image

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)

Tukirejea Qur’an (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a.s). Pamoja na Nabii Nuhu(a.s) kuahidiwa kuwa watu wake wa nyumbani watakuwa miongoni mwa watakaookolewa na gharka, mtoto wake alikataa kuingia kwenye jahazi(safina) na akawa ni miongoni mwa wenye kuangamia kama tunavyo jifunza katika aya zifuatazo.




Na akasema(Nuhu):”Pandeni humo, kwa jina la Mwenyezi Mungu kuwe kwenda kwake na kusimamma kwake. Hakika Mola wangu ni mwingi wa kusamehe na mwingi wa kurehemu.


Ikawa hiyo (jahazi) inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuhu akamwita mwanawe aliyekuwa mbali amekataa kuingia jahazini: “Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri”. Na akasema (huyo mtoto)” “Nitaukimbilia Mlima utakaonilinda na maji” Akasema(Nuhu): “Hakuna leo wa kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu isipokuwa yule atakayemrehemu (Mwenyezi Mungu).” Mara mawimbi yakaingia baina yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa. (11:41-43)



Baada ya Gharika

Baada ya gharika kuisha, Nabii Nuhu(a.s) Ilibidi amuelekee Mola wake kutaka kujua ni vipi mwanawe amekuwa miongoni mwa walioangamia.




Na Nuhu alimuomba Mola wake (alipomuona mwanawe anaangamia) akasema: Ewe Mola wangu! Mwanangu ni katika watu wa nyumbani kwangu (mbona anaangamia)? Na hakika ahadi Yako ni haki; nawe ni mwenye haki kuliko mahakimu (wote).”Akasema (Mwenyezi Mungu): “Ewe Nuhu! Huyu si miongoni mwa watu wako. Yeye ni (mwenye) mwenendo usiokuwa mzuri. Basi usiniombe ambayo huyajui. Mimi nakunasihi usiwe miongoni mwa wajinga.” (Nuhu) Akasema: Ee Mola wangu! Mimi najikinga kwako nisije kukuombatena nisiyoyajua; na kama hutanisamehe na kunirehemu nitakuwa miongoni mwa watakaopata khasara.”(11:45-47)



Pia tunahamishwa juu ya kuangamia mke wa Nuhu(a.s) katika aya ifuatayo:




Mwenyezi Mungu amepiga (anapiga)mfano wa wale wabaya waliokufuru, ni mkewe Nuhu na mkewe Luti. Walikuwa chini ya waja wetu wema wawili hao miongoni mwa waja wetu (wema)’ lakini(wanawake hao), waliwafanyia khiana (waume zao watukufu hao) na (waume zao hao) hawakuweza kuwasaidia



chochote mbele ya Mwenyezi Mungu na ikasemwa: “Uingieni
Moto pamoja na hao wanaouingia.” (66:10)



Kuangamia kwa mtoto na mke wa Nuhu(a.s) pamoja na mke wa Lut(a.s) tunajifunza kuwa mtu hataokoka na ghadhabu ya Allah(s.w) kutokana a unasaba alioonao na watu wema na wala hata faidika na malipo ya amali njema walizofanya wengine. Kinyume chake hataadhibiwa mtu mwema kwa kuwa na unasaba na watu waovu maadamu anawafikishia ujumbe na wakamkanusha kama tunavyopigiwa mfano wa mke wa firaun,aliyekuwa mcha-mungu.




Na Mwenyezi Mngu amepiga, (anapiga) mfano wa wale walioamini kweli, ni mkewe Firauni, aliposema; “Ee Mola wangu! Nijengee nyumba Peponi karibu yako na uniokoe na Firauni na amali zake (mbovu), na Niokoe na watu madhalimu”(66:11)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 676


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla, kulinda wasio waislamu na haki zao na mali zao.
Soma Zaidi...

HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA MTUME S.A.W KABLA YA UTUME
MAISHA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII HUD
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana
Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a. Soma Zaidi...

tarekh 4
KUANGAMIZWA KWA JESHI LA TEMBOTukio la pili ni lile tukio la tembo, na ilikuwa hivi:- Kiongozi mmoja wa kiyemeni aliyetambulika kwa jina la Abrah aliona waarabu kutoka maeneo mbalimbali wanafunga misafara kuelekea Makkah kwa lengo la kwenda kuhiji. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NASABA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABILA LAKE, UKOO WAKE NA FAMILIA YAKE
NASABA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi
Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A. Soma Zaidi...