HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)

Ismail(a.

HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)

HISTORIA YA NABII ISMAIL(A.S)


Ismail(a.s) ni mtoto wa kwanza wa Mtume Ibrahim(a.s.). Alizaliwa wakati uzee umekwishamfikia Ibrahim(a.s). Kama Qur’an inavyobainisha, katika umri huo wa uzeeni, MtumeIbrahiim(a.s) alimuomba Mola wake ampe mtoto mwema atakaendeleza harakati za Kiislamu.



“Ee Mola wangu! Nipe (mtoto awe) miongoni mwa watenda mema.” Ndipo tukampa habari njema ya (kuwa atapata) mtoto mpole. (Basi akapata. Naye ndiye Nabii Ismail).” (37:100-101).



Mtume Ibrahim(a.s.) aliletewa mitihani migumu miwili juu ya mtoto huyu. Mosi ni kule kuamriwa kumwacha yeye pamoja na mama yake katika bonde kavu lisilo na watu wala maji. Hilo lilikuwa bonde la Makka. Maji ya kisima zamzam yaliyo katika Msikiti wa Makka, aliyabubujisha Allah(s.w) kwa ajili ya Ismail na mama yake. Chem-chem hiyo imedumu hadi leo. Aidha, vilima vya Safa na Marwa vimepata umaarufu na kuwa miongoni mwa alama muhimu katika Uislamu, kutokana na kitendo cha mama yake Ismail Hajirah, kukimbia baina ya vilima hivyo katika jitihada za kumtafutia mwanae Ismail maji.



Mtihani mwingine alioupata MtumeIbrahiim(a.s) juu ya Ismail(a.s) ni kule kuamrishwa amchinje. Huu haukuwa ni mtihani kwa baba tu, lakini pia mtoto Ismail(a.s). Hebu fikiri ungekuwa katika hali gani, kama ungekuwa mahali pa Ismail(a.s). Baba yako anakwambia ameamrishwa na Allah(s.w.) akuchinje! Hakika ni mtihani mgumu ila kwa wale wanaonyenyekea kikweli kweli kwa Muumba wao.



Qur’an yatufahamisha kuwa Ismail alikuwa mpole na mnyenyekevu kwa Mola wake. Kwa hiyo hakusita kutoa nafsi yake kwa ajili ya Muumba wake. Bali alimhimiza baba yake amchinje kama Allah(s.w) alivyomuamrisha.



Basi alipofikia (makamu ya) kwenda na kurudi pamoja naye akamwambia: “Ee mwanangu! Hakika nimeona katika ndoto ya kwamba ninakuchinja. (Na ndoto ya Mitume ni Wahayi). Basi fikiri,waonaje?”Akasema:“Ee baba yangu! Fanya unayoamrish wa, utanikuta Inshallah miongoni mwa wanaosubiri”.(37:102).



Utii na unyenyekevu huu wa Nabii Ismail(a.s) ni kielelezo muhimu kwetu. Kwamba, amri ya Allah(s.w) ni lazima itiiwe kwa gharama yoyote ile ikiwa ni pamoja na roho zetu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 4323

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...
Kusingiziwa Nabii Sulaiman Uchawi

Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.

Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata

Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.

Soma Zaidi...
Historia ya Dhulqarnain

Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”.

Soma Zaidi...
Historia ya Al-Khidhri

Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an.

Soma Zaidi...