Imam Muhammad Idris al-Shafii
Imam Muhammad Idris al-Shafii
Imam Shafii alizaliwa mwaka (150 A.D.) huko Gaza katika ukanda wa Pwani ya bahari ya Meditteranean. Yeye ni wa kabila la Quraysh. Akiwa bado kijana, Imam Shafii alihifadhi Qurβan na Kitabu cha Imam Malik, al-Muwata. Alisoma elimu ya sheria ya Kiislamu toka kwa mwanachuoni mashuhuri na Mufti wa Makka Muslim bin Khalid al-Zanji. Baada ya kifo cha Khalid, alikwenda Madinah ambapo alisoma kwa Imam Malik bin Anas. Wakati Imam Malik anafariki tayari Imam Shafii alikuwa ashavuma ndani ya Arabuni na kwingineko kwa ujuzi wake wa elimu ya sheria na Uislamu kwa ujumla.
Kutokana na elimu na uadilifu wake, Imam Shafii aliteuliwa kufanya kazi Serikalini. Hata hivyo hakudumu kwani kwa uadilifu na utendaji wake wa kazi kwa haki aligongana na wakuu wa Serikali wasiotaka haki. Alikamatwa na kuhamishiwa Iraq akiwa amefungwa minyororo kwa tuhuma kuwa anafanya uchochezi dhidi ya Serikali. Huo ulikuwa mwaka 187 A.H. (803 A.D.) wakati wa utawala wa Harun al-Rashid. Baadae aliachiwa huru kwa kuonekana hana hatia. Alibaki kwa muda Baghdad akisoma chini ya wanafunzi wa Imam Abu Hanifah. Alifanya kazi ya kudarasisha Makka na akapata wasikilizaji wengi akiwemo Imam Ahmad bin Hambal ambaye wakati huo alikuwa anasoma Makka. Pamoja na kuwa alikuwa na maoni ya kifiqh tofauti na yale ya Imam Malik na Abu Hanafi, aliwaheshimu na kuthamini juhudi na michango yao. Hakujenga kundi la Shafii dhidi ya Maimamu wengine kama ambavyo baadhi ya Masheikh hufanya hivi leo.
Maimamu ambao tunajinasibisha nao hivi leo wao walikuwa wamoja katika Uislamu. Pale walipokuwa na maoni tofauti katika ufahamu wa baadhi ya mambo walikubaliana kutofautiana, wakazikubali tofauti zao, lakini walibaki kuwa wamoja walioshikamana katika kamba (dini) ya Allah(s.w).
Kazi kubwa ya kufundisha na uandishi, Imam Shafii aliifanyia Misri katika mji wa Cairo ya leo. Huko alizungukwa na wanafunzi na wanachuoni toka sehemu mbalimbali. Walijifunza na kuandika kila alichosema. Imam Shafii alikuwa na kawaida ya kuwaamrisha wanafunzi wake kusoma kwa sauti kila walichoandika ili apate kusahihisha. Kazi kubwa muhimu za Imam Shafii ambazo zinaendelea kutoa mchango mkubwa katika elimu ya Fiqh na sheria ya Kiislamu mpaka hivi leo ni Kitab al-Umm na Kitab al- Risalah Fi-Usul-al Fiqh (al-Risalah). Imam Shafii alifariki na kuzikwa Cairo mwezi Rajabu mwaka 204 A.H/20/1/820 A.D.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 ai web app π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Dua za Mitume na Manabii π4 kitabu cha Simulizi π5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Sulaiman(a.s)
Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a.
Soma Zaidi...KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S.
Soma Zaidi...tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee βAbdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.
Soma Zaidi...Kuchimbwa upya kwa kisima cha Zamzam
Sura na historia ya mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 3.Hapa utajifunza kuhusu kufukuliwa kwa kisima cha Zamzam baada ya kufukiwa muda mrefu.
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.
Soma Zaidi...