Kuangamizwa kwa Watu wa Lut(a.s) watu wa Sodoma na Gomora

Watu wa Lut(a.

Kuangamizwa kwa Watu wa Lut(a.s) watu wa Sodoma na Gomora

Kuangamizwa kwa Watu wa Lut(a.s)


Watu wa Lut(a.s) walipokataa kabisa kuonyeka kwa nasaha na maonyo ya Nabii Lut(a.s) na badala yake wakazidi kushabikia machafu na kupania kuwafanyia ubaya waumini, Allah(s.w) alipitisha hukumu yake ya kuwanusuru waumini na kuwaangamiza makafiri.




(Wale wajumbe) wakasema: “Ewe Lut! Sisi ni wajumbe wa Mola wako (Malaika). Hawatakufikia (kwa baya lolote). Na ondoka pamoja na watu wako katika sehemu ya pingapinga la usiku.Wala yoyote miongoni mwenu asitazame nyuma. Isipokuwa mke wako (mwanamke mbaya huyo hatakufuata). Naye utampata msiba utakaowapata hao. Hakika miadi yao ni asubuhi. Jee, asubuhi si karibu tu? (Basi tuliza moyo wako. Umekwishafika wakatiwao wa kuangamizwa).(11:81)




Basi ilipofika amri yetu, tulifanya (ardhi hiyo iwe juu chini); juu yake kuwa chini yake, na tukawateremshia mvua ya changarawe za udongo mgumu (wa motoni uliyokamatana). (11:82) (Changarawe) zilizotiwa alama kwa Mola wako (kila moja kuwa ya mtu fulani). Na (adhabu) hii haiko mbali na madhalimu (wengine kama hawa watu wa umma huu wanaofanya machafu haya). (11:83)



Jeshi la Allah lililotumika kuwaangamiza watu wa Lut(a.s) ni mvua ya changarawe kutokea motoni na kisha ardhi ikapinduliwa juu – chini.

Na majeshi ya mbingu na ardhi ni ya Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima. (48:7)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2276

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?

Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri?

Soma Zaidi...
Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11

Soma Zaidi...