image

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah


Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu
75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.a.w) aliwaita Waislamu na kuwapa habari njema, akawaambia:



“Allah(s.w) keshakupeni mahala pazuri pa amani pa kukaa na kuendesha Dini yenu bila ya kuteswa na yeyote. Mahali penyewe ni Yathrib. Nimekwisha pata habari kuwa ndugu zenu wako tayari kukupokeeni kwa hali na mali. Basi kila aliyetayari aondoke leo asingoje kesho, kwani ndugu zenu huko wamesimama mikono wazi, wanangoja kukupokeeni.”17?



Mtume(s.a.w) alitoa amri ya kuhama mnamo April, 622 A.D. mwaka wa 13 B.U na Waislamu katika makundi makundi walianza kuhama kwa siri kuelekea Yathrib. Ili maadui wasije ng’amua kuhama kwao, Waislamu walisafiri usiku na mchana walijipumzisha mafichoni. Walihama na mali ile tu iliyokuwa nyepesi kuchukulika. Vitu vyao vingine vyote waliviacha Makka ikiwa ni pamoja na nyumba zao, vikachukuliwa na jamaa zao waliobakia katika ukafiri. Ni ‘Uthman bin Affan peke yake aliyeweza kuchukua mali yake yote. Mali ya ‘Uthman isiyochukulika ilinunuliwa na jamaa zake kwa fedha taslimu.



Baada ya miezi miwili hivi, takriban Waislamu wote walikwisha hamia Yathrib. Waislamu wachache, akiwemo Abubakar na ‘Ali bin Abu Talib, walibakia Makka na Mtume(s.a.w) ili kufanikisha maandalizi ya kuhama kwake pale atakapopewa ruhusa ya kuhama na Mola wake.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 322


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu
Musa(a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri
Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji. Soma Zaidi...

Kusilimu kwa Wachawi wa Firaun
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as). Soma Zaidi...

Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.
Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Isa(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Isa(a. Soma Zaidi...

NI IPI FAMILIA YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA NI IPI NASABA YAKE, UKOO WAKE NA KABILA LAKE
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)
“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”. Soma Zaidi...

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi
Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISMAIL
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SHU’AYB(A.S)
Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

tarekh11
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...