picha

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina


Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.s) aliamuriwa kuwaongoza Bani Israil hadi Palestina. Aliwaongoza kupitia Taberah na Hazeroth hadi kwenye jangwa la Paran. Hapo Nabii Musa(a.s) alituma watu mashuhuri kufanya upelelezi Palestina. Baada ya siku arobaini ujumbe huu ulirejea na taarifa yao waliitolea sehemu iitwayo Kadesh. Taarifa za wajumbe wote ila wawili (Joshua na Caleb) ziliwakatisha tamaa. Hivyo wakagoma kuingia Palestina. Hawakutaka kabisa kutoa nafsi zao muhanga. Bali walitaka Allah(s.w) awatengenezee kila kitu wao waje tu kuvuna na kufaidi matunda. Kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:




β€œ(Musa(a.s) akasema): "Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi (nchi) iliyotakaswa ambayo Mwenyezi Mungu amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika". Wakasema: "Ewe Musa! Huko kuna watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka watoke humo, wakitoka humo hapo tutaingia". Watu wawili miongoni mwa wale waliomwogopa (Allah) ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha, walisema (kuwaambaia wenzao). "Waingilieni katika hilo lango (la nchi yao); maana mtakapo waingilia hapo, kwa yakini nyinyi mtashinda. Na tegemeeni juu ya Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini". Wakaema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane, sisi tutakaa hapa (kungojea nini litakalokuwa)" (5:21-24).



Baada ya ukaidi huu Nabii Musa(a.s) hakuwa na la kufanya tena bali kuleta dua ifuatayo:

(Musa) akasema: "Mola wangu! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu; basi tutenge na hawa mafasiki".(5:25)

Allah(s.w) aliwatia adabu kwa ukaidi wao; wakawa wanatangatanga Jangwani kwa muda wa miaka arobaini.

(Mwenyezi Mungu) akasema: "Basi wameharamishiwa (ardhi) hiyo kwa (muda wa) miaka arobaini, watatangatanga (mumu humu) ardhini (jangwani muda wote huo). Basi usihuzunike juu ya watu maasi" (5:26).



Basi Mayahudi hawa wakadumu kuhangaika majangwani bila kupumua. Kizazi kipya kilichochipuka baadaye wakawa na mwendo mzuri na utii. Wakapigana na majabari wa Palestina na wakatawala wao.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 769

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰3 web hosting    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi

Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Soma Zaidi...
Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maandalizi ya Kimafunzo aliyoandaliwa Mtume Muhammad

(i) Suratul- β€˜Alaq (96:1-5)β€œSoma kwa jina la Mola wako aliyeumba Aliyemuumba mwanaadamu kwa β€˜alaq.

Soma Zaidi...