Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Musa(a.

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu


Musa(a.s) alizaliwa wakati bado msako unafanywa na askari wa Firauni kumwua kila mtoto wa kiume wa Kiisrail anayezaliwa. Kwa rehema zake Allah(s.w) mama yake Musa alijifungua bila kutambulika kwa askari wa Firauni. Na ili kumlinda zaidi Allah(s.w) alimteremshia Wahy mama yake Musa.




Ya kwamba mtie sandukuni, kisha litie mtoni, na mto utamtupa ufukoni ili amchukue adui yangu na adui yake (amlee kwa vizuri Naye ni Firaun). Na nimekutilia mapenzi yatokanayo kwangu (ili upendwe na watu wote), na ili ulelewe machoni mwangu.(20:39)



Baada ya kumtupa mtoni, mama yake akamtuma dada yake Musa kufuatilia:

Akamwambia dada yake: “Mfuate”. Basi yeye akamwangalia kwa mbali bila wao kumjua (28:11)



Kitoto Musa kiliokotwa na kufikishwa kwa Firaun. Mkewe Firaun akamrai mumewe kuwa wasimuue bali wamfanye mtoto wao wa kulea.



Na mkewe Firauni akasema (Kumwambia mumewe) “Usimuuwe, atakuwa kiburudisho cha macho kwangu na kwako; na msimuuwe;huwenda atatunufaisha, au tumpange kuwa mtoto wetu,walisema haya hali ya kuwa hawatambui(kuwa atakuwa adui yao)”(28:9)



Watu wa Firauni walipomwokota Musa bila shaka walitambua kuwa ni mtoto wa Kiisrail na walimpeleka kwa Firauni ili auawe kama watoto wengine Wakiisrail. Lakini mke wa Firauni alivutiwa na uzuri wa mtoto Musa. Ambaye kwa kweli Allah(s.w) alimfanya awe ni mwenye kupendeza machoni kwa watu. Allah(s.w) Ajaalia Musa(a.s) Kunyonyeshwa na Mama Yake Mzazi



Kwa uwezo wake, Mwenyezi Mungu aliharamisha Musa asinyonyeshwe na yeyote yule isipokuwa mama yake. Hivyo, dada yake Musa alijitokeza nyumbani kwa Firauni na kupendekeza:

“.........Basi akasema: Je nikuonesheni watu wa nyumba watakaomlea kwa ajili yenu, na pia watakuwa wema kwake? (28:12)



Dada yake Musa(a.s) alimpendekeza mama yake ambaye Firauni hawakumjua kuwa ndiye mama mzazi wa Nabii Musa(a.s). Ombi hilo lilikubaliwa na Musa(a.s)alirejeshwa kwa mama yake:



Basi tukamrejesha kwa mama yake ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike; na ajue ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli, lakini watu wengi hawajui (28:13)


Allah(s.w) Amruzuku Musa(a.s) Elimu


Ili kuweza kutekeleza jukumu la kutetea haki za binadamu na kuwaongoza watu katika njia iliyonyooka, Mwenyezi Mungu akamjaalia Musa elimu ya kutosha na akili yenye upeo mkubwa wa kupembua mambo. Tunafahamishwa kuwa:



Na Musa alipofikia baleghe yake na kustawi, tulimpa akili na elimu, na hivi ndivyo tunavyowalipa watu wema (28:14)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2200

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga

Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba.

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake.

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Musa(a.s)Kupewa Utume Rasmi

Musa alipotimiza muda, alifunga safari na ahali zake kurejea Misri.

Soma Zaidi...