Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina

Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina


Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.s) aliamuriwa kuwaongoza Bani Israil hadi Palestina. Aliwaongoza kupitia Taberah na Hazeroth hadi kwenye jangwa la Paran. Hapo Nabii Musa(a.s) alituma watu mashuhuri kufanya upelelezi Palestina. Baada ya siku arobaini ujumbe huu ulirejea na taarifa yao waliitolea sehemu iitwayo Kadesh. Taarifa za wajumbe wote ila wawili (Joshua na Caleb) ziliwakatisha tamaa. Hivyo wakagoma kuingia Palestina. Hawakutaka kabisa kutoa nafsi zao muhanga. Bali walitaka Allah(s.w) awatengenezee kila kitu wao waje tu kuvuna na kufaidi matunda. Kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:




β€œ(Musa(a.s) akasema): "Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi (nchi) iliyotakaswa ambayo Mwenyezi Mungu amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika". Wakasema: "Ewe Musa! Huko kuna watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka watoke humo, wakitoka humo hapo tutaingia". Watu wawili miongoni mwa wale waliomwogopa (Allah) ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha, walisema (kuwaambaia wenzao). "Waingilieni katika hilo lango (la nchi yao); maana mtakapo waingilia hapo, kwa yakini nyinyi mtashinda. Na tegemeeni juu ya Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini". Wakaema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane, sisi tutakaa hapa (kungojea nini litakalokuwa)" (5:21-24).



Baada ya ukaidi huu Nabii Musa(a.s) hakuwa na la kufanya tena bali kuleta dua ifuatayo:

(Musa) akasema: "Mola wangu! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu; basi tutenge na hawa mafasiki".(5:25)

Allah(s.w) aliwatia adabu kwa ukaidi wao; wakawa wanatangatanga Jangwani kwa muda wa miaka arobaini.

(Mwenyezi Mungu) akasema: "Basi wameharamishiwa (ardhi) hiyo kwa (muda wa) miaka arobaini, watatangatanga (mumu humu) ardhini (jangwani muda wote huo). Basi usihuzunike juu ya watu maasi" (5:26).



Basi Mayahudi hawa wakadumu kuhangaika majangwani bila kupumua. Kizazi kipya kilichochipuka baadaye wakawa na mwendo mzuri na utii. Wakapigana na majabari wa Palestina na wakatawala wao.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 402

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema

Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...
Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...
Malezi ya mtume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma

Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.

Soma Zaidi...
Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...