(Wakumbeshe watu khabari hii) wakati Mola wako alipowaambia
Malaika: “Mimi niteleta Khalifa kukaa katika ardhi” (2:30).
Hivyo bustani aliyowekwa ilikuwa ni mapito tu. Awamu ya kwanza ya maisha ya mwanaadamu ilikuwa ni peponi, awamu ya pili ni maisha ya hapa ardhini awamu ya tatu maisha ya Barzakh (kaburini) na awamu ya nne baada ya hukumu (Siku ya Kiyama),
maisha ya milele, peponi au motoni. Mwanzo wa mwanaadamu kuishi katika ardhi unabainishwa na aya zifuatazo;
Akasema (Mwenyezi Mungu): “Shukeni (katika ardhi), nyinyi kwa nyinyi ni maadui. Na makao yenu yatakuwa katika ardhi, na starehe yenu (pia) mpaka muda (niutakao mimi mwenyewe)”.Akasema (Mwenyezi Mungu): “Mtaishi humo na mtafia humo, na mtatolewa humo (mtafufuliwa kwenda Akhera kulipwa)” (7:24-25).
Mwongozo wa Allah kwa Wanaadamu.
Allah(s.w) hakumuacha Khalifa wake aanze maisha gizani. Bali alimpa mwongozo wa namna ya kuutekeleza Ukhalifa wake. Tunasoma katika Qur’an:
Tukasema: “Shukeni humo nyote, na kama ukikufikieni mwongozo utokao kwangu basi watakaofuata uongozi wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika, lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa motoni, humo watakaa milele” (2:38-39).
Utaratibu wa Allah unaobainishwa na aya hizi wa kuleta mwongozo unafanya kazi toka binaadamu wa mwanzo, Adam, hadi wa mwisho wa maisha haya ya duniani. Ni ahadi aliyoichukua Allah(s.w) kuwaletea waja wake mwongozo. Mwongozo ambao unakusudiwa watu waufuate wasibuni mifumo ya maisha kinyume na ule aliouleta Allah(s.w). Na zipo njia mbili tu za kuujua mwongozo wa Allah(s.w).
Ama mtu kuletewa Wahyi (Mitume) au kusoma kutoka kwa walioletewa Wahyi. Ndio maana tunaona Allah(s.w) ameleta Mitume pamoja na vitabu kuubanisha mwongozo huo.
Mwongozo huo umeletwa hatua kwa hatua, hadi kufikia kwa Mtume wa mwisho. Ni mwongozo unaokigusa kila kipengele cha maisha kwa mtu binafsi, taifa, na kimataifa katika ngazi zote, hali zote, mahali popote na wakati wowote. Hapana anachokihitajia mwanaadamu ila kimebainishwa katika mwongozo wa Allah(s.w)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 921
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
kitabu cha Simulizi
👉3
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Madrasa kiganjani
MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AANALELEWA NA BABU YAKE MZEE ABDUL-ALMUTALIB AKIWA NA UMRI WA MIAKA SITA (6)
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...
Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9. Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s. Soma Zaidi...
Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...
HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...
Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Historia ya Dhana ya Kudhibiti Uzazi
Soma Zaidi...
Mapambano Dhidi ya Maadui wa Dola ya Kiislamu
1. Soma Zaidi...