Imam Abu Daud na Sunan Abi Daud
Sunnan Abu Daud
Sunnan Abu Daud ni kitabu cha Hadith cha Abu Daud. Imamu Abu Daud alizaliwa 203 A.H. na akafiriki 275 A.H. Elimu yake ya mwanzo aliipata Khurasan. Alisafiri sehemu mbali mbali ambazo zilikuwa mashuhuri kwa kuwa na wanazuoni wa Hadith. Ni miongoni mwa wanafunzi wa Imam Ahmad bin Hambali. Alikusanya Hadith 500,000 na alizoziandika katika kitabu chake cha Hadith kinachojulikana kwa jina la "Sunnan" ni Hadith 48,000 tu.
Japo hakuwa mkali sana katika uchambuzi na uhakiki wa Hadith zake kama walivyokuwa Bukhari na Muslim, Sunan yake imekuwa ni kitabu cha Hadith mashuhuri sana kwa Umma wa Kiislamu na imeshika daraja la 2 kwa usahihi baada ya sahihi mbili. Hapana shaka kitabu hiki kimejaza mapengo ya mambo yale ambayo hayakugusiwa na Imam Bukhari na Imamu Muslim. Pia Abu Dawud naye alipanga Hadith zake kulingana na vichwa vya habari vya mada mbali mbali.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)
“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.
Soma Zaidi...Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...