Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.

Download Post hii hapa

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.


Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w). Makafiri hao walichimba mahandaki na ndani yake wakawasha moto mkubwa kisha wakawa wanawatosa waumini humo mmoja baada ya mwingine. Dhun-Nuwas mmoja



wa waliokuwa wafalme wa Mayahudi; aliingia Najran akiwa na jeshi kubwa ili awalazimishe watu wa Najran wasifuate mafundisho ya Mitume. Watu wa Najran walipokataa kumfuata, alichimba handaki kubwa akawasha moto akawa anamtumbukiza Muumini mmoja baada ya mwingine huku yeye na watu wake wanachekelea. Habari hii inaelezwa katika Suratul-Buruj, kama ifuatavyo:




“(Kuwa) wameangamizwa watu waliowaadhibu Waislamu katika mahandaki. Yenye moto wenye kuni (nyingi). Walipokuwa wamekaa hapo (Waliangamizwa makafiri hao pale wakati walipokuwa) wanatazama yale wanayowafanyia hao Waislamu (walipokuwa wakiwaadhibu). Nao hawajaona baya lolote kwao (Waislamu) ila kumuamini Mwenyezi Mungu Mwenye kushinda (na) Mwenye kusifiwa. Ambaye ni Mwenye Ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuona kila kitu” (85:4-9).



Kisa hiki kimesimuliwa kiwape fundisho na kuwaliwaza waumini wa zama zote; kwamba taabu iwapatayo kutoka kwa makafiri imeanza kuwafikia ndugu zao waliotangulia. Aidha, kutokana na kisa hiki Waislamu wanapata funzo kuwa kubakia na Imani Thabiti na suala la kusimamisha Uislamu katika jamii, kwahitaji juhudi na subira kubwa sana.

Mwenyezi Mungu anawaliwaza Waislamu kuwa makafiri wanaowatesa na kuwaghasi Waislamu hivi leo, atawaadhibu na kuwatesa kweli kweli kama alivyowatesa As-habul- Khudud.




“Hakika wale waliowaadhibu Waislamu wanaume na Waislamu wanawake, kisha wasitubie basi watapata adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu ya kuungua (barabara)” (85:10). “Hakika kutesa kwa Mola wako ni kukali (sana)” (85:12).



Lakini pamoja na kuliwazwa huko; Waislamu hawatakiwi walale usingizi wasubiri nusura ya Mwenyezi Mungu. Ni wajibu wao wajiandae kwa kila mbinu kupambana na vitimvi vya maadui zao.



“Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezao (silaha), mafarasi yaliyofungwa tayari tayari ili kwazo muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu .................” (8:60).



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1323

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri
Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya vita vya Muta
Historia ya vita vya Muta

hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita.

Soma Zaidi...