image

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne

Hitimisho juu ya Historia ya maimam wanne

Hitimisho


Maimamu wote wanne walikuwa wanachuoni wacha Mungu na waadilifu katika zama zao. Walifanya juhudi kubwa kusoma na kufanya ijtihada ya kutafsiri na kutoa maoni yao juu ya sheria na masuala mbalimbali ya Fiqh. Ni vizuri tunufaike na matunda ya juhudi zao, lakini tusigawike wala kubaguana kutokana na maoni tofauti ya Maimamu hao juu ya masuala mbalimbali. Wao wenyewe walisoma pamoja au kusomesha na wakaheshimiana na wakaafikiana kutofautiana katika mambo ya msingi bila ya kugombana.


Jambo jingine la msingi la kuzingatia ni kuwa Maimamu hawa walipata mateso makubwa kutokana na misimamo na juhudi zao katika kuuhuisha na kuusimamisha Uislamu katika


jamii. Walichapwa viboko, walifungwa gerezani na kufungwa minyororo na watawala madhalimu. Zaidi ya hivyo hawakukubali kununuliwa na Serikali. Walikataa kabisa kuwa vibaraka wa Serikali. Je, wakati tunafuata Fiqh na Fat’wa zao tunao pia uadilifu kama wao? Misimamo yetu juu ya Serikali za kidhalimu ni kama wao? Je, hatununuliwi na Serikali na kuifanyia kazi kinyume na maslahi ya Uislamu? Je, tupo tayari kufungwa na kuchapwa viboko kwa ajili ya kusimamisha haki kama Imam Abu Hanifa, Malik, Shafii na Hambal?





                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 308


Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...

HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...

CHANZO CHA VITA VYA VITA VYA AL-FIJAR NA ATHARI ZAKE
MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU). Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...

Kuchaguliwa kwa Makhalifa wanne baada ya kutawaf (kufariki) kwa Mtume muhammad (s.a.w)
8. Soma Zaidi...

tarekh 10
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...

HARAKATI ZA DINI WAKATI WA MATABIINA NA TABII TABIINA
Soma Zaidi...

Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu
Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Soma Zaidi...

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake
Soma Zaidi...

KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S. Soma Zaidi...

Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga
Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba. Soma Zaidi...