Kuibuka kwa Khawarij
Baada ya makubaliano, Ali aliwatangazia makubaliano haya wapiganaji wake. Lakini ndugu wawili wa kabila la Azza walisimama kupinga suluhu kwa hoja kuwa wanazo hukumu za Mwenyezi Mungu katika Qur’an hivyo hawahitaji wasuluhishi. Watu wengi waliunga mkono rai hii na kufikia 12,000. Wao hawakurudi Kufa, walipiga kambi mahali paitwapo Harorah. Walimteua Sheikh bin Rabi kuwa kamanda wao na Abdullah bin Kawa kuwa Imam wa kuongoza Swala. Walitangaza imani yao ambayo ilikuwa:
“Ba’iyah iwe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu tu, yeye tu ndiye wa kutiiwa. Kuhubiri mema na kukataza mabaya. Hakuna Khalifa au Amir. wote Ali na Muawiya wana makosa, Muawiyah anamakosa kwa kutomtii Ali, na Ali anamakosa kwa kukubaliana na Muawiyah juu ya suluhu. tutaposhika mamlaka tutaanzisha mfumo wa maisha ya jamii uliojengwa juu ya Qur’an”.
Ali aliporudi Kufa alimtuma Abdullah bin Abbas, Harorah kuzungumza na Khawarij. Aliweza kuwavuta na wakakubaliana na Khalifa baada ya mazungumzo ya muda mrefu. Hata hivyo kukubali huku kulikuwa kwa muda tu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Historia na sura ya Mtume Muhammad, sehemu ya 10.
Soma Zaidi...“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”.
Soma Zaidi...Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.
Soma Zaidi...Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7
Soma Zaidi...