Msonge wa uongozi na siasa katika serikali ya kiislamu mafinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Tofauti na serikali zingine, serikali ya Kiislamu ilijengwa katika misingi mikuu mitatu; Tawhiid, Utume na Ukhalifa (nafasi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni). Rejea Qur’an (30:20), (3:189), (12:40), (7:54), (4:80), (4:65), (24:55), (2:30).

Mgawanyo na msonge wa uongozi wa Dola ya Kiislamu ulikuwa kama ifuatavyo;

 

-    Qur’an – ilikuwa ndio Katiba kuu (Constitution) ya kuongozea Dola iliyotafsiriwa kivitendo (Sunnah) na Mtume (s.a.w) mwenyewe.  

 

-    Mtume (s.a.w.) – alikuwa ndio kiongozi na amiri jeshi mkuu (commander in chief) wa Dola ya Kiislamu aliyesimamia na kuendesha kazi zote za Dola ambapo Msikiti ulikuwa ndio Ikulu ya Dola (State House).

 

-    Shura (Cabinet) – Mtume (s.a.w) aliteua washauri wake wakuu wakaribu, weledi na wazoefu (Baraza la Mawaziri) katika shughuli zote za kuongoza Dola ambao ni Abu Bakr (r.a), Umar bin Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a), Ally bin Abu Twalib (r.a) na Hamza bin Abdul-Muttalib (r.a) na wengineo.

 

-    Sekretarieti (Secretarial) – Mtume (s.a.w) aliteua jopo la waandishi na watunza kumbukumbu na nyaraka zote za serikali.

 

-    Wali au Gavana – Walikuwa ni wakuu wa majimbo (mikoa) ambao waliteuliwa na Mtume (s.a.w) ili kuhakikisha sheria na haki zinatekelezwa ipasavyo katika majimbo yao.

 

-    Amil – Walikuwa ni wakusanyaji wa Zaka na Sadaka walioteuliwa na Mtume (s.a.w) kila jimbo la Dola ya Kiislamu.


-    Kadhi – Mtume (s.a.w) alikuwa ndiye Jaji mkuu wa Dola ya Kiislamu na aliteua Kadhi (Jaji) kila jimbo (mkoa) aliyesimamia haki na hukumu zote kwa mujibu wa Qur’an na Hadith.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1475

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana: