image

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini


(Wakumbeshe watu khabari hii) wakati Mola wako alipowaambia

Malaika: “Mimi niteleta Khalifa kukaa katika ardhi” (2:30).

Hivyo bustani aliyowekwa ilikuwa ni mapito tu. Awamu ya kwanza ya maisha ya mwanaadamu ilikuwa ni peponi, awamu ya pili ni maisha ya hapa ardhini awamu ya tatu maisha ya Barzakh (kaburini) na awamu ya nne baada ya hukumu (Siku ya Kiyama),

maisha ya milele, peponi au motoni. Mwanzo wa mwanaadamu kuishi katika ardhi unabainishwa na aya zifuatazo;


Akasema (Mwenyezi Mungu): “Shukeni (katika ardhi), nyinyi kwa nyinyi ni maadui. Na makao yenu yatakuwa katika ardhi, na starehe yenu (pia) mpaka muda (niutakao mimi mwenyewe)”.Akasema (Mwenyezi Mungu): “Mtaishi humo na mtafia humo, na mtatolewa humo (mtafufuliwa kwenda Akhera kulipwa)” (7:24-25).


Mwongozo wa Allah kwa Wanaadamu.
Allah(s.w) hakumuacha Khalifa wake aanze maisha gizani. Bali alimpa mwongozo wa namna ya kuutekeleza Ukhalifa wake. Tunasoma katika Qur’an:


Tukasema: “Shukeni humo nyote, na kama ukikufikieni mwongozo utokao kwangu basi watakaofuata uongozi wangu huo haitakuwa khofu juu yao wala hawatahuzunika, lakini wenye kukufuru na kuyakadhibisha maneno yetu, hao ndio watakaokuwa watu wa motoni, humo watakaa milele” (2:38-39).

Utaratibu wa Allah unaobainishwa na aya hizi wa kuleta mwongozo unafanya kazi toka binaadamu wa mwanzo, Adam, hadi wa mwisho wa maisha haya ya duniani. Ni ahadi aliyoichukua Allah(s.w) kuwaletea waja wake mwongozo. Mwongozo ambao unakusudiwa watu waufuate wasibuni mifumo ya maisha kinyume na ule aliouleta Allah(s.w). Na zipo njia mbili tu za kuujua mwongozo wa Allah(s.w).

Ama mtu kuletewa Wahyi (Mitume) au kusoma kutoka kwa walioletewa Wahyi. Ndio maana tunaona Allah(s.w) ameleta Mitume pamoja na vitabu kuubanisha mwongozo huo.

Mwongozo huo umeletwa hatua kwa hatua, hadi kufikia kwa Mtume wa mwisho. Ni mwongozo unaokigusa kila kipengele cha maisha kwa mtu binafsi, taifa, na kimataifa katika ngazi zote, hali zote, mahali popote na wakati wowote. Hapana anachokihitajia mwanaadamu ila kimebainishwa katika mwongozo wa Allah(s.w)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 552


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima
Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s. Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Afanywa Kiongozi wa Harakati za Uislamu Ulimwenguni
“Na (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza. Soma Zaidi...

Imam Abu Hanifa: Nuuman Ibn Thabit
Soma Zaidi...

Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil
Mtume Isa(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...

Waliomuamini Nabii Nuhu(a.s)
Waliomuamini Nuhu(a. Soma Zaidi...

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE
Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a. Soma Zaidi...

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)
Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s. Soma Zaidi...

tarekh
Soma Zaidi...