Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Tofauti na serikali zingine, serikali ya Kiislamu ilijengwa katika misingi mikuu mitatu; Tawhiid, Utume na Ukhalifa (nafasi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni). Rejea Qur’an (30:20), (3:189), (12:40), (7:54), (4:80), (4:65), (24:55), (2:30).
Mgawanyo na msonge wa uongozi wa Dola ya Kiislamu ulikuwa kama ifuatavyo;
- Qur’an – ilikuwa ndio Katiba kuu (Constitution) ya kuongozea Dola iliyotafsiriwa kivitendo (Sunnah) na Mtume (s.a.w) mwenyewe.
- Mtume (s.a.w.) – alikuwa ndio kiongozi na amiri jeshi mkuu (commander in chief) wa Dola ya Kiislamu aliyesimamia na kuendesha kazi zote za Dola ambapo Msikiti ulikuwa ndio Ikulu ya Dola (State House).
- Shura (Cabinet) – Mtume (s.a.w) aliteua washauri wake wakuu wakaribu, weledi na wazoefu (Baraza la Mawaziri) katika shughuli zote za kuongoza Dola ambao ni Abu Bakr (r.a), Umar bin Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a), Ally bin Abu Twalib (r.a) na Hamza bin Abdul-Muttalib (r.a) na wengineo.
- Sekretarieti (Secretarial) – Mtume (s.a.w) aliteua jopo la waandishi na watunza kumbukumbu na nyaraka zote za serikali.
- Wali au Gavana – Walikuwa ni wakuu wa majimbo (mikoa) ambao waliteuliwa na Mtume (s.a.w) ili kuhakikisha sheria na haki zinatekelezwa ipasavyo katika majimbo yao.
- Amil – Walikuwa ni wakusanyaji wa Zaka na Sadaka walioteuliwa na Mtume (s.a.w) kila jimbo la Dola ya Kiislamu.
- Kadhi – Mtume (s.a.w) alikuwa ndiye Jaji mkuu wa Dola ya Kiislamu na aliteua Kadhi (Jaji) kila jimbo (mkoa) aliyesimamia haki na hukumu zote kwa mujibu wa Qur’an na Hadith.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1
Soma Zaidi...Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.
Soma Zaidi...