image

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa


Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.s):


Na kwa kusema kwao: “Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana wa Maryam Mtume wa Mungu”, hawakumuua wala hawakumsulubu ila walibabaishiwa (mtu mwingine aliyefananishwa na Nabii Isa). Na hakika wale waliokhitilafiana katika hayo wamo katika shaka nalo. Wao hawana yakini juu ya hili, isipokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumuua(4:157).



Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake, Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima (4:158)



Kuokolewa Nabii Isa(a.s)


Hukumu ilipitishwa Nabii Issa auawe kwa kusulubiwa. Lakini Allah(s.w)alimnusuru na badala yake akasulubiwa Yuda msaliti aliyefananishwa naye kwa sura na sauti. Kwa hiyo aliyesulubiwa si Yesu bali ni Yuda aliyemsaliti Yesu kama inavyotueleza kwa uwazi Injili ya barnabas katika sura ya 214, 215, 216 na 217.



“Yesu akatoka nje ya nyumba, akaenda bustanini kusali, kama ilivyokuwa ada yake kusali, kwa kurukuu mara mia na kusujudu kwa paji lake la uso. Yuda, ambaye alipajua mahali alipokuwa Yesu na wanafunzi wake, akaenda kwa kuhani mkuu, na akanena: “Ukinipa kilichoahidiwa, nitakupa mkononi mwako Yesu mnayemtafuta: Kwani yu pekee na wanafunzi kumi na moja’.

Kuhani mkuu akajibu: “Wataka kiasi gani?’ Akasema Yuda, “Vipande thalathini vya dhahabu.”



Kisha papo hapo kuhani mkuu akamuhesabia pesa hizo, na akamtuma Mfarisayo kwa gavana kuchukua askari na kwa Herodi, na Wakatoa kikosi chao, kwani waliwahofia watu; wakachukua silaha zao na huku wakiwa na kurunzi na taa ya bakora zao, wakatoka nje ya Yerusalemu.



Askari waliokuwa pamoja na Yuda walipokaribia mahali alipokuwa Yesu, Yesu alisikia kishindo cha watu wengi wakija, naye kwa hofu akaingia ndani ya nyumba. Na wale wanafunzi kumi na moja walikuwa wamelala.
Kisha Mwenyezi Mungu kwa kuiona hatari iliyomkabili mja wake, akamwamuru Jibrili, Mikaili, Rafaili na Urieli, watumishi wake wamuondoshe Yesu ulimwenguni.


Malaika watakatifu wakaja na wakamtoa Yesu nje kupitia katika dirisha la upande wa Kusini. Wakambeba na kumweka katika mbingu ya tatu akiwa katika kundi la Malaika wanaomsabihi Mwenyezi Mungu daima.
Yuda akatangulia kuingia kwa ufidhuli, kabla ya wote katika kile chumba ambacho Yesu alikuwamo. Wanafunzi walikuwa wamelala. Hapo Mwenyezi Mungu Mwingi wa miujiza akafanya muujiza, kwani akambadilisha Yuda kwa sauti na sura akawa kama Yesu hadi tukaamini kuwa alikuwa ni Yesu. Naye baada ya kutuamsha akatuuliza Bwana Yesu aliko. Ndipo tukastaajabu na kumjibu: ‘Wewe, bwana ndiye bwana wetu; je, sasa umetusahau?’



Hisia za wanafunzi wa Yesu kama zilivyoelezwa katika Injili ya Barmabas zinafanana na zilizoelezwa katika Injili nyingine. Injili ya Barnabas yasema kama ifuatavyo na hatua za mwisho za kusulubiwa kwa Yuda Iskariot badala ya Yesu:



“Makuhani Wakuu pamoja na waandishi wa Wafarisayo, walipoona kuwa Yuda hakufa kwa mateso waliyomfanyia na kwa kuhofia kuwa Pilato aweza kumwacha kutundikwa Msalabani. Hivyo wakamhukumu Yuda pamoja na maharamia wawili wafe pamoja naye kifo cha msalabani. Hivyo wakampeleka kwenye Mlima wa Kalvari ambako walikuwa wakinyongwa watu waovu. Wakamsulubisha uchi, ili kumdhalilisha zaidi. Yuda hakufanya chochote isipokuwa kulalamika, “Mwenyezi Mungu kwanini umenitupa, mwovu ametoroka nami nafa, waandishi wa wafarisayo wamchukue Yuda kama mhalifu anayestahili kifo cha msalabani pasi na haki?



Amini nasema kwamba sauti sura na umbo la Yuda vilifanana mno na Yesu kiasi ambacho wanafunzi wake na waumini wengine waliamini kuwa ni Yesu. Hivyo baadhi yao wakayawacha mafundisho ya Yesu kwa kuamini kuwa Yesu alikuwa yu Nabii wa uwongo, na kwamba alifanya miujiza kwa hila za uchawi kwani Yesu aliesema kuwa hatakufa hadi karibu na mwisho wa ulimwengu. Lakini wale waliosimama imara katika mafundisho ya Yesu walisononeshwa sana nyoyo zao kumwona yule aliyefanana kabisa na Yesu (katika hali ile) na wakasahau aliyosema Yesu. Mungu atamfisha karibu na mwisho wa ulimwengu. Ukiwaondoa wafuasi ishirini na watano waliokimbilia Damascus, wengine wote kati ya wale wafuasi 72 walimwona na walikula pamoja na Yesu. Hata hivyo Yesu aliitumia fursa hiyo pia kuwakemea wale ambao waliamini kuwa yeye alikuwa amekufa na kufufuka. “Na aliwakemea wengi ambao waliamini kuwa yeye alikuwa amekufa na kufufuka kwa kusema: ‘Je, mnadhani kuwa mimi na Mwenyezi Mungu tu waongo? Kwani Mwenyezi Mungu amenijaalia mimi kuishi hadi karibu na mwisho wa ulimwengu, kama nilivyokwishakuwaambia. Amin, Amin nawaambia, sikufa bali (alikufa) Yuda, Msaliti. Jihadharini, kwani shetani atafanya kila jitihada kukudanganyeni. Basi kuweni mashahidi wangu kwa Israeli yote na kwa ulimwengu wote kwa yote mliyoyasikia na

kuyaona.” Baada ya kusema hayo alimwomba Mwenyezi Mungu awajaalie waumini uokovu, na awajaalie waasi toba. Na alipomaliza dua yake akamkumbatia mama yake, na kusema:
‘Amani iwe juu yako, wewe mama yangu, tulizana kwa Mwenyezi Mungu aliyekuumba wewe na mimi! Baada ya kusema hivyo aliwageukia wanafunzi wake na kusema: ‘Rehema za Mwenyezi Mungu na amani ziwe juu yenu! “Nao wakashuhudia kwa macho yao Malaika wane wakimchukua Yesu hadi mbinguni.” (Injili ya Barnabas, sura ya 221)



Maelezo haya ya Barnabas, aliyekuwa miongoni mwa wale wanafunzi kumi na moja waliokuwa pamoja na Yesu yanathibitishwa na Qur-an pale Allah(s.w) anapotufahamisha:



Na kwa kusema kwao: “Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana wa Maryamu Mtume wa Mungu”, hawakumuua wala hawakumsulubu ila walibabaishiwa (mtu mwingine waliyemdhani Nabii Isa). Na hakika wale waliokhitilafiana katika hayo wamo katika shaka nalo. Wao hawana yakini juu ya hili, isipokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumuua Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na mwenye hekima.” (4:157-158)



Hapa pana fundisho kubwa kwa kila mwenye kupigania na kusimamisha haki. Mateso na magumu yanayompata mtu katika kazi hii isiwe ni sababu ya kukata tamaa. Bali imzidishie imani na kumtegemea zaidi Allah(s.w). Na hatima ya mambo yote ni ushindi kwa waliosimama katika haki.



                   



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 608


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kulingania Uislamu kwa Jamii Nzima
Baada ya miaka mitatu ya Utume, Muhammad(s. Soma Zaidi...

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh
Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII AYUBU
Soma Zaidi...

Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII MUSA(A.S) NA HARUN(A.S)
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uchaguzi wa Ali bin Abu Twalib kuwa Khalifa wa nne na chanzo cha Makundi katika Uislamu
Soma Zaidi...

Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ghasia na chokochoko za Makhawariji na kuuliwa kwa Ally
Soma Zaidi...

Imam Nasai na kitabu cha Sunan
Soma Zaidi...

Vipengele vya mkataba wa Hudaibiya na faida zake katika Ukombozi (ufunguzi) wa mji wa Makkah
Soma Zaidi...