Kuibuka kwa kundi la khawarij baada ya vita vya Siffin

Kuibuka kwa kundi la khawarij baada ya vita vya Siffin

Kuibuka kwa Khawarij


Baada ya makubaliano, Ali aliwatangazia makubaliano haya wapiganaji wake. Lakini ndugu wawili wa kabila la Azza walisimama kupinga suluhu kwa hoja kuwa wanazo hukumu za Mwenyezi Mungu katika Qurโ€™an hivyo hawahitaji wasuluhishi. Watu wengi waliunga mkono rai hii na kufikia 12,000. Wao hawakurudi Kufa, walipiga kambi mahali paitwapo Harorah. Walimteua Sheikh bin Rabi kuwa kamanda wao na Abdullah bin Kawa kuwa Imam wa kuongoza Swala. Walitangaza imani yao ambayo ilikuwa:


โ€œBaโ€™iyah iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu, yeye tu ndiye wa kutiiwa. Kuhubiri mema na kukataza mabaya. Hakuna Khalifa au Amir. wote Ali na Muawiya wana makosa, Muawiyah anamakosa kwa kutomtii Ali, na Ali anamakosa kwa kukubaliana na Muawiyah juu ya suluhu. tutaposhika mamlaka tutaanzisha mfumo wa maisha ya jamii uliojengwa juu ya Qurโ€™anโ€.


Ali aliporudi Kufa alimtuma Abdullah bin Abbas, Harorah kuzungumza na Khawarij. Aliweza kuwavuta na wakakubaliana na Khalifa baada ya mazungumzo ya muda mrefu. Hata hivyo kukubali huku kulikuwa kwa muda tu.





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 934

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Shukurani za Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Allah(s.w)

Kwa neema hii ya kuruzukiwa watoto wawili - Ismail na Is- haqa(a.

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee โ€˜Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...