Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.s). Pamoja na Nabii Nuhu(a.s) kuahidiwa kuwa watu wake wa nyumbani watakuwa miongoni mwa watakaookolewa na gharka, mtoto wake alikataa kuingia kwenye jahazi(safina) na akawa ni miongoni mwa wenye kuangamia kama tunavyo jifunza katika aya zifuatazo.




Na akasema(Nuhu):”Pandeni humo, kwa jina la Mwenyezi Mungu kuwe kwenda kwake na kusimamma kwake. Hakika Mola wangu ni mwingi wa kusamehe na mwingi wa kurehemu.


Ikawa hiyo (jahazi) inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuhu akamwita mwanawe aliyekuwa mbali amekataa kuingia jahazini: “Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri”. Na akasema (huyo mtoto)” “Nitaukimbilia Mlima utakaonilinda na maji” Akasema(Nuhu): “Hakuna leo wa kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu isipokuwa yule atakayemrehemu (Mwenyezi Mungu).” Mara mawimbi yakaingia baina yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa. (11:41-43)



Baada ya Gharika

Baada ya gharika kuisha, Nabii Nuhu(a.s) Ilibidi amuelekee Mola wake kutaka kujua ni vipi mwanawe amekuwa miongoni mwa walioangamia.




Na Nuhu alimuomba Mola wake (alipomuona mwanawe anaangamia) akasema: Ewe Mola wangu! Mwanangu ni katika watu wa nyumbani kwangu (mbona anaangamia)? Na hakika ahadi Yako ni haki; nawe ni mwenye haki kuliko mahakimu (wote).”Akasema (Mwenyezi Mungu): “Ewe Nuhu! Huyu si miongoni mwa watu wako. Yeye ni (mwenye) mwenendo usiokuwa mzuri. Basi usiniombe ambayo huyajui. Mimi nakunasihi usiwe miongoni mwa wajinga.” (Nuhu) Akasema: Ee Mola wangu! Mimi najikinga kwako nisije kukuombatena nisiyoyajua; na kama hutanisamehe na kunirehemu nitakuwa miongoni mwa watakaopata khasara.”(11:45-47)



Pia tunahamishwa juu ya kuangamia mke wa Nuhu(a.s) katika aya ifuatayo:




Mwenyezi Mungu amepiga (anapiga)mfano wa wale wabaya waliokufuru, ni mkewe Nuhu na mkewe Luti. Walikuwa chini ya waja wetu wema wawili hao miongoni mwa waja wetu (wema)’ lakini(wanawake hao), waliwafanyia khiana (waume zao watukufu hao) na (waume zao hao) hawakuweza kuwasaidia



chochote mbele ya Mwenyezi Mungu na ikasemwa: “Uingieni
Moto pamoja na hao wanaouingia.” (66:10)



Kuangamia kwa mtoto na mke wa Nuhu(a.s) pamoja na mke wa Lut(a.s) tunajifunza kuwa mtu hataokoka na ghadhabu ya Allah(s.w) kutokana a unasaba alioonao na watu wema na wala hata faidika na malipo ya amali njema walizofanya wengine. Kinyume chake hataadhibiwa mtu mwema kwa kuwa na unasaba na watu waovu maadamu anawafikishia ujumbe na wakamkanusha kama tunavyopigiwa mfano wa mke wa firaun,aliyekuwa mcha-mungu.




Na Mwenyezi Mngu amepiga, (anapiga) mfano wa wale walioamini kweli, ni mkewe Firauni, aliposema; “Ee Mola wangu! Nijengee nyumba Peponi karibu yako na uniokoe na Firauni na amali zake (mbovu), na Niokoe na watu madhalimu”(66:11)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2552

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Vita vya badri

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema

Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...
Mtume kumuoa bi khadija

Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 15. Hapa utajifunza kuhusu chimbuko la ndoa ya Mtume s.a.w na bi Khadija.

Soma Zaidi...
Historia ya Dhulqarnain

Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”.

Soma Zaidi...
Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)

Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza.

Soma Zaidi...
Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu

Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s.

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...
Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...