picha

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Khalid Ibn al walid kwa mara ya kwanza akiwa Muislamu alishiriki vita vya Muuta. Hivi ni vita vilivyopiganwa kati ya waislamu na watu wa Peshia wakichanganyika na Sasanid mwaka 629 mwezi wa 9 katika kijiji kilichoitwa Mu'ta

 

 

 

Sababu ya vita vya muuta ni kulipiza kisasi cha muislamu aliyeuliwa wakati akitekeleza majukumu aliyopewa na Mtume Muhammad. Mtume Muhammad (s.a.w) alimtuma Al-Harith bin Umair Al-Azdi (R.A.) kwenda Basra kupeleka barua ya kuwalingania katika dini ya Uislamu. Lakini akiwa njiani alikamatwa na Shurahbil bin Amrul-Ghassani ambaye ni gavana wa Balqa. Katika wakati huo kumuuwa mjumbe ni katika makosa makubwa na ni sawa na kutangaza vita.

 

 

 

Jeshi la waislamu lilikuwa na askari 3000 huku jeshi la makafiriblikawa na idadi kubwa sana ya askari. Baadhi ya wanahistoria wa kiislamu wametaja kuwa makafiri walikuwa na jeshibkatibya askati 100000 hadi 200000. Hata hivyo wanahistiria wa leo wanataja kuwa wanajeshi wa kikristo walikuwa 10000 ama chini ya hapo. 

 

 

 

Makamanda wa kikosi cha waislamu walikuwa ni Zayd ibn Haritha, Ja'far ibn Abi Talib, na Abd Allah ibn Rawahah na wote walikufa vitani. Makamanda hawq walichaguliwa na Mtume mwenyewe. Pia aliwapangilia kwa myiririko kuwa atanza Zayd akifa atachukuwa uongozi Ja'far na akifa atachukuwa Ibn Rawah. 

 

 

 

Makamanda walipigana kiume hadi wote wakauwawa kwa mpangilio huo huo. Baada ya kuuliwa makamanda wote jeshi la waislamu lilipata mtafaruku na hapo Thabit ibn Aqram akachukuwq bendera kuwa kama kiongozi. 

 

 

 

Baada ya hapo akampatia uongizi khalid Ibn al walid. Sasa Khalid kwa mara ya kwanza anapewa kazi ya kuongoza jeshi la waislamu. Baada ya kuoigana kiume khalid akagunduwa kuwa waislamu wamezidiwa na hivyo watafute njia ya murudi nyumbani salama. 

 

Khalid alilipanga vyema jeshi lake katika muonekano kuwa wataonekana kama nj wageni. Yaani kumfanya adui ahisi kama jeshi la waislamu limeongezeka. Hivyo akawapanga katika swafu tifauti na walivyokuwa siku chache zilizopita. Mfano waliokuwa wanapigana uoande wa kulia wapelekwe nyuma kushito na wanyuma kushito wapelekwe mbele kulia. 

 

Basi makafiri wqlivyoona vile wakapata mshangao na kuhisi kuwa wenzetu wamepata nguvu mpya. Khalid alipoona makafiri wamepata woga ndipo akaamrisha jeshi lishambukie kwa nguvu zote na japo makafiri wakapata mvurugiko kwenye safu zao na wengi waliuliwa hapo. 

 

Khalid akatumia mvurugiko huo na kuanza kurudi nyuma kidogo kidogo. Huku makafiri wqkiogopa kuwafatilia wakidhani wanaweza kuzungukwa. Hatimaye khalid aliweza kulirudisha jeshi la Waislamu salama. 

 

 

 

Waislamu 12 tu waliweza walikufa mashahidi. Makafiri waliokufa kwenye vita idadi yao haijulikani, ijapokuwa inasemekana ni kubwa sana. Hata hivyo baadhi ya nukuu zinasema idadi yao ni kubwa kuliko idadi ya waliokufa katika waislamu. Wanahistoria wa leo wanakataa kuhusu idadi ya walokufa katiika jeshi la waislamu kuwa ni ndogo ukilinganisha na wingi wa jeshi la adui pamoja na njia iliyotumika kupigana. Hata hivyo bado hakuna ushahidi wa kuthibitisha idadi wanayoikubali.

 

Kwa maelezo zaidi ya vita hivi tafadhali rejea makala yetu ya vita vya Muta

https://www.bongoclass.com/madrasa/historia-ya-vita-vya-muta

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-09-05 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2413

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Nuhu(a.s)

(i) Tuanze kulingania kwa Tawhiid – kumjua Allah(s.

Soma Zaidi...
tarekh 10

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...
KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI

KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka.

Soma Zaidi...
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.

Soma Zaidi...
Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma

Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.

Soma Zaidi...
Madhumuni ya dola ya uislamu

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...