Imam Abu Hanifah
Imam Abu Hanifah ndiye anayenasibishwa na madh’hab ya Hanafi. Jina lake kamili ni Nu’man bin Thabit Abu Hanifah. Imam Abu Hanifah alizaliwa Kufa, Iraq katika mwaka wa 80 baada ya Hijrah. Yeye ni katika watu wa kipindi cha Tabiin kwani aliwashuhudia maswahaba wa Mtume ikiwa ni pamoja na Khalifa bin Abu Taalib, Anas bin Malik na Sahl bin Sa’d. Alipata elimu katika miji ya Kufa na Basra kisha Makka na Madinah. Miongoni mwa waalimu wake alikuwa Abdallah bin Umar mtoto wa Khalifa Umar bin Khattaab. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi na umaarufu kutokana na elimu na ucha Mungu wake; Imam Abu Hanifah alibakia kuwa mnyenyekevu na mwenye msimamo usiotetereka.
Mwaka 146 A.H Khalifah Mansur alimteua Abu Hanifah awe Kadhi; lakini alikataa akitoa hoja kuwa nafasi hiyo ni nzito kuliko uwezo wake. Mansur alikasirika na kumwambia Imam Abu Hanifah kuwa ni mwongo. Imam Abu Hanifah alimjibu, “kama mimi ni mwongo basi kauli yangu kuwa sifai ni sahihi kwani mwongo hawezi kuchaguliwa kuwa Kadhi”. Mansur alikasirika zaidi na kumtupa gerezani Imam Abu Hanifah.
Hata hivyo, kutokana na vilio vya watu ilibidi Mansur aruhusu Imam Abu Hanifah aendeshe darsa hapo hapo jela. Lakini alivyoona watu wanazidi kufurika jela kuhudhuria darsa, alimpa sumu Abu Hanifah akafa katika mwezi wa Rajab 150 A.H., miaka kumi na nane (18) tangu Abbasids kushika mamlaka.
Jeneza lake liliswaliwa mara sita na kila mara watu zaidi ya hamsini elfu walisimama kumswalia. Na hata baada ya kuzikwa watu toka sehemu mbalimbali duniani walifurika kuja kuswali swala ya jeneza.
Umeionaje Makala hii.. ?
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋
Soma Zaidi...Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.
Soma Zaidi...Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.
Soma Zaidi...Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.
Soma Zaidi...KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.
Soma Zaidi...KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...