Imam Abu Hanifa: Nuuman Ibn Thabit

Imam Abu Hanifa: Nuuman Ibn Thabit

Imam Abu Hanifah


Imam Abu Hanifah ndiye anayenasibishwa na madh'hab ya Hanafi. Jina lake kamili ni Nu'man bin Thabit Abu Hanifah. Imam Abu Hanifah alizaliwa Kufa, Iraq katika mwaka wa 80 baada ya Hijrah. Yeye ni katika watu wa kipindi cha Tabiin kwani aliwashuhudia maswahaba wa Mtume ikiwa ni pamoja na Khalifa bin Abu Taalib, Anas bin Malik na Sahl bin Sa'd. Alipata elimu katika miji ya Kufa na Basra kisha Makka na Madinah. Miongoni mwa waalimu wake alikuwa Abdallah bin Umar mtoto wa Khalifa Umar bin Khattaab. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi na umaarufu kutokana na elimu na ucha Mungu wake; Imam Abu Hanifah alibakia kuwa mnyenyekevu na mwenye msimamo usiotetereka.


Mwaka 146 A.H Khalifah Mansur alimteua Abu Hanifah awe Kadhi; lakini alikataa akitoa hoja kuwa nafasi hiyo ni nzito kuliko uwezo wake. Mansur alikasirika na kumwambia Imam Abu Hanifah kuwa ni mwongo. Imam Abu Hanifah alimjibu, 'kama mimi ni mwongo basi kauli yangu kuwa sifai ni sahihi kwani mwongo hawezi kuchaguliwa kuwa Kadhi'. Mansur alikasirika zaidi na kumtupa gerezani Imam Abu Hanifah.


Hata hivyo, kutokana na vilio vya watu ilibidi Mansur aruhusu Imam Abu Hanifah aendeshe darsa hapo hapo jela. Lakini alivyoona watu wanazidi kufurika jela kuhudhuria darsa, alimpa sumu Abu Hanifah akafa katika mwezi wa Rajab 150 A.H., miaka kumi na nane (18) tangu Abbasids kushika mamlaka.


Jeneza lake liliswaliwa mara sita na kila mara watu zaidi ya hamsini elfu walisimama kumswalia. Na hata baada ya kuzikwa watu toka sehemu mbalimbali duniani walifurika kuja kuswali swala ya jeneza.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 367


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar
Soma Zaidi...

DUA 94 - 114
DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Isa(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu
Soma Zaidi...

Siku ya Taqwiya na kusimama Arafa
5. Soma Zaidi...

Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza
4. Soma Zaidi...

Haki na Wajibu wa mume kwa mkewe na familia
Soma Zaidi...

Hukumu na taratibu za mirathi na kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...

namna ya kuswali swala ya msafiri, nguzo zake na hukumu zake
Soma Zaidi...

DUA 61 - 84
61. Soma Zaidi...

Twahara
FIQH 1. Soma Zaidi...

Ujuwe utaratibu mzima wa funga na kutekeleza ibada ya Swaumu
Soma Zaidi...