image

Kuanzishwa kwa mahakama na mahakama ya Kadhi wakati wa makhalifa

Kuanzishwa kwa mahakama na mahakama ya Kadhi wakati wa makhalifa

Khalifa na Mahakama



Kabla ya kuangalia suala la mahakama katika Uislamu, tuanze na mtazamo wa Uislamu juu ya uhalifu, makosa au hatia. Makosa katika Uislamu yapo katika mafungu matatu:


(i) Makosa yanayomuhusu Mwenyezi Mungu kama vile uzinzi, ambao adhabu yake ni bakora mia moja, kumsingizia mtu kuzini, ambako adhabu yake viboko themanini, kuritadi adhabu yake ni kifo, kunywa vileo adhabu yake viboko themanini, wizi ambao adhabu yake ni kukatwa mkono na unyang’anyi au ujambazi ambao adhabu yake ni
kukatwa mkono na miguu. Makosa haya yanajumuishwa katika istilahi moja kuwa ni Al-Hudud. Khalifa hawezi kusamehe makosa haya. Kazi yake ni kutekeleza hadd (adhabu). Kwa wasio Waislamu makosa haya husameheka endapo atasilimu.


(ii) Makosa dhidi ya mwanadamu yanayohitaji fidia al-qisas.
Mengi ya makosa haya kama kuuwa, kuumiza, kumtukana mtu n.k yanaweza kumalizwa kwa makubaliano kwa mujibu wa sheria lakini Khalifa hana mamlaka ya kusamehe ila aliyekosewa. Hali kadhalika makosa haya hayahesabiwi kuwa makosa dhidi ya Serikali.


(iii) Yapo baadhi ya makosa kama, uasi (Rebellion), kula mali ya umma yamehesabika kama makosa dhidi ya Serikali.Kwa kuzingatia haya, kazi za Khalifa kimahakama ni za aina tatu. Kwanza kuhakikisha kuna amani katika himaya yake, maendeleo kwa tabaka zote za watu na kuwalinda wanyonge mbele ya wenye kujiweza. Pili ni kutekeleza adhabu, kuratibu na kutekeleza haki za wanaodhulumiwa. Na tatu ni kuteua mahakimu wa kusimamia haki.


Mahakimu hawa walikuwa watu wazima, waadilifu, waliobobea katika sheria ambao kazi zao ni pamoja na kuhukumu kesi, kusuluhisha magomvi, kurudisha amana za watu, ulipaji wa zaka, utekelezaji wa usia, utekelezaji wa adhabu, kusimamia mipango ya ndoa, mirathi, talaka, na haki za wanyonge.


Katika kuhakikisha kuwa haki inatendeka kwa wote, tangu wakati wa Ukhalifa wa Abubakar ilianzishwa ofisi ya mufti au taasisi ya mufti au tume ya uchambuzi wa sheria. Ofisi hii ndio pekee iliyoruhusiwa kutoa uchambuzi wa kina wa Fatwa za mamlaka mbali mbali. Hakuruhusiwa mtu mwingine kutoa uchambuzi wa sheria. Walioteuliwa wakati wa Abu bakar kushika wadhifa huu ni Umar, Ali, Uthman, Abul Rahman bin Auf, Ali bin Kaab, Zaid bin Thabit na Abu Huraira - Mufti hawa walisaidia kuwafahamisha watu kuhusu sheria na kuwashauri bila malipo. Serikali ilifanya hivi ili kupunguza makosa kwani kwa kujua sheria watu walijizuia kufanya makosa.


Waraka, Khalifa Umar,aliowatumia mahakimu ni kielelezo cha utaratibu wa mahakama ulivyokuwa wakati wa makhalifa ambao leo hii unafuatwa duniani kote. waraka huo tunaufupisha kama ifuatavyo:


(i) Utawala wa haki ni amri ya Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake, hivyo ni lazima kufuatwa.


(ii) Mashtaka yanapowasilishwa ipitishwe hukumu kwa uangalifu. (iii) Mshitaki na mshitakiwa wote watendewe haki ili maskini asikate
tamaa ya kufanyiwa haki na wenye uwezo wasifikirie kupendelewa.


(iv) Ushahidi ni juu ya mlalamikaji na anayelalamikiwa anaweza kukana anacholalamikiwa kwa kuapa.


(v) Suluhu inaweza kufikiwa nje ya mahakama lakini mazingira ya suluhu yasichupe mipaka ya maamrisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu.


(vi) Hukumu inaweza kubadilishwa katika jambo lililodhahiri, kwani kubadilishwa hukumu ni bora kuliko kuendelea na uonevu.


(vii) Ikitokea kesi isiyo angukia kwenye sheria wala hukumu iliyoitangulia, ilinganishwe na kesi zinazofanana kisha deduction itumike kupitisha hukumu inayompendeza Mwenyezi Mungu na ya haki.


(viii) Mlalamikaji apewe muda wa kutolea ushahidi kesi yake ataposhindwa kesi inaweza kufutwa.


(ix) Hakimu asijione wala kuonyesha kuchukia inaposemwa kweli.


Watu wote ni sawa mbele ya sheria ndio mafunzo ya Qur’an. Uislamu hauruhusu ule msemo wa “Mfalme hakosei”. Hakuna mwanadamu aliyekamilika asiyekosea kabisa. Mtume (s.a.w.) aliweka mfano pale alipowataka watu wenye madai dhidi yake wajitokeze. Maswahaba wake nao walifuata nyayo zake kama mtu angewashitaki kama ilivyotokea kwa Umar au wao pia wangeshitaki kama ilivyotokea kwa Ali.


Khalifa umar na Ubayy ibn Kaab, walikuwa na tofauti zao. Ubayy ibn Kaab alikwenda kumshtaki Khalifa kwenye mahakama ya Zayd bin Thabit. Hivyo Khalifa aliingia mahakamani kwa kujitetea. Alipokuwa anaingia mahakamani Zayd alisimama. Hapa Khalifa alisema hili ni tendo la kwanza la kuvunja haki. Kwa kufuata nafasi ya Khalifa kuwa alikuwa anajitetea alilazimika kuapa. Hakimu Zayd alimuomba Ubayy aondoe haki yake ya kumtaka Khalifa aape. Khalifa Umar aliingilia kati na kusema “kama Umar na watu wengine siyo sawa mbele yako, hufai kuwa Hakim.33





                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 330


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Vipengele vya Mikataba ya ‘Aqabah na faida zake katika kuimarisha uislamu Maka na Madina
Katika Hija iliyofuatia katika mwaka wa 621 A. Soma Zaidi...

Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima
Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s. Soma Zaidi...

Je, Nabii Isa(a.s) ni Mtoto wa Mungu?
Mwenyezi Mungu si kiumbe. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...

Musa(a.s) Ahamia Madiani
Mchana wa siku moja Musa(a. Soma Zaidi...

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu
Musa(a. Soma Zaidi...

Musa(a.s)Kupewa Utume Rasmi
Musa alipotimiza muda, alifunga safari na ahali zake kurejea Misri. Soma Zaidi...

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao
Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 04
Soma Zaidi...

tarekh 4
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji. Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...

Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri
Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji. Soma Zaidi...