image

Khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Yiomyokea khalid Ibn al walid katika vita vya Muta

Khalid Ibn al walid kwa mara ya kwanza akiwa Muislamu alishiriki vita vya Muuta. Hivi ni vita vilivyopiganwa kati ya waislamu na watu wa Peshia wakichanganyika na Sasanid mwaka 629 mwezi wa 9 katika kijiji kilichoitwa Mu'ta

 

 

 

Sababu ya vita vya muuta ni kulipiza kisasi cha muislamu aliyeuliwa wakati akitekeleza majukumu aliyopewa na Mtume Muhammad. Mtume Muhammad (s.a.w) alimtuma Al-Harith bin Umair Al-Azdi (R.A.) kwenda Basra kupeleka barua ya kuwalingania katika dini ya Uislamu. Lakini akiwa njiani alikamatwa na Shurahbil bin Amrul-Ghassani ambaye ni gavana wa Balqa. Katika wakati huo kumuuwa mjumbe ni katika makosa makubwa na ni sawa na kutangaza vita.

 

 

 

Jeshi la waislamu lilikuwa na askari 3000 huku jeshi la makafiriblikawa na idadi kubwa sana ya askari. Baadhi ya wanahistoria wa kiislamu wametaja kuwa makafiri walikuwa na jeshibkatibya askati 100000 hadi 200000. Hata hivyo wanahistiria wa leo wanataja kuwa wanajeshi wa kikristo walikuwa 10000 ama chini ya hapo. 

 

 

 

Makamanda wa kikosi cha waislamu walikuwa ni Zayd ibn Haritha, Ja'far ibn Abi Talib, na Abd Allah ibn Rawahah na wote walikufa vitani. Makamanda hawq walichaguliwa na Mtume mwenyewe. Pia aliwapangilia kwa myiririko kuwa atanza Zayd akifa atachukuwa uongozi Ja'far na akifa atachukuwa Ibn Rawah. 

 

 

 

Makamanda walipigana kiume hadi wote wakauwawa kwa mpangilio huo huo. Baada ya kuuliwa makamanda wote jeshi la waislamu lilipata mtafaruku na hapo Thabit ibn Aqram akachukuwq bendera kuwa kama kiongozi. 

 

 

 

Baada ya hapo akampatia uongizi khalid Ibn al walid. Sasa Khalid kwa mara ya kwanza anapewa kazi ya kuongoza jeshi la waislamu. Baada ya kuoigana kiume khalid akagunduwa kuwa waislamu wamezidiwa na hivyo watafute njia ya murudi nyumbani salama. 

 

Khalid alilipanga vyema jeshi lake katika muonekano kuwa wataonekana kama nj wageni. Yaani kumfanya adui ahisi kama jeshi la waislamu limeongezeka. Hivyo akawapanga katika swafu tifauti na walivyokuwa siku chache zilizopita. Mfano waliokuwa wanapigana uoande wa kulia wapelekwe nyuma kushito na wanyuma kushito wapelekwe mbele kulia. 

 

Basi makafiri wqlivyoona vile wakapata mshangao na kuhisi kuwa wenzetu wamepata nguvu mpya. Khalid alipoona makafiri wamepata woga ndipo akaamrisha jeshi lishambukie kwa nguvu zote na japo makafiri wakapata mvurugiko kwenye safu zao na wengi waliuliwa hapo. 

 

Khalid akatumia mvurugiko huo na kuanza kurudi nyuma kidogo kidogo. Huku makafiri wqkiogopa kuwafatilia wakidhani wanaweza kuzungukwa. Hatimaye khalid aliweza kulirudisha jeshi la Waislamu salama. 

 

 

 

Waislamu 12 tu waliweza walikufa mashahidi. Makafiri waliokufa kwenye vita idadi yao haijulikani, ijapokuwa inasemekana ni kubwa sana. Hata hivyo baadhi ya nukuu zinasema idadi yao ni kubwa kuliko idadi ya waliokufa katika waislamu. Wanahistoria wa leo wanakataa kuhusu idadi ya walokufa katiika jeshi la waislamu kuwa ni ndogo ukilinganisha na wingi wa jeshi la adui pamoja na njia iliyotumika kupigana. Hata hivyo bado hakuna ushahidi wa kuthibitisha idadi wanayoikubali.

 

Kwa maelezo zaidi ya vita hivi tafadhali rejea makala yetu ya vita vya Muta

https://www.bongoclass.com/madrasa/historia-ya-vita-vya-muta





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1412


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋 Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

Waliomuamini Nabii Nuhu(a.s)
Waliomuamini Nuhu(a. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri? Soma Zaidi...

Kuanzishwa kwa Tawala za kifalme baada ya uongozi wa Makhalifa.
Kuanzishwa Ufalme. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)
Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

Miujiza Kama Ushahidi wa Utume wa Nabii Musa(a.s)
Allah(s. Soma Zaidi...

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume
Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili. Soma Zaidi...

HISTORIA NA VISA VYA MITUME, MANABII NA WATU WEMA WALIOTAJWA KWENYE QURAN
Soma Zaidi...