Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Mafunzo kutokana na Vita vya Badri.
Ushindi wa waislamu katika vita unatoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na sio kutokana na ubora wa silaha na wingi wa askari.
Rejea Qur’an (3:123-124), (8:42-45).
Tunajifunza pia namna ya kuwafanyia mateka wa kivita ikiwa ni pamoja na;
- Kuwapatia haki na huduma zote msingi za kimaisha, kibinaadamu na kiutu.
- Kuwalea na kuwafanyia wema na uadilifu kama wanafamilia wengine.
- Kwa mateka wanaoweza kuleta madhara kwa waislamu na Uislamu, ni bora
kuuawa badala ya kuachwa huru kwa kujikomboa.
Rejea Qur’an (8:67-69).
Mwenyezi Mungu (s.w) aliwaadhibu makafiri na kuwanusuru waislamu katika vita vya Badri na hawakuadhibu walipokuwa Makkah kwa sababu walikuwa pamoja na Mtume (s.a.w) na pia walipewa muda wa kutubia.
Rejea Qur’an (8:32-34) na (8:19).
Tunajifunza pia, inafaa nguvu ya kivita kutumika ikibidi katika kuzuia na kuondoa uovu, udhalimu, uonevu na choko choko za maadui.
Rejea Qur’an (8:60) na (60:8-9).
Tunajifunza pia, Uislamu bila ya juhudi za kweli kufanyika na kumwagika damu na kujitoa muhanga ipasavyo, hautasimama katika jamii.
Choko choko na mbinu za maadui dhidi ya Uislamu na waislamu ni zenye kuendelea na hazitaisha kamwe hadi siku ya Qiyama.
Download App Yetu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.