image

Imam Muhammad Idris al-Shafii

Imam Muhammad Idris al-Shafii

Imam Muhammad Idris al-Shafii



Imam Shafii alizaliwa mwaka (150 A.D.) huko Gaza katika ukanda wa Pwani ya bahari ya Meditteranean. Yeye ni wa kabila la Quraysh. Akiwa bado kijana, Imam Shafii alihifadhi Qurโ€™an na Kitabu cha Imam Malik, al-Muwata. Alisoma elimu ya sheria ya Kiislamu toka kwa mwanachuoni mashuhuri na Mufti wa Makka Muslim bin Khalid al-Zanji. Baada ya kifo cha Khalid, alikwenda Madinah ambapo alisoma kwa Imam Malik bin Anas. Wakati Imam Malik anafariki tayari Imam Shafii alikuwa ashavuma ndani ya Arabuni na kwingineko kwa ujuzi wake wa elimu ya sheria na Uislamu kwa ujumla.


Kutokana na elimu na uadilifu wake, Imam Shafii aliteuliwa kufanya kazi Serikalini. Hata hivyo hakudumu kwani kwa uadilifu na utendaji wake wa kazi kwa haki aligongana na wakuu wa Serikali wasiotaka haki. Alikamatwa na kuhamishiwa Iraq akiwa amefungwa minyororo kwa tuhuma kuwa anafanya uchochezi dhidi ya Serikali. Huo ulikuwa mwaka 187 A.H. (803 A.D.) wakati wa utawala wa Harun al-Rashid. Baadae aliachiwa huru kwa kuonekana hana hatia. Alibaki kwa muda Baghdad akisoma chini ya wanafunzi wa Imam Abu Hanifah. Alifanya kazi ya kudarasisha Makka na akapata wasikilizaji wengi akiwemo Imam Ahmad bin Hambal ambaye wakati huo alikuwa anasoma Makka. Pamoja na kuwa alikuwa na maoni ya kifiqh tofauti na yale ya Imam Malik na Abu Hanafi, aliwaheshimu na kuthamini juhudi na michango yao. Hakujenga kundi la Shafii dhidi ya Maimamu wengine kama ambavyo baadhi ya Masheikh hufanya hivi leo.


Maimamu ambao tunajinasibisha nao hivi leo wao walikuwa wamoja katika Uislamu. Pale walipokuwa na maoni tofauti katika ufahamu wa baadhi ya mambo walikubaliana kutofautiana, wakazikubali tofauti zao, lakini walibaki kuwa wamoja walioshikamana katika kamba (dini) ya Allah(s.w).


Kazi kubwa ya kufundisha na uandishi, Imam Shafii aliifanyia Misri katika mji wa Cairo ya leo. Huko alizungukwa na wanafunzi na wanachuoni toka sehemu mbalimbali. Walijifunza na kuandika kila alichosema. Imam Shafii alikuwa na kawaida ya kuwaamrisha wanafunzi wake kusoma kwa sauti kila walichoandika ili apate kusahihisha. Kazi kubwa muhimu za Imam Shafii ambazo zinaendelea kutoa mchango mkubwa katika elimu ya Fiqh na sheria ya Kiislamu mpaka hivi leo ni Kitab al-Umm na Kitab al- Risalah Fi-Usul-al Fiqh (al-Risalah). Imam Shafii alifariki na kuzikwa Cairo mwezi Rajabu mwaka 204 A.H/20/1/820 A.D.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 894


Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 kitabu cha Simulizi     ๐Ÿ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA KUPASULIWA KWA KIFUA AU TUMBO CHA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AKIWA MTOTO KWA BI HALIMA
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Siku za Hija
Baada ya Mtume(s. Soma Zaidi...

Maana ya Funga ya ramadhani kisheria na Aina za funga
Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga. Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME YUNUS(A.S)
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Maadui wa uislamu na mbinu zao: wanafiki, makafiri, mayahudi, wakristo,
Upinzani dhidi ya Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

Chanzo cha Mapato katika serekali ya Kiislamu wakati wa Makhalifa
Soma Zaidi...

historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YAโ€˜AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...

Zakaria(a.s) Akabidhiwa Ulezi wa Maryam
Baada ya kupigwa kura juu ya nani awe mlezi wa Maryam, Nabii Zakaria akachaguliwa kuwa mlezi wa Maryam. Soma Zaidi...

Mawazo Tofauti Kuhusiana na Uchaguzi wa Abubakar
Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Kuulingania Uislamu kwa Jamii Yake
Nabii Ibrahim(a. Soma Zaidi...

UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...