picha

Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)

Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a.

Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)

Vitimbi vya Wapinzani Dhidi ya Ujumbe wa Nabii Shu’ayb(a.s)

Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a.s) na kufuata nasaha zake walikuwa watu wachache tu katika jamii yake. Wengi wao walikaidi mafundisho ya Mtume wao wakiongozwa na wakuu wa jamii. Katika kumkanusha Mtume wao walitumia mbinu mbali mbali.



Kwanza, walitumia vitisho
Wakuu waliotakabari katika kaumu yake wakasema: “Ewe Shu’ayb! Tutakutoa wewe na wale walioamini pamoja nawe katika mji wetu, au mrejee katika mila yetu.” Akasema: “Je, ingawa tunaichukia?” (7:88)



Pili, walitumia mbinu ya kuwakatisha watu tamaa

Na wakuu waliokufuru katika kaumu yake wakasema: “Kama nyinyi mkimfuata Shu’ayb, hapo bila shaka mtakuwa wenye kukhasirika.” (7:90)



Tatu,walimdhihaki Mtume wao.

Wakasema: Ewe Shuaibu! Swala zako zinakuamrisha tuyaache yaliyokuwa wakiyaabudu baba zetu au tuache kufanya tupendavyo katika mali zetu? Bila shaka wewe ni mwenye akili na mnyoofu (11:87)



Nne, walitumia mbinu ya kumdhalilisha.

Wakasema: “Ewe Shu’ayb! Hatufahamu mengi katika hayo unayoyasema. Na sisi tunakuona mdhalilifu kwetu. Lau kuwa si jamaa zako tungekupiga mawe, wala wewe si mtu mtukufu kwetu! (ila tunachunga hishima ya jamaa zako tu).” (11:91)



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2309

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 ai web app     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Historia ya Al-Khidhri

Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an.

Soma Zaidi...
Kisa cha Malkia wa Sabaa.

Sabaa ulikuwa mji katika nchi inayojulikana leo kama Yemen.

Soma Zaidi...
Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Dhulqarnain

Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”.

Soma Zaidi...