image

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa


Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.s):


Na kwa kusema kwao: “Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana wa Maryam Mtume wa Mungu”, hawakumuua wala hawakumsulubu ila walibabaishiwa (mtu mwingine aliyefananishwa na Nabii Isa). Na hakika wale waliokhitilafiana katika hayo wamo katika shaka nalo. Wao hawana yakini juu ya hili, isipokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumuua(4:157).



Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake, Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima (4:158)



Kuokolewa Nabii Isa(a.s)


Hukumu ilipitishwa Nabii Issa auawe kwa kusulubiwa. Lakini Allah(s.w)alimnusuru na badala yake akasulubiwa Yuda msaliti aliyefananishwa naye kwa sura na sauti. Kwa hiyo aliyesulubiwa si Yesu bali ni Yuda aliyemsaliti Yesu kama inavyotueleza kwa uwazi Injili ya barnabas katika sura ya 214, 215, 216 na 217.



“Yesu akatoka nje ya nyumba, akaenda bustanini kusali, kama ilivyokuwa ada yake kusali, kwa kurukuu mara mia na kusujudu kwa paji lake la uso. Yuda, ambaye alipajua mahali alipokuwa Yesu na wanafunzi wake, akaenda kwa kuhani mkuu, na akanena: “Ukinipa kilichoahidiwa, nitakupa mkononi mwako Yesu mnayemtafuta: Kwani yu pekee na wanafunzi kumi na moja’.

Kuhani mkuu akajibu: “Wataka kiasi gani?’ Akasema Yuda, “Vipande thalathini vya dhahabu.”



Kisha papo hapo kuhani mkuu akamuhesabia pesa hizo, na akamtuma Mfarisayo kwa gavana kuchukua askari na kwa Herodi, na Wakatoa kikosi chao, kwani waliwahofia watu; wakachukua silaha zao na huku wakiwa na kurunzi na taa ya bakora zao, wakatoka nje ya Yerusalemu.



Askari waliokuwa pamoja na Yuda walipokaribia mahali alipokuwa Yesu, Yesu alisikia kishindo cha watu wengi wakija, naye kwa hofu akaingia ndani ya nyumba. Na wale wanafunzi kumi na moja walikuwa wamelala.
Kisha Mwenyezi Mungu kwa kuiona hatari iliyomkabili mja wake, akamwamuru Jibrili, Mikaili, Rafaili na Urieli, watumishi wake wamuondoshe Yesu ulimwenguni.


Malaika watakatifu wakaja na wakamtoa Yesu nje kupitia katika dirisha la upande wa Kusini. Wakambeba na kumweka katika mbingu ya tatu akiwa katika kundi la Malaika wanaomsabihi Mwenyezi Mungu daima.
Yuda akatangulia kuingia kwa ufidhuli, kabla ya wote katika kile chumba ambacho Yesu alikuwamo. Wanafunzi walikuwa wamelala. Hapo Mwenyezi Mungu Mwingi wa miujiza akafanya muujiza, kwani akambadilisha Yuda kwa sauti na sura akawa kama Yesu hadi tukaamini kuwa alikuwa ni Yesu. Naye baada ya kutuamsha akatuuliza Bwana Yesu aliko. Ndipo tukastaajabu na kumjibu: ‘Wewe, bwana ndiye bwana wetu; je, sasa umetusahau?’



Hisia za wanafunzi wa Yesu kama zilivyoelezwa katika Injili ya Barmabas zinafanana na zilizoelezwa katika Injili nyingine. Injili ya Barnabas yasema kama ifuatavyo na hatua za mwisho za kusulubiwa kwa Yuda Iskariot badala ya Yesu:



“Makuhani Wakuu pamoja na waandishi wa Wafarisayo, walipoona kuwa Yuda hakufa kwa mateso waliyomfanyia na kwa kuhofia kuwa Pilato aweza kumwacha kutundikwa Msalabani. Hivyo wakamhukumu Yuda pamoja na maharamia wawili wafe pamoja naye kifo cha msalabani. Hivyo wakampeleka kwenye Mlima wa Kalvari ambako walikuwa wakinyongwa watu waovu. Wakamsulubisha uchi, ili kumdhalilisha zaidi. Yuda hakufanya chochote isipokuwa kulalamika, “Mwenyezi Mungu kwanini umenitupa, mwovu ametoroka nami nafa, waandishi wa wafarisayo wamchukue Yuda kama mhalifu anayestahili kifo cha msalabani pasi na haki?



Amini nasema kwamba sauti sura na umbo la Yuda vilifanana mno na Yesu kiasi ambacho wanafunzi wake na waumini wengine waliamini kuwa ni Yesu. Hivyo baadhi yao wakayawacha mafundisho ya Yesu kwa kuamini kuwa Yesu alikuwa yu Nabii wa uwongo, na kwamba alifanya miujiza kwa hila za uchawi kwani Yesu aliesema kuwa hatakufa hadi karibu na mwisho wa ulimwengu. Lakini wale waliosimama imara katika mafundisho ya Yesu walisononeshwa sana nyoyo zao kumwona yule aliyefanana kabisa na Yesu (katika hali ile) na wakasahau aliyosema Yesu. Mungu atamfisha karibu na mwisho wa ulimwengu. Ukiwaondoa wafuasi ishirini na watano waliokimbilia Damascus, wengine wote kati ya wale wafuasi 72 walimwona na walikula pamoja na Yesu. Hata hivyo Yesu aliitumia fursa hiyo pia kuwakemea wale ambao waliamini kuwa yeye alikuwa amekufa na kufufuka. “Na aliwakemea wengi ambao waliamini kuwa yeye alikuwa amekufa na kufufuka kwa kusema: ‘Je, mnadhani kuwa mimi na Mwenyezi Mungu tu waongo? Kwani Mwenyezi Mungu amenijaalia mimi kuishi hadi karibu na mwisho wa ulimwengu, kama nilivyokwishakuwaambia. Amin, Amin nawaambia, sikufa bali (alikufa) Yuda, Msaliti. Jihadharini, kwani shetani atafanya kila jitihada kukudanganyeni. Basi kuweni mashahidi wangu kwa Israeli yote na kwa ulimwengu wote kwa yote mliyoyasikia na

kuyaona.” Baada ya kusema hayo alimwomba Mwenyezi Mungu awajaalie waumini uokovu, na awajaalie waasi toba. Na alipomaliza dua yake akamkumbatia mama yake, na kusema:
‘Amani iwe juu yako, wewe mama yangu, tulizana kwa Mwenyezi Mungu aliyekuumba wewe na mimi! Baada ya kusema hivyo aliwageukia wanafunzi wake na kusema: ‘Rehema za Mwenyezi Mungu na amani ziwe juu yenu! “Nao wakashuhudia kwa macho yao Malaika wane wakimchukua Yesu hadi mbinguni.” (Injili ya Barnabas, sura ya 221)



Maelezo haya ya Barnabas, aliyekuwa miongoni mwa wale wanafunzi kumi na moja waliokuwa pamoja na Yesu yanathibitishwa na Qur-an pale Allah(s.w) anapotufahamisha:



Na kwa kusema kwao: “Sisi tumemuua Masihi Isa, mwana wa Maryamu Mtume wa Mungu”, hawakumuua wala hawakumsulubu ila walibabaishiwa (mtu mwingine waliyemdhani Nabii Isa). Na hakika wale waliokhitilafiana katika hayo wamo katika shaka nalo. Wao hawana yakini juu ya hili, isipokuwa wanafuata dhana tu. Na kwa yakini hawakumuua Bali Mwenyezi Mungu alimnyanyua kwake; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na mwenye hekima.” (4:157-158)



Hapa pana fundisho kubwa kwa kila mwenye kupigania na kusimamisha haki. Mateso na magumu yanayompata mtu katika kazi hii isiwe ni sababu ya kukata tamaa. Bali imzidishie imani na kumtegemea zaidi Allah(s.w). Na hatima ya mambo yote ni ushindi kwa waliosimama katika haki.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 951


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mikataba ya aqabah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SALIH(A.S
Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani
3. Soma Zaidi...

Kuchimbwa upya kwa kisima cha Zamzam
Sura na historia ya mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 3.Hapa utajifunza kuhusu kufukuliwa kwa kisima cha Zamzam baada ya kufukiwa muda mrefu. Soma Zaidi...

Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...

Historia ya Dhana ya Kudhibiti Uzazi
Soma Zaidi...

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.
Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam
“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUPASULIWA KWA KIFUA AU TUMBO CHA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) AKIWA MTOTO KWA BI HALIMA
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...