Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah


Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu
75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.a.w) aliwaita Waislamu na kuwapa habari njema, akawaambia:



“Allah(s.w) keshakupeni mahala pazuri pa amani pa kukaa na kuendesha Dini yenu bila ya kuteswa na yeyote. Mahali penyewe ni Yathrib. Nimekwisha pata habari kuwa ndugu zenu wako tayari kukupokeeni kwa hali na mali. Basi kila aliyetayari aondoke leo asingoje kesho, kwani ndugu zenu huko wamesimama mikono wazi, wanangoja kukupokeeni.”17?



Mtume(s.a.w) alitoa amri ya kuhama mnamo April, 622 A.D. mwaka wa 13 B.U na Waislamu katika makundi makundi walianza kuhama kwa siri kuelekea Yathrib. Ili maadui wasije ng’amua kuhama kwao, Waislamu walisafiri usiku na mchana walijipumzisha mafichoni. Walihama na mali ile tu iliyokuwa nyepesi kuchukulika. Vitu vyao vingine vyote waliviacha Makka ikiwa ni pamoja na nyumba zao, vikachukuliwa na jamaa zao waliobakia katika ukafiri. Ni ‘Uthman bin Affan peke yake aliyeweza kuchukua mali yake yote. Mali ya ‘Uthman isiyochukulika ilinunuliwa na jamaa zake kwa fedha taslimu.



Baada ya miezi miwili hivi, takriban Waislamu wote walikwisha hamia Yathrib. Waislamu wachache, akiwemo Abubakar na ‘Ali bin Abu Talib, walibakia Makka na Mtume(s.a.w) ili kufanikisha maandalizi ya kuhama kwake pale atakapopewa ruhusa ya kuhama na Mola wake.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 629

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija

Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu.

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Nasaba ya Mtume Muhammad S.A.W na familia yake.

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 1

Soma Zaidi...