Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a.
Kama ilivyokuwa katika kaumu zilizotangulia, waliomuamini Shu’ayb(a.s) na kufuata nasaha zake walikuwa watu wachache tu katika jamii yake. Wengi wao walikaidi mafundisho ya Mtume wao wakiongozwa na wakuu wa jamii. Katika kumkanusha Mtume wao walitumia mbinu mbali mbali.
Kwanza, walitumia vitisho
Wakuu waliotakabari katika kaumu yake wakasema: “Ewe Shu’ayb! Tutakutoa wewe na wale walioamini pamoja nawe katika mji wetu, au mrejee katika mila yetu.” Akasema: “Je, ingawa tunaichukia?” (7:88)
Pili, walitumia mbinu ya kuwakatisha watu tamaa
Na wakuu waliokufuru katika kaumu yake wakasema: “Kama nyinyi mkimfuata Shu’ayb, hapo bila shaka mtakuwa wenye kukhasirika.” (7:90)
Tatu,walimdhihaki Mtume wao.
Wakasema: Ewe Shuaibu! Swala zako zinakuamrisha tuyaache yaliyokuwa wakiyaabudu baba zetu au tuache kufanya tupendavyo katika mali zetu? Bila shaka wewe ni mwenye akili na mnyoofu (11:87)
Nne, walitumia mbinu ya kumdhalilisha.
Wakasema: “Ewe Shu’ayb! Hatufahamu mengi katika hayo unayoyasema. Na sisi tunakuona mdhalilifu kwetu. Lau kuwa si jamaa zako tungekupiga mawe, wala wewe si mtu mtukufu kwetu! (ila tunachunga hishima ya jamaa zako tu).” (11:91)
Umeionaje Makala hii.. ?
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.
Soma Zaidi...Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.
Soma Zaidi...Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto.
Soma Zaidi...Pamoja na Ucha-Mungu aliokuwa nao Nabii Sulaiman watu hawakuacha kumsingizia mambo machafu.
Soma Zaidi...KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani.
Soma Zaidi...