Musa(a.s) Ahamia Madiani

Mchana wa siku moja Musa(a.

Musa(a.s) Ahamia Madiani

Musa(a.s) Ahamia Madiani


Mchana wa siku moja Musa(a.s) alimuona mtu wa Firauni amemuelemea Muisrail akimtwanga makonde mazito. Musa alichukizwa na kitendo kile, hivyo alipoombwa msaada alijikuta amemtwika Mmisri huyo ngumi nzito na kumuuwa palepale. Hapo Musa(a.s) akashituka na kuleta toba:



Mola wangu! Bila shaka nimedhulumu nafsi yangu, basi nisamehe; naye (Allah) akamsamehe. Kwa hakika yeye ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu. (28:16)

Akasema: Mola wangu! Kwa kuwa umenineemesha, basi sitakuwa kabisa msaidizi wa watu wabaya. (28:17)



Habari ile ya kuuliwa mtu na Musa(a.s) ilifika kwa Firaun na ikatoka shauri kuwa Musa(a.s) akamatwe na kuuliwa. Musa(a.s) alipopata habari za kuaminika kutoka kwa mtu mwema,kuhusu hukumu ile, aliamua kutorokea nchini Madian katika mji awa Al-Bid uliopo kilometa 480 hivi mashariki ya Misr. Alipofika Madian hakuwa na pakwenda bali alijipumzisha kisimani ambapo aliwasaidia wasichana wawili kuwanywesha wanyama wao. Wasichana wale hawakuweza kupigana vikumbo na wanaume katika kunywesha wanyama wao, wakawa tu wanabakia pembeni wanaangalia. Kitendo kile kilimfurahisha Mzee wa Madian na akaagiza Musa(a.s) aitwe ili apate ujira wa kazi ile.



Basi akamjia mmoja katika (wasichana) wale wawili, anakwenda na huku anaona haya, akasema: โ€œBaba yangu anakuita ili akulipe ujira wa kutunyweshea..........(28:25)

Musa alipofika kwa yule mzee alimsimulia hali halisi kuhusu dhulma, ukandamizaji na ukiukwaji wa haki za binadamu uliopo nchini Misri, pamoja na kisa kilichompelekea yeye kuhamia Madiani. Yule mzee akamtuliza Musa(a.s), akasema: Usiogope umekwisha kuokoka na watu madhalimu (28:25)




Akasema: Mimi nataka nikuoze mmoja wapo katika binti zangu hawa wawili kwa kunitumikia miaka minane na kama ukitimiza kumi hiari yako, lakini mimi sitaki kukutaabisha utanikuta Inshaa-Allah miongoni mwa watu wema .(28:27)



Musa(a.s) aliafiki suala hilo, na mmoja katika wale mabinti aliridhia kuolewa na Musa(a.s) kwa mahari ya kutoa nguvukazi:
โ€œAkasema(Musa: โ€œMapatano) hayo yamekwisha kuwa baina yangu na baina yako; muda mmoja wapo nitakaoumaliza, basi nisidhulumumiwe; na Mwenyzi Mungu ni Mlinzi juu ya haya tunayoyasema.โ€(28:28)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1269

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰4 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

tarekh 06

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

Soma Zaidi...
Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qurโ€™an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Historia ya vita vya Muta

hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake

Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s.

Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina

Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.

Soma Zaidi...
Vita vya uhudi

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...