Navigation Menu



Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Namna Uislamu ulivyoingia Tanzania na Afrika Mashariki

- Kupitia misafara ya Wafanyabiashara tangu karne ya 8 A.D kutoka Bara Arab, India, Asia na Ghuba kuja Pwani ya Afrika Mashariki.

- Kufikia karne ya 9 A.D, wahamiaji wengi toka Bara Arab, India na Asia wengi wao wakiwa waislamu, walifanya makazi Pwani ya Somalia na kuufundisha Uislamu kwa wenyeji.
- Kuna alama na ishara za kale za kuonesha kuwepo Uislamu katika Pwani ya Afrika Mashariki zikiwemo magofu ya;

1. Msikiti wa Kaole – Bagamoyo

2. Msikiti wa Kizimkazi – Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, uliojengwa mwaka 500 A.H (1107 A.D)
3. Misikiti ya Kilwa Kisiwani n.k.

- Ibn Batuta alipotembelea Afrika Mashariki mnamo mwaka 1332 A.D, tayari miji mingi ya Pwani hasa Kilwa ilikuwa na Waislamu wengi zaidi.
- Kutokana na mchanganyiko wa Waarab na wenyeji wa Pwani, kulizuka lugha ya Kiswahili na Kibantu na kuzidi kuenea.
- Miji ya Unguja, Tanga, Dar es Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi na Mikindani ilikuwa ndio vituo vikuu vya kueneza Uislamu miji ya bara ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.
- Misafara ya Wafanyabiashara kutoka miji ya Pwani walipofanya makao ya biashara walijenga misikiti kama kituo cha elimu ya Dini ya Kiislamu.
- Hivyo, kutokana fursa ya mchanganyiko huo, waislamu wengi wakawa wafanyabiashara na wamiliki wa kubwa wa maduka, magari, n.k.




Hali ya Uislamu uliofundishwa enzi za Ukoloni

- Historia inaonesha kuwa Uislamu Afrika Mashariki haukuenezwa kwa lengo la kutawala maisha ya jamii, bali ilikuwa ni kitu cha ziada na cha mtu binafsi na lengo kuu likiwa ni biashara.
- Mambo mengi ya msingi katika kuusimamisha Uislamu katika nyanja za uchumi, siasa, jamii hayakupewa umuhimu zaidi ya fiqh ya kufunga, kuswali na sitara kuwa na nafasi kubwa zaidi.
- Mambo mengi yaliyozuliwa kama matanga, dhikiri za kitwariqa, maulidi, khitima, n.k. ndio yalipewa umuhimu na nafasi kubwa.

- Qur’an ilifundishwa sio kwa lengo la kuwa mwongozo wa maisha kibinafsi na kijamii bali kupata thawabu na baraka, kufukuzishia majini na mashetani, kuimbishwa bila kujua maana ya ujumbe wake, n.k




Nafasi ya Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki wakati wa Ukoloni

- Pamoja na kuwa waarabu wengi walikuja na Uislamu Tanganyika, athari ya uvaaji sitara na mila zingine ziliwaathiri sana wenyeji.
- Waislamu walifanya jitihada za kueneza mafundisho ya Uislamu kwa njia za mihadhara, makongamano, n.k. ambapo wakristo wengi walisilimu.
- Waislamu kupitia taasisi na jumuiya mbali mbali, kama vile EAMWS

walianzisha vituo vya elimu kama vile; madrasa, shule za msingi na sekondari.

- Viongozi wengi wa serikali walikuwa ni waislamu kwa sababu ndiyo watu wa mwanzo kujua kusoma na kuandika kwa herufi na tarakimu za kiarabu.
- Sehemu kubwa ya uchumi ilikuwa chini ya miliki ya waislamu waliokuwa ndio wafanya biashara wakuu.
- Waislamu walianzisha vyama vya siasa kama TAA (Tanganyika African

Association), n.k kama vyombo vya kuongozea serikali.




                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 2470


Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu. Soma Zaidi...

Waliomuamini Nabii Nuhu(a.s)
Waliomuamini Nuhu(a. Soma Zaidi...

Waliomshambulia na kumuuwa Ali, makhawariji na si muawiya
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Bara arabu enzi za jahiliyyah, jiografia ya bara arabu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Adam(a.s) na Mkewe Katika Pepo
Adam(a. Soma Zaidi...