Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah


Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu
75 kufika Yathrib salama, Mtume(s.a.w) aliwaita Waislamu na kuwapa habari njema, akawaambia:



“Allah(s.w) keshakupeni mahala pazuri pa amani pa kukaa na kuendesha Dini yenu bila ya kuteswa na yeyote. Mahali penyewe ni Yathrib. Nimekwisha pata habari kuwa ndugu zenu wako tayari kukupokeeni kwa hali na mali. Basi kila aliyetayari aondoke leo asingoje kesho, kwani ndugu zenu huko wamesimama mikono wazi, wanangoja kukupokeeni.”17?



Mtume(s.a.w) alitoa amri ya kuhama mnamo April, 622 A.D. mwaka wa 13 B.U na Waislamu katika makundi makundi walianza kuhama kwa siri kuelekea Yathrib. Ili maadui wasije ng’amua kuhama kwao, Waislamu walisafiri usiku na mchana walijipumzisha mafichoni. Walihama na mali ile tu iliyokuwa nyepesi kuchukulika. Vitu vyao vingine vyote waliviacha Makka ikiwa ni pamoja na nyumba zao, vikachukuliwa na jamaa zao waliobakia katika ukafiri. Ni ‘Uthman bin Affan peke yake aliyeweza kuchukua mali yake yote. Mali ya ‘Uthman isiyochukulika ilinunuliwa na jamaa zake kwa fedha taslimu.



Baada ya miezi miwili hivi, takriban Waislamu wote walikwisha hamia Yathrib. Waislamu wachache, akiwemo Abubakar na ‘Ali bin Abu Talib, walibakia Makka na Mtume(s.a.w) ili kufanikisha maandalizi ya kuhama kwake pale atakapopewa ruhusa ya kuhama na Mola wake.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1031

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Maswali kuhusu Quran

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Chokochoko na Upinzani wakati wa khalifa uthman khalifa wa Tatu

KUPOROMOKA KWA DOLA YA KIISLAMU ALIYOICHA MTUME(S.

Soma Zaidi...
Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.

Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋

Soma Zaidi...
Jinsi tukio la Karatasi lilivyotokea wakati wa Mtume siku chache kabla ya kifo chake

Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.

Soma Zaidi...
Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga

Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba.

Soma Zaidi...
tarekh11

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...
Vita vya uhudi

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mitihani aliyopewa Nabii Ibrahimu kutoka kwa Allah

Tumeona katika historia yake kuwa Nabii Ibrahiim(a.

Soma Zaidi...