Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)

Baada ya Nabii Salih(a.

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)


Baada ya Nabii Salih(a.s) kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa ufasaha na kwa uwazi, watu wake waligawanyika makundi mawili.

Wachache wao waliamini, wengi katika hao wakiwa dhaifu.Wengi wao wakiongozwa na wakuu wa jamii walikufuru. Makafiri wa Kithamud waliukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.s) kwa sababu zifuatazo:



Kwanza, Walimuona Salih(a.s) kuwa ni mwongo, kuwa hapana cha kuwepo Allah wala adhabu kutoka kwake.

Wakasema wale waliotakabari 'Sisi tunayakataa yale mnayoyaamini. Na wakamtumbua (wakamuua) yule ngamia na wakaasi amri ya Mola wao na wakasema: 'Ee Salih! Tuletee unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa Mitume. (7:76-77)



Wakamchinja. Basi (Salih) akasema: 'Stareheni katika mji wenu huu (muda wa) siku tatu (tu, kisha mtaadhibiwa); hiyo ni ahadi isiyokuwa ya uwongo.' (11:65)



Pili,hawakuwa tayari kuacha miungu ya Babu zao:

Wakasema: 'Ewe Salih! Bila shaka ulikuwa unayetarajiwa (kheri) kwetu kabla ya haya (Sasa umeharibika). Oh! Unatukataza kuabudu waliowaabudu baba zetu? Na hakika sisi tumo katika shaka inayotusugua (katika nyoyo zetu) kwa haya unayotuitia.' (11:62)



Tatu, walimuona Salih(a.s) kama mtu aliyerogwa na wakamdai kuleta muujiza:

Wakasema 'Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa (wakakosa akili).' 'Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi; basi lete muujiza ikiwa ni miongoni mwa wasemao kweli.' (26:153-154)





Nne, walidai kuwa Salih(a.s) na wale waliomuamini pamoja naye wameleta nuksi katika nchi kwa kule kuikataa kwao miungu ya masanamu. Wakasema: 'Tumepata bahati mbaya, (ukorofi) kwa Sababu yako na kwa Sababu ya wale walio pamoja nawe.' Akasema: 'Ukorofi wenu uko kwa Mwenyezi Mungu (kwa ajili ya ubaya wenu;) lakini nyinyi ni watu mnaojaribiwa (na Mwenyezi Mungu kuwa mtafuata au hamfuati).' (27:47)



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 155


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

AINA ZA HADITHI
Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi. Soma Zaidi...

SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Mapambano Dhidi ya Maadui wa Dola ya Kiislamu
1. Soma Zaidi...

NAMNA YA KUSWALI: NIA YA SWWALA, NA KUPIGA TAKBIRA (yaani kusema Allah akbar)
Mtume (s. Soma Zaidi...

Nadharia ya uchumi kiislamu
1. Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe). Soma Zaidi...

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Hadithi inayokataza bidaa (bid's) uzushi katika dini
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': ': ' ' ' ' ' ' ' "... Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

kuletewa ujumbe
(c)Kuletewa Ujumbe na Malaika kutoka kwa Allah (s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISA
Soma Zaidi...

Namna ya kumuosha maiti hatua kwa hatua, nguzo na sunnah za josho la maiti
1. Soma Zaidi...