawa

1. Juisi ya kabichi

Kabihi ni katika mboga ambazo zina vitamini C. vitamini hii pia ni katika antioxidant ambayo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.

 

2. Asali

Asali nikatika baadhi ya vyakula ambavyo huhusishwa na matibabu mbalimbali. Asali husaidia kuimarisha afya ya moyo, pia hutumika kama dawa kwenye majeraha na majeraha ya moto ili kuzuia bakteria. Asali inaweza pia kupambana na bakteria wa kusababisha vidonda vya tumbo

 

3. Kitunguu thaumu.

ni katika viungo vya mboga kama kinavyotumika.lakini pia ni katika tiba za asili ambazo hutumiwa maeneo mengi duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa katika kitunguu thaumu kuna chembechembe ambazo husaidia katika kupambana na bakteria aina ya H.pylori ambao ndio chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo.

 

4. Shubiri

Shubiri si katika vyakula ila hutumika sana katika viwanda vya vyakula, urembo na viwanda vya kutengeneza madawa. Shubiri ni katika tiba asili ambazo hutumiwa maeneo mbalimbali duniani. Tafiti zinaonyesha kuwa shubiri lina uwezo wa kuzuia mashambulizi ya bakteria kwenye ngozi. Pia shubiri limeonekana kuwa na uwezo wa kutibu vidonda vya tumbo.

 

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:

1. Maziwa.

Wagonjwa wa vidonda vya tumbo wanatambuwa kuwa akinywa maziwa maumivu yanapunguwa. Hii ni faida, lakini tafiti zinaonyesha kuwa maziwa yanaongeza uzalishwaji na utaji wa tindikali za tumboni. Tindikali hizi zina mchango sana katika kusababisha vidonda vya tumbo

2. Pombe

Unywaji wa pombe unaweza kuathiri na kuharibu kuta za tumbo na utumbo. Hali hii inaweza kuongeza hatari ya kuweza kupata vidonda vya tumbo. Ama inaweza kusababisha hali ya mgonjwa kuwa mbaya zaidi.

3. Kahawa;

Kahawa inaweza kusababisha kuongezeka kwa uzalishwaji wa tindikali za tumboni (stomach acid). tindikal hizi zikizalishwa kwa wingi tumboni zinaweza kuchubuwa ukuta wa tumbo na hatimaye kusababisha vidonda vya tumbo

4. Vyakula vyenye mafuta na fati kwa wingi.

5. Pilipili kali vyema kupunguza kuzitumia

6. Vyakula vyenye chumvi nyingi

7. Vyakula vya kuoka

8. Vyakula vyenye uchachu

9. Wacha kuvuta sigara

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1996

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Faida za kiafya za kula bamia/okra

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia

Soma Zaidi...
UPUNGUFU WA PROTINI NA FATI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Faida za kula uyoga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kula uyoga

Soma Zaidi...
Faida za kula apple (tufaha)

Posti hii itakwende kukueleza kuhusu faida za kula apple na umuhimu wake kiafya

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula fenesi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula fenesi

Soma Zaidi...
Faida za kula kabichi

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula kabichi

Soma Zaidi...
Vyakula vya protini na kazi zake

Hapa utajifunza kuhusu kazi za protini mwilini na vyakula vipi vina protini kwa wingi

Soma Zaidi...
Faida za ubuyu

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula ubuyu

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula njegere, kunde, mbaazi, njugu mawe na maharage

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula njegere, kunde, mbaazi, njugu mawe na maharage

Soma Zaidi...