Navigation Menu



Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina


Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.s) aliamuriwa kuwaongoza Bani Israil hadi Palestina. Aliwaongoza kupitia Taberah na Hazeroth hadi kwenye jangwa la Paran. Hapo Nabii Musa(a.s) alituma watu mashuhuri kufanya upelelezi Palestina. Baada ya siku arobaini ujumbe huu ulirejea na taarifa yao waliitolea sehemu iitwayo Kadesh. Taarifa za wajumbe wote ila wawili (Joshua na Caleb) ziliwakatisha tamaa. Hivyo wakagoma kuingia Palestina. Hawakutaka kabisa kutoa nafsi zao muhanga. Bali walitaka Allah(s.w) awatengenezee kila kitu wao waje tu kuvuna na kufaidi matunda. Kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:




“(Musa(a.s) akasema): "Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi (nchi) iliyotakaswa ambayo Mwenyezi Mungu amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika". Wakasema: "Ewe Musa! Huko kuna watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka watoke humo, wakitoka humo hapo tutaingia". Watu wawili miongoni mwa wale waliomwogopa (Allah) ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha, walisema (kuwaambaia wenzao). "Waingilieni katika hilo lango (la nchi yao); maana mtakapo waingilia hapo, kwa yakini nyinyi mtashinda. Na tegemeeni juu ya Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini". Wakaema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane, sisi tutakaa hapa (kungojea nini litakalokuwa)" (5:21-24).



Baada ya ukaidi huu Nabii Musa(a.s) hakuwa na la kufanya tena bali kuleta dua ifuatayo:

(Musa) akasema: "Mola wangu! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu; basi tutenge na hawa mafasiki".(5:25)

Allah(s.w) aliwatia adabu kwa ukaidi wao; wakawa wanatangatanga Jangwani kwa muda wa miaka arobaini.

(Mwenyezi Mungu) akasema: "Basi wameharamishiwa (ardhi) hiyo kwa (muda wa) miaka arobaini, watatangatanga (mumu humu) ardhini (jangwani muda wote huo). Basi usihuzunike juu ya watu maasi" (5:26).



Basi Mayahudi hawa wakadumu kuhangaika majangwani bila kupumua. Kizazi kipya kilichochipuka baadaye wakawa na mwendo mzuri na utii. Wakapigana na majabari wa Palestina na wakatawala wao.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 371


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

MAMA YAKE MTUME MUHAMMAD (S.A.W) ANAMLEA MTUME MUHAMAD AKIWA NA UMRI WA MIAKA MINNE (4)
KULELEWA NA MAMA YAKE ALIPOFIKA MIAKA MINNEMtume (s. Soma Zaidi...

Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9. Soma Zaidi...

Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...

Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...

Mapambano ya waislamu dhidi ya Makabila ya kiarabu wakati wa Mtume
Soma Zaidi...

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah
Kuanzishwa kwa Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

Mtume amezaliwa mwaka gani?
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...

Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7 Soma Zaidi...