picha

Kuibuka kwa kundi la khawarij baada ya vita vya Siffin

Kuibuka kwa kundi la khawarij baada ya vita vya Siffin

Kuibuka kwa Khawarij


Baada ya makubaliano, Ali aliwatangazia makubaliano haya wapiganaji wake. Lakini ndugu wawili wa kabila la Azza walisimama kupinga suluhu kwa hoja kuwa wanazo hukumu za Mwenyezi Mungu katika Qur’an hivyo hawahitaji wasuluhishi. Watu wengi waliunga mkono rai hii na kufikia 12,000. Wao hawakurudi Kufa, walipiga kambi mahali paitwapo Harorah. Walimteua Sheikh bin Rabi kuwa kamanda wao na Abdullah bin Kawa kuwa Imam wa kuongoza Swala. Walitangaza imani yao ambayo ilikuwa:


“Ba’iyah iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu, yeye tu ndiye wa kutiiwa. Kuhubiri mema na kukataza mabaya. Hakuna Khalifa au Amir. wote Ali na Muawiya wana makosa, Muawiyah anamakosa kwa kutomtii Ali, na Ali anamakosa kwa kukubaliana na Muawiyah juu ya suluhu. tutaposhika mamlaka tutaanzisha mfumo wa maisha ya jamii uliojengwa juu ya Qur’an”.


Ali aliporudi Kufa alimtuma Abdullah bin Abbas, Harorah kuzungumza na Khawarij. Aliweza kuwavuta na wakakubaliana na Khalifa baada ya mazungumzo ya muda mrefu. Hata hivyo kukubali huku kulikuwa kwa muda tu.





                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1324

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 web hosting    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Mtume Muhammad s.a. w amelewa na Baba yake mdogo

Historia na sura ya Mtume Muhammad, sehemu ya 10.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”.

Soma Zaidi...
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...
Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7

Soma Zaidi...