Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri

Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a.

Download Post hii hapa

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri


Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a.s) hawakusilimu,badala yake wakapitisha hukumu ya kumteketeza kwa moto wakasema:

“Mteketezeni kwa moto na muinusuru miungu yenu, ikiwa nyinyi ni watendao jambo.” (21:68)

Allah(s.w) alimnusuru Mtume wake kwa kuuamrisha moto uwe “baridi na salama” kwa Ibrahim:

Tukasema:“Ewe moto! Kuwa baridi na salama juu ya Ibrahimu.” (21:69)

“Basi walitaka kumfanyia vitimbi (vya kumchoma moto) lakini tukawafanya wao kuwa wadhalilifu. Na Tulimuokoa yeye na Lut....... (21:70-71)



Nabii Ibrahiim(a.s) Kuhama Iraq


Nabii Ibrahiim(a.s) pamoja na jitihada zote alizozifanya za kuulingania Uislamu kwa hekima na kwa hoja madhubuti kwa baba yake, Mfalme na jamii kwa ujumla hakupata watu walioamini ila mkewe Sarah na mpwawe Lut(a.s). Kwa hali hiyo, Nabii Ibrahiim(a.s) baada ya kupata idhini ya Mola wake, alihama nchini mwake, Iraq, na kwenda katika nchi nyingine za Mashariki ya kati ili kulingania Uislamu humo. Alianza kuhamia Shamu (Syria).




“Basi Lut akamuamini na akasema (Ibrahiim). Hakika mimi nahamia katika (nchi aliyoniamrisha) Mola wangu, bila shaka yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.” (29:26) Na (Ibrahiim) akasema:Nakwenda. Mola wangu ndiye atakayeniongoza.” (37:99)



Nabii Ibrahiim(a.s) baada ya kuhama Iraq alizizungukia nchi nyingi za Mashiriki ya kati ikiwa ni pamoja na Misri, Palestina, Trans-jordan na Hijaz. Sehemu zote hizi aliweka vituo vya harakati alivyokuwa akivitembelea. Alimuweka mpwa wake, Lut(a.s),katika kituo cha T rans-jordan.Aliporuzukiwa watoto wema aliowaomba,Ismail(a.s) na Is-haq(a.s) aliwaingiza kwenye harakati,na akamfanya Ismail(a.s) mkuu wa kituo Hijaz na Is-haq(a.s) mkuu wa kituo cha Palestina. Allah(s.w) aliwateua viongozi hawa wa vituo vya harakati kuwa Manabii wa sehemu hizo na Mzee Ibrahiim(a.s) akiwa kiongozi wao.



Mji wa Makka katika nchi ya Hijaz alipokuwa akiishi Ismail (a.s), ulifanywa kuwa makao makuu ya harakati za kuhuisha Uislamu. Makka ilianza kutumika rasmi kama kituo kikuu cha harakati pale Mzee Ibrahiim (a.s) walipokamilisha kujenga upya Ka’abah na Allah(s.w) kumuamrisha awatangazie watu kuja kuhiji pale kila mwaka.




“Na Ibrahiim alipoinua kuta za nyumba (hii ya Al-Ka’abah) na Ismail (pia) (wakaomba wakasema:) “Ee Mola wetu! Tutakabalie (amali yetu hii ya kujenga huu msikiti). Hakika wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.” (2:127)




Na (kumbuka) tulipomkalisha Ibrahimu mahali penye ile Nyumba (takatifu na tukamwambia): “Usinishirikishe na chochote na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya waizungukao na wanaokaa hapo (kufanya ibada yao) na wanaorukuu na kusujudu, (wanaosali).” Na (tukamwambia) “Utangaze kwa watu habari za Hija, watakujia, (wengine) kwa miguu na (wengine) juu ya kila mnyama aliyekonda (kwa machofu ya njiani) wakija kutoka katika kila njia ya mbali. (22:26-27)



                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 911

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Vita vya uhudi
Vita vya uhudi

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Maana ya kusimamisha uislamu katika dini

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Soma Zaidi...
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA

KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.

Soma Zaidi...
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Soma Zaidi...