Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)



“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. (12:7).

Baadhi ya mazingatio kutokana na kisa hiki ni haya yafuatayo:



(i) Mitume huzaliwa Mitume na maisha yao yote kuanzia utotoni ni kiigizo cha tabia njema kwa waumini



(ii) Wazazi hatunabudi kuwafunza watoto wetu tabia njema na kuwalea hivyo mpaka utuuzima wao.



(iii) Watoto wenye tabia njema tuwapende na tuwashajiishe kubakia na mwenendo huo.



(iv) Si vema kutangaza neema tulizo nazo kwa watu hata wale wa karibu yetu ili kujikinga na husuda.



(v) Uislamu ni neema kubwa, hivyo kila atakayejaaliwa kufuata Uislamu vilivyo na kufanya jitihada za kuusimamisha katika jamii,ajiandae kuhusudiwa na makafiri na wanafiki.



(vi) Hila za watu wenye roho mbaya na husuda dhidi ya watu wema wenye kujitahidi kusimamisha Uislamu katika jamii mwisho wake huwafedhehesha wenyewe hapa hapa duniani kama walivyofedheheka ndugu zake Yusufu na mkewe Al-aziz.



(vii) Kutenda mema, ukweli na subira humnyanyua mtu daraja hapa duniani na huko akhera.



(viii) Ukweli ukidhihiri uwongo hujitenga kama tulivyoona kwa nduguze Yusufu na mkewe Al-Aziz.



(ix) Muungwana katika watu ni yule anayekiri makosa yake na kuomba msamaha kama walivyofanya nduguze Yusufu(a.s).



(x) Waumini wanatakiwa wamuige Yusufu(a.s) kwa kuwa wepesi wa kusamehe na kulipa wema badala ya kulipiza kisasi baada ya kufanyiwa ubaya na kisha kuombwa msamaha. Pamoja na Yusufu kuwasamehe ndugu zake, aliwapatia chakula wakati wa njaa na kuwakaribisha Misr katika makazi ya Kifalme.



(xi) Ngao dhidi ya mahasidi, mafatani, n.k. ni kumcha – Mungu, subira,kujitegemeza kwa Allah(s.w) na kuomba kinga yake.



(xii) Hatunabudi kutumia fursa zinazojitokeza katika kulingania Uislamu, kama Yusufu(a.s) alivyoitumia fursa ile alipokutana na wale wafungwa wawili.



(xiii)Matwaaghuuti daima hawawezi kuhukumu kwa uadilifu na kutoa haki sawa hasa pale kesi itakapokuwa ni baina ya mdau wa nchi na raia wa kawaida. Ilidhihirika kwa ushahidi wa wazi kuwa Yusufu(a.s) ndiye aliyekosewa na yule mkewe Al-Aziz, lakini kwa kumlinda na kashfa ile ilibidi Yusufu(a.s) ahukumiwe kwenda gerezani.



(xiv)Waumini wanapobambikiziwa maovu na machafu kutokana na husuda na chuki ya makafiri na wanafiki, wasitengeneze majukwaa ya kujitetea bali waendelee kufanya wema kama Allah(s.w)anavyoagiza:




Na sema(uwaambie): “Tendeni mambo (mazuri). Mwenyezi Mungu atayaona mambo yenu hayo na Mtume Wake na Waislamu. Na mtarudishwa kwa Mjuzi wa siri na dhahiri; naye atakwambieni (yote) mliyokuwa mkiyatenda.” (9:105)


(xv)Tunapokubalika na kuhitajika kuongoza jamii hatunabudi kupendekeza tukabidhiwe kuongoza katika maeneo tunayoyamudu vizuri kitaaluma, kiuzoefu na kiuadilifu na hasa pale tutakapoona hapana watu wengine wa kuongoza kwa uadilifu katika maeneo hayo.



(xvi)Tuchague viongozi waadilifu na wenye tabia njema bila ya kujali ukabila, utaifa, n.k. Yusufu(a.s) alikuwa mtu wa kuja na mtumwa lakini alipewa Uongozi Misr kutokana na elimu yake, tabia yake njema na uadilifu wake.



(xvii)Kiongozi Muumini ni yule anayekumbuka na kuzingatia kuwa wadhifa alionao ni amana aliyokabidhiwa na Allah (s.w) kwa manufaa ya jamii, hivyo hujiepusha na kibri,

majivuno, kujikweza au tabia yoyote inayoashiria dharau kwa wenzake. Funzo hili tunalipata kwenye dua ya Nabii Yusufu(a.s).



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1302

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa

Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.
Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9.

Soma Zaidi...
tarekh 3
tarekh 3

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija

Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.

Soma Zaidi...