Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Download Post hii hapa

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki

Namna Uislamu ulivyoingia Tanzania na Afrika Mashariki

- Kupitia misafara ya Wafanyabiashara tangu karne ya 8 A.D kutoka Bara Arab, India, Asia na Ghuba kuja Pwani ya Afrika Mashariki.

- Kufikia karne ya 9 A.D, wahamiaji wengi toka Bara Arab, India na Asia wengi wao wakiwa waislamu, walifanya makazi Pwani ya Somalia na kuufundisha Uislamu kwa wenyeji.
- Kuna alama na ishara za kale za kuonesha kuwepo Uislamu katika Pwani ya Afrika Mashariki zikiwemo magofu ya;

1. Msikiti wa Kaole – Bagamoyo

2. Msikiti wa Kizimkazi – Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, uliojengwa mwaka 500 A.H (1107 A.D)
3. Misikiti ya Kilwa Kisiwani n.k.

- Ibn Batuta alipotembelea Afrika Mashariki mnamo mwaka 1332 A.D, tayari miji mingi ya Pwani hasa Kilwa ilikuwa na Waislamu wengi zaidi.
- Kutokana na mchanganyiko wa Waarab na wenyeji wa Pwani, kulizuka lugha ya Kiswahili na Kibantu na kuzidi kuenea.
- Miji ya Unguja, Tanga, Dar es Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi na Mikindani ilikuwa ndio vituo vikuu vya kueneza Uislamu miji ya bara ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.
- Misafara ya Wafanyabiashara kutoka miji ya Pwani walipofanya makao ya biashara walijenga misikiti kama kituo cha elimu ya Dini ya Kiislamu.
- Hivyo, kutokana fursa ya mchanganyiko huo, waislamu wengi wakawa wafanyabiashara na wamiliki wa kubwa wa maduka, magari, n.k.




Hali ya Uislamu uliofundishwa enzi za Ukoloni

- Historia inaonesha kuwa Uislamu Afrika Mashariki haukuenezwa kwa lengo la kutawala maisha ya jamii, bali ilikuwa ni kitu cha ziada na cha mtu binafsi na lengo kuu likiwa ni biashara.
- Mambo mengi ya msingi katika kuusimamisha Uislamu katika nyanja za uchumi, siasa, jamii hayakupewa umuhimu zaidi ya fiqh ya kufunga, kuswali na sitara kuwa na nafasi kubwa zaidi.
- Mambo mengi yaliyozuliwa kama matanga, dhikiri za kitwariqa, maulidi, khitima, n.k. ndio yalipewa umuhimu na nafasi kubwa.

- Qur’an ilifundishwa sio kwa lengo la kuwa mwongozo wa maisha kibinafsi na kijamii bali kupata thawabu na baraka, kufukuzishia majini na mashetani, kuimbishwa bila kujua maana ya ujumbe wake, n.k




Nafasi ya Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki wakati wa Ukoloni

- Pamoja na kuwa waarabu wengi walikuja na Uislamu Tanganyika, athari ya uvaaji sitara na mila zingine ziliwaathiri sana wenyeji.
- Waislamu walifanya jitihada za kueneza mafundisho ya Uislamu kwa njia za mihadhara, makongamano, n.k. ambapo wakristo wengi walisilimu.
- Waislamu kupitia taasisi na jumuiya mbali mbali, kama vile EAMWS

walianzisha vituo vya elimu kama vile; madrasa, shule za msingi na sekondari.

- Viongozi wengi wa serikali walikuwa ni waislamu kwa sababu ndiyo watu wa mwanzo kujua kusoma na kuandika kwa herufi na tarakimu za kiarabu.
- Sehemu kubwa ya uchumi ilikuwa chini ya miliki ya waislamu waliokuwa ndio wafanya biashara wakuu.
- Waislamu walianzisha vyama vya siasa kama TAA (Tanganyika African

Association), n.k kama vyombo vya kuongozea serikali.




                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 3317

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

tarekh 09
tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira
Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11

Soma Zaidi...
tarekh 07
tarekh 07

KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO.

Soma Zaidi...