Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)



“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. (12:7).

Baadhi ya mazingatio kutokana na kisa hiki ni haya yafuatayo:



(i) Mitume huzaliwa Mitume na maisha yao yote kuanzia utotoni ni kiigizo cha tabia njema kwa waumini



(ii) Wazazi hatunabudi kuwafunza watoto wetu tabia njema na kuwalea hivyo mpaka utuuzima wao.



(iii) Watoto wenye tabia njema tuwapende na tuwashajiishe kubakia na mwenendo huo.



(iv) Si vema kutangaza neema tulizo nazo kwa watu hata wale wa karibu yetu ili kujikinga na husuda.



(v) Uislamu ni neema kubwa, hivyo kila atakayejaaliwa kufuata Uislamu vilivyo na kufanya jitihada za kuusimamisha katika jamii,ajiandae kuhusudiwa na makafiri na wanafiki.



(vi) Hila za watu wenye roho mbaya na husuda dhidi ya watu wema wenye kujitahidi kusimamisha Uislamu katika jamii mwisho wake huwafedhehesha wenyewe hapa hapa duniani kama walivyofedheheka ndugu zake Yusufu na mkewe Al-aziz.



(vii) Kutenda mema, ukweli na subira humnyanyua mtu daraja hapa duniani na huko akhera.



(viii) Ukweli ukidhihiri uwongo hujitenga kama tulivyoona kwa nduguze Yusufu na mkewe Al-Aziz.



(ix) Muungwana katika watu ni yule anayekiri makosa yake na kuomba msamaha kama walivyofanya nduguze Yusufu(a.s).



(x) Waumini wanatakiwa wamuige Yusufu(a.s) kwa kuwa wepesi wa kusamehe na kulipa wema badala ya kulipiza kisasi baada ya kufanyiwa ubaya na kisha kuombwa msamaha. Pamoja na Yusufu kuwasamehe ndugu zake, aliwapatia chakula wakati wa njaa na kuwakaribisha Misr katika makazi ya Kifalme.



(xi) Ngao dhidi ya mahasidi, mafatani, n.k. ni kumcha – Mungu, subira,kujitegemeza kwa Allah(s.w) na kuomba kinga yake.



(xii) Hatunabudi kutumia fursa zinazojitokeza katika kulingania Uislamu, kama Yusufu(a.s) alivyoitumia fursa ile alipokutana na wale wafungwa wawili.



(xiii)Matwaaghuuti daima hawawezi kuhukumu kwa uadilifu na kutoa haki sawa hasa pale kesi itakapokuwa ni baina ya mdau wa nchi na raia wa kawaida. Ilidhihirika kwa ushahidi wa wazi kuwa Yusufu(a.s) ndiye aliyekosewa na yule mkewe Al-Aziz, lakini kwa kumlinda na kashfa ile ilibidi Yusufu(a.s) ahukumiwe kwenda gerezani.



(xiv)Waumini wanapobambikiziwa maovu na machafu kutokana na husuda na chuki ya makafiri na wanafiki, wasitengeneze majukwaa ya kujitetea bali waendelee kufanya wema kama Allah(s.w)anavyoagiza:




Na sema(uwaambie): “Tendeni mambo (mazuri). Mwenyezi Mungu atayaona mambo yenu hayo na Mtume Wake na Waislamu. Na mtarudishwa kwa Mjuzi wa siri na dhahiri; naye atakwambieni (yote) mliyokuwa mkiyatenda.” (9:105)


(xv)Tunapokubalika na kuhitajika kuongoza jamii hatunabudi kupendekeza tukabidhiwe kuongoza katika maeneo tunayoyamudu vizuri kitaaluma, kiuzoefu na kiuadilifu na hasa pale tutakapoona hapana watu wengine wa kuongoza kwa uadilifu katika maeneo hayo.



(xvi)Tuchague viongozi waadilifu na wenye tabia njema bila ya kujali ukabila, utaifa, n.k. Yusufu(a.s) alikuwa mtu wa kuja na mtumwa lakini alipewa Uongozi Misr kutokana na elimu yake, tabia yake njema na uadilifu wake.



(xvii)Kiongozi Muumini ni yule anayekumbuka na kuzingatia kuwa wadhifa alionao ni amana aliyokabidhiwa na Allah (s.w) kwa manufaa ya jamii, hivyo hujiepusha na kibri,

majivuno, kujikweza au tabia yoyote inayoashiria dharau kwa wenzake. Funzo hili tunalipata kwenye dua ya Nabii Yusufu(a.s).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1386

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)

Kwa tabia zake njema Yusufu(a.

Soma Zaidi...
Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Soma Zaidi...
Mafunzo kutokana na vita vya badri

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga

Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.

Soma Zaidi...
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...
Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao

Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.

Soma Zaidi...