Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Musa(a.

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu


Musa(a.s) alizaliwa wakati bado msako unafanywa na askari wa Firauni kumwua kila mtoto wa kiume wa Kiisrail anayezaliwa. Kwa rehema zake Allah(s.w) mama yake Musa alijifungua bila kutambulika kwa askari wa Firauni. Na ili kumlinda zaidi Allah(s.w) alimteremshia Wahy mama yake Musa.




Ya kwamba mtie sandukuni, kisha litie mtoni, na mto utamtupa ufukoni ili amchukue adui yangu na adui yake (amlee kwa vizuri Naye ni Firaun). Na nimekutilia mapenzi yatokanayo kwangu (ili upendwe na watu wote), na ili ulelewe machoni mwangu.(20:39)



Baada ya kumtupa mtoni, mama yake akamtuma dada yake Musa kufuatilia:

Akamwambia dada yake: 'Mfuate'. Basi yeye akamwangalia kwa mbali bila wao kumjua (28:11)



Kitoto Musa kiliokotwa na kufikishwa kwa Firaun. Mkewe Firaun akamrai mumewe kuwa wasimuue bali wamfanye mtoto wao wa kulea.



Na mkewe Firauni akasema (Kumwambia mumewe) 'Usimuuwe, atakuwa kiburudisho cha macho kwangu na kwako; na msimuuwe;huwenda atatunufaisha, au tumpange kuwa mtoto wetu,walisema haya hali ya kuwa hawatambui(kuwa atakuwa adui yao)'(28:9)



Watu wa Firauni walipomwokota Musa bila shaka walitambua kuwa ni mtoto wa Kiisrail na walimpeleka kwa Firauni ili auawe kama watoto wengine Wakiisrail. Lakini mke wa Firauni alivutiwa na uzuri wa mtoto Musa. Ambaye kwa kweli Allah(s.w) alimfanya awe ni mwenye kupendeza machoni kwa watu. Allah(s.w) Ajaalia Musa(a.s) Kunyonyeshwa na Mama Yake Mzazi



Kwa uwezo wake, Mwenyezi Mungu aliharamisha Musa asinyonyeshwe na yeyote yule isipokuwa mama yake. Hivyo, dada yake Musa alijitokeza nyumbani kwa Firauni na kupendekeza:

'.........Basi akasema: Je nikuonesheni watu wa nyumba watakaomlea kwa ajili yenu, na pia watakuwa wema kwake? (28:12)



Dada yake Musa(a.s) alimpendekeza mama yake ambaye Firauni hawakumjua kuwa ndiye mama mzazi wa Nabii Musa(a.s). Ombi hilo lilikubaliwa na Musa(a.s)alirejeshwa kwa mama yake:



Basi tukamrejesha kwa mama yake ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike; na ajue ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli, lakini watu wengi hawajui (28:13)


Allah(s.w) Amruzuku Musa(a.s) Elimu


Ili kuweza kutekeleza jukumu la kutetea haki za binadamu na kuwaongoza watu katika njia iliyonyooka, Mwenyezi Mungu akamjaalia Musa elimu ya kutosha na akili yenye upeo mkubwa wa kupembua mambo. Tunafahamishwa kuwa:



Na Musa alipofikia baleghe yake na kustawi, tulimpa akili na elimu, na hivi ndivyo tunavyowalipa watu wema (28:14)



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 517


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu
Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu. Soma Zaidi...

Kulaaniwa Bani Israil
Pamoja na kuteuliwa na Allah(s. Soma Zaidi...

JIFUNZE FIQH
Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka. Soma Zaidi...

HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU
' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' ' ' ' "' ' ' ' ' [ ' ' '?... Soma Zaidi...

DARSA LA KUJIFUNZA KUHUSU QURAN NA SUNNAH
Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 03
Soma Zaidi...

DUA 41 - 50
41. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa surat al-Fiil
SURAT AL-FIILSura hii imeteremshwa Makkah na ina Aya Sita pamoja na Basmallah. Soma Zaidi...

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri
Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII NUHU
Soma Zaidi...

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga
Soma Zaidi...

NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU
Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s. Soma Zaidi...