Imam Muhammad Idris al-Shafii

Imam Muhammad Idris al-Shafii

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Imam Muhammad Idris al-Shafii

Imam Muhammad Idris al-Shafii



Imam Shafii alizaliwa mwaka (150 A.D.) huko Gaza katika ukanda wa Pwani ya bahari ya Meditteranean. Yeye ni wa kabila la Quraysh. Akiwa bado kijana, Imam Shafii alihifadhi Qur’an na Kitabu cha Imam Malik, al-Muwata. Alisoma elimu ya sheria ya Kiislamu toka kwa mwanachuoni mashuhuri na Mufti wa Makka Muslim bin Khalid al-Zanji. Baada ya kifo cha Khalid, alikwenda Madinah ambapo alisoma kwa Imam Malik bin Anas. Wakati Imam Malik anafariki tayari Imam Shafii alikuwa ashavuma ndani ya Arabuni na kwingineko kwa ujuzi wake wa elimu ya sheria na Uislamu kwa ujumla.


Kutokana na elimu na uadilifu wake, Imam Shafii aliteuliwa kufanya kazi Serikalini. Hata hivyo hakudumu kwani kwa uadilifu na utendaji wake wa kazi kwa haki aligongana na wakuu wa Serikali wasiotaka haki. Alikamatwa na kuhamishiwa Iraq akiwa amefungwa minyororo kwa tuhuma kuwa anafanya uchochezi dhidi ya Serikali. Huo ulikuwa mwaka 187 A.H. (803 A.D.) wakati wa utawala wa Harun al-Rashid. Baadae aliachiwa huru kwa kuonekana hana hatia. Alibaki kwa muda Baghdad akisoma chini ya wanafunzi wa Imam Abu Hanifah. Alifanya kazi ya kudarasisha Makka na akapata wasikilizaji wengi akiwemo Imam Ahmad bin Hambal ambaye wakati huo alikuwa anasoma Makka. Pamoja na kuwa alikuwa na maoni ya kifiqh tofauti na yale ya Imam Malik na Abu Hanafi, aliwaheshimu na kuthamini juhudi na michango yao. Hakujenga kundi la Shafii dhidi ya Maimamu wengine kama ambavyo baadhi ya Masheikh hufanya hivi leo.


Maimamu ambao tunajinasibisha nao hivi leo wao walikuwa wamoja katika Uislamu. Pale walipokuwa na maoni tofauti katika ufahamu wa baadhi ya mambo walikubaliana kutofautiana, wakazikubali tofauti zao, lakini walibaki kuwa wamoja walioshikamana katika kamba (dini) ya Allah(s.w).


Kazi kubwa ya kufundisha na uandishi, Imam Shafii aliifanyia Misri katika mji wa Cairo ya leo. Huko alizungukwa na wanafunzi na wanachuoni toka sehemu mbalimbali. Walijifunza na kuandika kila alichosema. Imam Shafii alikuwa na kawaida ya kuwaamrisha wanafunzi wake kusoma kwa sauti kila walichoandika ili apate kusahihisha. Kazi kubwa muhimu za Imam Shafii ambazo zinaendelea kutoa mchango mkubwa katika elimu ya Fiqh na sheria ya Kiislamu mpaka hivi leo ni Kitab al-Umm na Kitab al- Risalah Fi-Usul-al Fiqh (al-Risalah). Imam Shafii alifariki na kuzikwa Cairo mwezi Rajabu mwaka 204 A.H/20/1/820 A.D.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2667

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi
Kwanini mwanadamu hawezi kuunda dini sahihi

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kulelewa kwa Mtume,  maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.
Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.

Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto.

Soma Zaidi...
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake

Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake.

Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina

Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.

Soma Zaidi...
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...