image

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Namna Uislamu ulivyoingia Tanzania na Afrika Mashariki

- Kupitia misafara ya Wafanyabiashara tangu karne ya 8 A.D kutoka Bara Arab, India, Asia na Ghuba kuja Pwani ya Afrika Mashariki.

- Kufikia karne ya 9 A.D, wahamiaji wengi toka Bara Arab, India na Asia wengi wao wakiwa waislamu, walifanya makazi Pwani ya Somalia na kuufundisha Uislamu kwa wenyeji.
- Kuna alama na ishara za kale za kuonesha kuwepo Uislamu katika Pwani ya Afrika Mashariki zikiwemo magofu ya;

1. Msikiti wa Kaole – Bagamoyo

2. Msikiti wa Kizimkazi – Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, uliojengwa mwaka 500 A.H (1107 A.D)
3. Misikiti ya Kilwa Kisiwani n.k.

- Ibn Batuta alipotembelea Afrika Mashariki mnamo mwaka 1332 A.D, tayari miji mingi ya Pwani hasa Kilwa ilikuwa na Waislamu wengi zaidi.
- Kutokana na mchanganyiko wa Waarab na wenyeji wa Pwani, kulizuka lugha ya Kiswahili na Kibantu na kuzidi kuenea.
- Miji ya Unguja, Tanga, Dar es Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi na Mikindani ilikuwa ndio vituo vikuu vya kueneza Uislamu miji ya bara ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.
- Misafara ya Wafanyabiashara kutoka miji ya Pwani walipofanya makao ya biashara walijenga misikiti kama kituo cha elimu ya Dini ya Kiislamu.
- Hivyo, kutokana fursa ya mchanganyiko huo, waislamu wengi wakawa wafanyabiashara na wamiliki wa kubwa wa maduka, magari, n.k.




Hali ya Uislamu uliofundishwa enzi za Ukoloni

- Historia inaonesha kuwa Uislamu Afrika Mashariki haukuenezwa kwa lengo la kutawala maisha ya jamii, bali ilikuwa ni kitu cha ziada na cha mtu binafsi na lengo kuu likiwa ni biashara.
- Mambo mengi ya msingi katika kuusimamisha Uislamu katika nyanja za uchumi, siasa, jamii hayakupewa umuhimu zaidi ya fiqh ya kufunga, kuswali na sitara kuwa na nafasi kubwa zaidi.
- Mambo mengi yaliyozuliwa kama matanga, dhikiri za kitwariqa, maulidi, khitima, n.k. ndio yalipewa umuhimu na nafasi kubwa.

- Qur’an ilifundishwa sio kwa lengo la kuwa mwongozo wa maisha kibinafsi na kijamii bali kupata thawabu na baraka, kufukuzishia majini na mashetani, kuimbishwa bila kujua maana ya ujumbe wake, n.k




Nafasi ya Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki wakati wa Ukoloni

- Pamoja na kuwa waarabu wengi walikuja na Uislamu Tanganyika, athari ya uvaaji sitara na mila zingine ziliwaathiri sana wenyeji.
- Waislamu walifanya jitihada za kueneza mafundisho ya Uislamu kwa njia za mihadhara, makongamano, n.k. ambapo wakristo wengi walisilimu.
- Waislamu kupitia taasisi na jumuiya mbali mbali, kama vile EAMWS

walianzisha vituo vya elimu kama vile; madrasa, shule za msingi na sekondari.

- Viongozi wengi wa serikali walikuwa ni waislamu kwa sababu ndiyo watu wa mwanzo kujua kusoma na kuandika kwa herufi na tarakimu za kiarabu.
- Sehemu kubwa ya uchumi ilikuwa chini ya miliki ya waislamu waliokuwa ndio wafanya biashara wakuu.
- Waislamu walianzisha vyama vya siasa kama TAA (Tanganyika African

Association), n.k kama vyombo vya kuongozea serikali.




                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1079


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Maadui wa uislamu na mbinu zao: wanafiki, makafiri, mayahudi, wakristo,
Upinzani dhidi ya Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...

Nini maana ya tabii tabiina
Soma Zaidi...

Historia ya vita vya Muta
hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita. Soma Zaidi...

HISTORIANA MAISHA YA MTUME ISA(A.S)
Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”. Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hadhi na haki za Mwanamke Ulaya Wakati wa mapinduzi ya viwnda
Soma Zaidi...

Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...