Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik Ibn Anas

Imam Malik bin Anas



Kwa mujibu wa 'Kitab al-Ansab na Dhahabi, Tadhkirah al- Huffaz' juzuu ya kwanza, Imam Malik alizaliwa mwaka 93 A.H. Baadhi ya vitabu vimetaja pia mwaka 94 na 95 A.H. Wazazi wa Imam Malik walitoka katika familia ya kifalme ya Kiarabu toka Yemen ambayo ilihamia Madinah. Wakati anazaliwa Imam Malik dola ya Kiislamu ilikuwa chini ya uongozi wa Khalifa Walid bin Abd- al-Malik na japo makao makuu ya dola yalikuwa yamehamishiwa Damascus, Syria, lakini mji wa Madinah ulibakia mashuhuri na kitovu cha elimu ya Uislamu. Familia ya Imam Malik ilizungukwa na ndugu na jamaa wa karibu waliokuwa na elimu ya kutosha.


Hivyo alianza kupata elimu yake katika mazingira ya nyumbani. Zaidi ya hapo alisoma kwa waalimu wengine saba mashuhuri wa fani mbalimbali, miongoni mwao alikuwa Jafar al-Sadiq, kitukuu cha Imam Hussein. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi, umaarufu wa Imam Malik ulizidi kuvuma kutokana na unyenyekevu na ucha Mungu wake. Watu walitoka masafa ya mbali kuja Madina kuhudhuria darsa za Imam Malik.


Sehemu kubwa ya muda wake aliitoa kwa kufundisha na akiifurahia kazi hii. Japo Imam Malik alikuwa mtaalam mzuri wa Hadith, lakini alikuwa dhaifu kidogo katika mambo ya sheria na kutoa fa-twa za kifiqh. Hata hivyo alikuwa mtu madhubuti na mwenye msimamo. Hakukubali kutolewa katika haki kwa hali yoyote iwayo. Wakati fulani alitoa fa'twa ambayo ilikuwa kinyume na matakwa ya Gavana wa Madinah. Gavana alimuonya asitoe fa'twa hiyo hadharani, lakini kwa kuridhika kuwa ndio haki, Imam Malik alitoa maoni yake hadharani na akachapwa viboko hadharani kwa tendo hilo. Katika kazi muhimu alizoziacha Imam Malik ni kitabu chake al-Muwatta chenye mjumuiko wa Hadith na mafundisho ya Mtume(s.a.w) ya ibada na mas'ala mbalimbali ya Kiislamu. Imam Malik alitawafu mwaka 179A.H.Madinah.




                   


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 287

Post zifazofanana:-

VYAKULA VYA WANGA NA MADINI
Kuna aina nyingi za vyakula kama mafuta, wanga, fati, protini na vitamini. Je! unajuwa faida zake na hasara zake? Soma Zaidi...

Jinsi Mtume Muhammad (s.a.w) alivyoipokea Qur-an:
(iii)Jinsi Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Mayai
Soma Zaidi...

tarekh
Soma Zaidi...

Fahamau protini na kazi zake, vyakula vya protini, na athari za upungufu wake.
unayopaswa kuyajuwa kuhusu protini na vyakula vya protini, faida zake na hasara zake. Madhara ya kiafya yanayohusiana na protini pamoja na kuyaepuka madhara hayo Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Nyanya
Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Spinachi
Soma Zaidi...

Sheria Katika Uislamu
4. Soma Zaidi...

ASUBUHI YA VARANGATI NA KAMARALZAMAN
VARANGATI ASUBUHI; Baada ya kugunduwa kuwa haikuwa ndoto kamaralzamani aliamini kuwa yule ndio mke ambaye baba yake alimchagulia. Soma Zaidi...

maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimba
Je kupata maumivu sehemu zinazoota mavuzi na kuwa namaumiv wakat wa haja ndogo na pia kwenye kichwa cha uume kunakua kama kunavimb hizo syo dalili moja wapi? Soma Zaidi...

Namna ya kuswali
2. Soma Zaidi...

dondoo za afya
Basi tambua haya;- 1. Soma Zaidi...