“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.
“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. (12:7).
Baadhi ya mazingatio kutokana na kisa hiki ni haya yafuatayo:
(i) Mitume huzaliwa Mitume na maisha yao yote kuanzia utotoni ni kiigizo cha tabia njema kwa waumini
(ii) Wazazi hatunabudi kuwafunza watoto wetu tabia njema na kuwalea hivyo mpaka utuuzima wao.
(iii) Watoto wenye tabia njema tuwapende na tuwashajiishe kubakia na mwenendo huo.
(iv) Si vema kutangaza neema tulizo nazo kwa watu hata wale wa karibu yetu ili kujikinga na husuda.
(v) Uislamu ni neema kubwa, hivyo kila atakayejaaliwa kufuata Uislamu vilivyo na kufanya jitihada za kuusimamisha katika jamii,ajiandae kuhusudiwa na makafiri na wanafiki.
(vi) Hila za watu wenye roho mbaya na husuda dhidi ya watu wema wenye kujitahidi kusimamisha Uislamu katika jamii mwisho wake huwafedhehesha wenyewe hapa hapa duniani kama walivyofedheheka ndugu zake Yusufu na mkewe Al-aziz.
(vii) Kutenda mema, ukweli na subira humnyanyua mtu daraja hapa duniani na huko akhera.
(viii) Ukweli ukidhihiri uwongo hujitenga kama tulivyoona kwa nduguze Yusufu na mkewe Al-Aziz.
(ix) Muungwana katika watu ni yule anayekiri makosa yake na kuomba msamaha kama walivyofanya nduguze Yusufu(a.s).
(x) Waumini wanatakiwa wamuige Yusufu(a.s) kwa kuwa wepesi wa kusamehe na kulipa wema badala ya kulipiza kisasi baada ya kufanyiwa ubaya na kisha kuombwa msamaha. Pamoja na Yusufu kuwasamehe ndugu zake, aliwapatia chakula wakati wa njaa na kuwakaribisha Misr katika makazi ya Kifalme.
(xi) Ngao dhidi ya mahasidi, mafatani, n.k. ni kumcha – Mungu, subira,kujitegemeza kwa Allah(s.w) na kuomba kinga yake.
(xii) Hatunabudi kutumia fursa zinazojitokeza katika kulingania Uislamu, kama Yusufu(a.s) alivyoitumia fursa ile alipokutana na wale wafungwa wawili.
(xiii)Matwaaghuuti daima hawawezi kuhukumu kwa uadilifu na kutoa haki sawa hasa pale kesi itakapokuwa ni baina ya mdau wa nchi na raia wa kawaida. Ilidhihirika kwa ushahidi wa wazi kuwa Yusufu(a.s) ndiye aliyekosewa na yule mkewe Al-Aziz, lakini kwa kumlinda na kashfa ile ilibidi Yusufu(a.s) ahukumiwe kwenda gerezani.
(xiv)Waumini wanapobambikiziwa maovu na machafu kutokana na husuda na chuki ya makafiri na wanafiki, wasitengeneze majukwaa ya kujitetea bali waendelee kufanya wema kama Allah(s.w)anavyoagiza:
Na sema(uwaambie): “Tendeni mambo (mazuri). Mwenyezi Mungu atayaona mambo yenu hayo na Mtume Wake na Waislamu. Na mtarudishwa kwa Mjuzi wa siri na dhahiri; naye atakwambieni (yote) mliyokuwa mkiyatenda.” (9:105)
(xv)Tunapokubalika na kuhitajika kuongoza jamii hatunabudi kupendekeza tukabidhiwe kuongoza katika maeneo tunayoyamudu vizuri kitaaluma, kiuzoefu na kiuadilifu na hasa pale tutakapoona hapana watu wengine wa kuongoza kwa uadilifu katika maeneo hayo.
(xvi)Tuchague viongozi waadilifu na wenye tabia njema bila ya kujali ukabila, utaifa, n.k. Yusufu(a.s) alikuwa mtu wa kuja na mtumwa lakini alipewa Uongozi Misr kutokana na elimu yake, tabia yake njema na uadilifu wake.
(xvii)Kiongozi Muumini ni yule anayekumbuka na kuzingatia kuwa wadhifa alionao ni amana aliyokabidhiwa na Allah (s.w) kwa manufaa ya jamii, hivyo hujiepusha na kibri,
majivuno, kujikweza au tabia yoyote inayoashiria dharau kwa wenzake. Funzo hili tunalipata kwenye dua ya Nabii Yusufu(a.s).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s.
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7
Soma Zaidi...KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.
Soma Zaidi...Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.
Soma Zaidi...Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Musa alipotimiza muda, alifunga safari na ahali zake kurejea Misri.
Soma Zaidi...Sahaba wa kwanz akufariki akiwa shahidi, alifariki kwa sababu ya mateso aliyoyapata kutoka kwa Makafiri wa ki Quraysh
Soma Zaidi...