Imam Abu Hanifah
Imam Abu Hanifah ndiye anayenasibishwa na madh’hab ya Hanafi. Jina lake kamili ni Nu’man bin Thabit Abu Hanifah. Imam Abu Hanifah alizaliwa Kufa, Iraq katika mwaka wa 80 baada ya Hijrah. Yeye ni katika watu wa kipindi cha Tabiin kwani aliwashuhudia maswahaba wa Mtume ikiwa ni pamoja na Khalifa bin Abu Taalib, Anas bin Malik na Sahl bin Sa’d. Alipata elimu katika miji ya Kufa na Basra kisha Makka na Madinah. Miongoni mwa waalimu wake alikuwa Abdallah bin Umar mtoto wa Khalifa Umar bin Khattaab. Pamoja na kujikusanyia elimu nyingi na umaarufu kutokana na elimu na ucha Mungu wake; Imam Abu Hanifah alibakia kuwa mnyenyekevu na mwenye msimamo usiotetereka.
Mwaka 146 A.H Khalifah Mansur alimteua Abu Hanifah awe Kadhi; lakini alikataa akitoa hoja kuwa nafasi hiyo ni nzito kuliko uwezo wake. Mansur alikasirika na kumwambia Imam Abu Hanifah kuwa ni mwongo. Imam Abu Hanifah alimjibu, “kama mimi ni mwongo basi kauli yangu kuwa sifai ni sahihi kwani mwongo hawezi kuchaguliwa kuwa Kadhi”. Mansur alikasirika zaidi na kumtupa gerezani Imam Abu Hanifah.
Hata hivyo, kutokana na vilio vya watu ilibidi Mansur aruhusu Imam Abu Hanifah aendeshe darsa hapo hapo jela. Lakini alivyoona watu wanazidi kufurika jela kuhudhuria darsa, alimpa sumu Abu Hanifah akafa katika mwezi wa Rajab 150 A.H., miaka kumi na nane (18) tangu Abbasids kushika mamlaka.
Jeneza lake liliswaliwa mara sita na kila mara watu zaidi ya hamsini elfu walisimama kumswalia. Na hata baada ya kuzikwa watu toka sehemu mbalimbali duniani walifurika kuja kuswali swala ya jeneza.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1665
Sponsored links
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
Kitabu cha Afya
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Imam Bukhari na Sahihul Bukhari
Soma Zaidi...
tarekh 06
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...
tarekh 02
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...
Vita vya Badr: Chanzo na sababu za vita vya Badr, Mafunzo ya Vita Vya Badr
Vita vya Badri. Soma Zaidi...
Bani Israil Kuabudu Ndama
Wakati Nabii Musa(a. Soma Zaidi...
Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani
Yusufu(a. Soma Zaidi...
Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.
Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto. Soma Zaidi...
Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake
Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s. Soma Zaidi...
Kifo cha Nabii Sulaiman
Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine. Soma Zaidi...