image

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake


Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.s), hakutetereka katika msimamo wake wa kutangaza Ufalme wa Allah(s.w) na kufikisha ujumbe wake. Hakutetereka kwa sababu alitegemea ulinzi wa yule aliyemtuma, mwenye uwezo juu ya kila kitu kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



“..........Akasema (Hud) mimi namshuhudia Mwenyezi Mungu, nanyi shuhudieni ya kwamba mimi niko mbali na hao mnaowashirikisha (na Mwenyezi Mungu) mkaacha (kumuabudu)



yeye (pekee). Basi nyote nifanyieni hila (za kunidhuru) kisha msinipe muhula wowote”.(11:54-55).



Mimi nimemtegemea Mwenyezi Mungu, Mola wangu na Mola wenu. Hakuna kiumbe chochote isipokuwa (Mwenyezi Mungu) anamsanifu atakavyo. Bila shaka Mola wangu yuko juu ya njia iliyonyooka.(11:56)





Na kama mkirudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya Makhalifa (wakazi wa mahala hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni mwenye kuhifadhi kila kitu.”. (11:57)



Ushindi wa Nabii Hud(a.s) Juu ya Makafiri


Makafiri walivyozidi kutakabari na kuzidisha fisadi katika ardhi ikiwa ni pamoja na kutaka kumdhuru Nabii Hud(a.s) na wale walioamini pamoja naye, Allah(s.w) alipitisha hukumu yake ya kuwahilikisha makafiri na kuwanusuru waumini kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



Ilipofika amri yetu ya (kuangamizwa) tulimuokoa Hud pamoja na wale walioamini pamoja naye kwa rehema itokayo kwetu. Na tukawaokoa katika adhabu ngumu.(11:58)




Na hao ndio ‘Ad. Walikanusha aya za Mola wao, na wakawaasi
Mitume yake na wakafuata amri ya kila jabari mkaidi.(11:59)



Na wakafuatishiwa laana katika dunia hii na siku ya kiyama. Sikilizeni hakika ‘Ad walimkufuru Mola wao. Wakaangamizwa hao
‘Ad kaumu ya Hud.” (11:60)

Jeshi la Allah(s.w) lililotumika dhidi ya makafiri katika jamii ya akina ‘Ad ni upepo mkali uliovuma mfululizo kwa siku nane (mausiku Sabaa na michana minane) kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



Basi walipoliona wingu likiyaelekea mabonde yao, walisema: “Wingu hili la kutunyeshea mvua.” (Wakaambiwa) “Bali haya ni ile mliyokuwa mkitaka ije kwa upesi, (adhabu ya Mwenyezi Mungu). Ni upepo ambao ndani yake iko adhabu iumizayo.” “Unaoangamiza kila kitu kwa amri ya Mola wake.” Basi wakawa si wenye kuonekana tena ila nyumba zao tu (ndizo zilizosalia). Hivyo ndivyo tuwalipavyo watu waovu. (46:24-25)




Na bila shaka tuliwastawisha katika yale tusiyokustawisheni nyinyi, na tuliwapa masikio na macho na nyoyo; lakini masikio yao na macho yao na nyoyo zao hazikuwafaa chochote walipokuwa wakikanusha Aya za Mwenyezi Mungu, na yakawazunguka yale waliyoyafanyia mzaha. (46:26)




Na katika (habari za), Adi (ziko alama kadhalika). (Kumbusha) Tulipowapelekea upepo wa papazi uangamizao. Haukuacha chochote ulichokijia ila ulikifanya kama kamba mbovu. (51:41-42)




Walikadhibisha kina Adi (nao); basi ilikuwaje adhabu Yangu na maonyo Yangu! Hakika tuliwapelekea upepo mkali katika siku ya nuhsi iendeleayo (kwao mpaka leo). Ukiwang’oa watu (katika ardhi kisha unawabwata chini, wamelala, wamekufa) kana kwamba ni magogo ya mitende iliyong’olewa. Basi ilikuwaje adhabu Yangu na maonyo Yangu! (54:18-21).



Na majeshi ya mbingu na ardhi ni ya Mwenyezi Mungu; na
Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu; Mwenye hikima. (48:7)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 451


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kifo cha Khalia Uthman kilivyotokea
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII IBRAHIM
Soma Zaidi...

Utekwaji wa Misri na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake. Soma Zaidi...

Mjadala juu ya ndoa ya Mtume Muhammad s.a.w na bi Khadija.
Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi. Soma Zaidi...

Historia ya Kuzuka Imani ya Kishia waliodai kuwa ni wafuasi wa Ally
Soma Zaidi...

Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

tarekh 5
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1 Soma Zaidi...

vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu. Soma Zaidi...