Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.
Baada ya matukio haya ndipo Musa(a.s) aliamuriwa kuwaongoza Bani Israil hadi Palestina. Aliwaongoza kupitia Taberah na Hazeroth hadi kwenye jangwa la Paran. Hapo Nabii Musa(a.s) alituma watu mashuhuri kufanya upelelezi Palestina. Baada ya siku arobaini ujumbe huu ulirejea na taarifa yao waliitolea sehemu iitwayo Kadesh. Taarifa za wajumbe wote ila wawili (Joshua na Caleb) ziliwakatisha tamaa. Hivyo wakagoma kuingia Palestina. Hawakutaka kabisa kutoa nafsi zao muhanga. Bali walitaka Allah(s.w) awatengenezee kila kitu wao waje tu kuvuna na kufaidi matunda. Kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:
“(Musa(a.s) akasema): "Enyi watu wangu! Ingieni katika hiyo ardhi (nchi) iliyotakaswa ambayo Mwenyezi Mungu amekuandikieni. Wala msirudi nyuma, msije mkawa wenye kukhasirika". Wakasema: "Ewe Musa! Huko kuna watu majabari. Nasi hatutaingia huko mpaka watoke humo, wakitoka humo hapo tutaingia". Watu wawili miongoni mwa wale waliomwogopa (Allah) ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha, walisema (kuwaambaia wenzao). "Waingilieni katika hilo lango (la nchi yao); maana mtakapo waingilia hapo, kwa yakini nyinyi mtashinda. Na tegemeeni juu ya Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni wenye kuamini". Wakaema: Ewe Musa! Sisi hatutaingia humo kamwe maadamu wao wamo humo. Basi nenda wewe na Mola wako mkapigane, sisi tutakaa hapa (kungojea nini litakalokuwa)" (5:21-24).
Baada ya ukaidi huu Nabii Musa(a.s) hakuwa na la kufanya tena bali kuleta dua ifuatayo:
(Musa) akasema: "Mola wangu! Hakika mimi similiki ila nafsi yangu na ndugu yangu; basi tutenge na hawa mafasiki".(5:25)
Allah(s.w) aliwatia adabu kwa ukaidi wao; wakawa wanatangatanga Jangwani kwa muda wa miaka arobaini.
(Mwenyezi Mungu) akasema: "Basi wameharamishiwa (ardhi) hiyo kwa (muda wa) miaka arobaini, watatangatanga (mumu humu) ardhini (jangwani muda wote huo). Basi usihuzunike juu ya watu maasi" (5:26).
Basi Mayahudi hawa wakadumu kuhangaika majangwani bila kupumua. Kizazi kipya kilichochipuka baadaye wakawa na mwendo mzuri na utii. Wakapigana na majabari wa Palestina na wakatawala wao.
Umeionaje Makala hii.. ?
LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
Soma Zaidi...Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a.
Soma Zaidi...Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.
Soma Zaidi...KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.
Soma Zaidi...Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a.
Soma Zaidi...Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.
Soma Zaidi...