image

Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik bin Anas



Kwa mujibu wa “Kitab al-Ansab na Dhahabi, Tadhkirah al- Huffaz” juzuu ya kwanza, Imam Malik alizaliwa mwaka 93 A.H. Baadhi ya vitabu vimetaja pia mwaka 94 na 95 A.H. Wazazi wa Imam Malik walitoka katika familia ya kifalme ya Kiarabu toka Yemen ambayo ilihamia Madinah. Wakati anazaliwa Imam Malik dola ya Kiislamu ilikuwa chini ya uongozi wa Khalifa Walid bin Abd- al-Malik na japo makao makuu ya dola yalikuwa yamehamishiwa Damascus, Syria, lakini mji wa Madinah ulibakia mashuhuri na kitovu cha elimu ya Uislamu. Familia ya Imam Malik ilizungukwa na ndugu na jamaa wa karibu waliokuwa na elimu ya kutosha.


Hivyo alianza kupata elimu yake katika mazingira ya nyumbani. Zaidi ya hapo alisoma kwa waalimu wengine saba mashuhuri wa fani mbalimbali, miongoni mwao alikuwa Jafar al-Sadiq, kitukuu cha Imam Hussein. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi, umaarufu wa Imam Malik ulizidi kuvuma kutokana na unyenyekevu na ucha Mungu wake. Watu walitoka masafa ya mbali kuja Madina kuhudhuria darsa za Imam Malik.


Sehemu kubwa ya muda wake aliitoa kwa kufundisha na akiifurahia kazi hii. Japo Imam Malik alikuwa mtaalam mzuri wa Hadith, lakini alikuwa dhaifu kidogo katika mambo ya sheria na kutoa fa-twa za kifiqh. Hata hivyo alikuwa mtu madhubuti na mwenye msimamo. Hakukubali kutolewa katika haki kwa hali yoyote iwayo. Wakati fulani alitoa fa’twa ambayo ilikuwa kinyume na matakwa ya Gavana wa Madinah. Gavana alimuonya asitoe fa’twa hiyo hadharani, lakini kwa kuridhika kuwa ndio haki, Imam Malik alitoa maoni yake hadharani na akachapwa viboko hadharani kwa tendo hilo. Katika kazi muhimu alizoziacha Imam Malik ni kitabu chake al-Muwatta chenye mjumuiko wa Hadith na mafundisho ya Mtume(s.a.w) ya ibada na mas’ala mbalimbali ya Kiislamu. Imam Malik alitawafu mwaka 179A.H.Madinah.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 755


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah
Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a. Soma Zaidi...

Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME SULAIMAN(A.S)
Sulaiman(a. Soma Zaidi...

Mji wa Makkah na kabila la kiqureish
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume(s.a.w) maandalizi ya kimafunzo na maandalizi ya ki ilham
Mitume huzaliwa Mitume. Soma Zaidi...

Musa(a.s) Ahamia Madiani
Mchana wa siku moja Musa(a. Soma Zaidi...

Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA NABII ISMAIL(A.S)
Ismail(a. Soma Zaidi...

Kukomeshwa kwa Riddah na Chokochoko Nyingine katika dola ya kiislamu
Soma Zaidi...

Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Historia ya uislamu wakati wa Makhalifa wanne: Abubakar, Umar, Uthman na Ally
Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...