Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a.
Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a.s) hawakusilimu,badala yake wakapitisha hukumu ya kumteketeza kwa moto wakasema:
“Mteketezeni kwa moto na muinusuru miungu yenu, ikiwa nyinyi ni watendao jambo.” (21:68)
Allah(s.w) alimnusuru Mtume wake kwa kuuamrisha moto uwe “baridi na salama” kwa Ibrahim:
Tukasema:“Ewe moto! Kuwa baridi na salama juu ya Ibrahimu.” (21:69)
“Basi walitaka kumfanyia vitimbi (vya kumchoma moto) lakini tukawafanya wao kuwa wadhalilifu. Na Tulimuokoa yeye na Lut....... (21:70-71)
Nabii Ibrahiim(a.s) pamoja na jitihada zote alizozifanya za kuulingania Uislamu kwa hekima na kwa hoja madhubuti kwa baba yake, Mfalme na jamii kwa ujumla hakupata watu walioamini ila mkewe Sarah na mpwawe Lut(a.s). Kwa hali hiyo, Nabii Ibrahiim(a.s) baada ya kupata idhini ya Mola wake, alihama nchini mwake, Iraq, na kwenda katika nchi nyingine za Mashariki ya kati ili kulingania Uislamu humo. Alianza kuhamia Shamu (Syria).
“Basi Lut akamuamini na akasema (Ibrahiim). Hakika mimi nahamia katika (nchi aliyoniamrisha) Mola wangu, bila shaka yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.” (29:26) Na (Ibrahiim) akasema:Nakwenda. Mola wangu ndiye atakayeniongoza.” (37:99)
Nabii Ibrahiim(a.s) baada ya kuhama Iraq alizizungukia nchi nyingi za Mashiriki ya kati ikiwa ni pamoja na Misri, Palestina, Trans-jordan na Hijaz. Sehemu zote hizi aliweka vituo vya harakati alivyokuwa akivitembelea. Alimuweka mpwa wake, Lut(a.s),katika kituo cha T rans-jordan.Aliporuzukiwa watoto wema aliowaomba,Ismail(a.s) na Is-haq(a.s) aliwaingiza kwenye harakati,na akamfanya Ismail(a.s) mkuu wa kituo Hijaz na Is-haq(a.s) mkuu wa kituo cha Palestina. Allah(s.w) aliwateua viongozi hawa wa vituo vya harakati kuwa Manabii wa sehemu hizo na Mzee Ibrahiim(a.s) akiwa kiongozi wao.
Mji wa Makka katika nchi ya Hijaz alipokuwa akiishi Ismail (a.s), ulifanywa kuwa makao makuu ya harakati za kuhuisha Uislamu. Makka ilianza kutumika rasmi kama kituo kikuu cha harakati pale Mzee Ibrahiim (a.s) walipokamilisha kujenga upya Ka’abah na Allah(s.w) kumuamrisha awatangazie watu kuja kuhiji pale kila mwaka.
“Na Ibrahiim alipoinua kuta za nyumba (hii ya Al-Ka’abah) na Ismail (pia) (wakaomba wakasema:) “Ee Mola wetu! Tutakabalie (amali yetu hii ya kujenga huu msikiti). Hakika wewe ndiye Mwenye kusikia na Mwenye kujua.” (2:127)
Na (kumbuka) tulipomkalisha Ibrahimu mahali penye ile Nyumba (takatifu na tukamwambia): “Usinishirikishe na chochote na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya waizungukao na wanaokaa hapo (kufanya ibada yao) na wanaorukuu na kusujudu, (wanaosali).” Na (tukamwambia) “Utangaze kwa watu habari za Hija, watakujia, (wengine) kwa miguu na (wengine) juu ya kila mnyama aliyekonda (kwa machofu ya njiani) wakija kutoka katika kila njia ya mbali. (22:26-27)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.
Soma Zaidi...Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.
Soma Zaidi...KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.
Soma Zaidi...Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Soma Zaidi...Kutokana na Historia ya Nabii Musa na Harun(a.
Soma Zaidi...LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).
Soma Zaidi...(i) Tuanze kulingania kwa kuonesha upweke wa Allah(s.
Soma Zaidi...Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji.
Soma Zaidi...