image

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif

Baada tu ya Mtume(s.

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif

Mtume(s.a.w) Kulingania Uislamu Katika Mji wa Taif

Baada tu ya Mtume(s.a.w) na Waislamu kurejea Makka kutoka kule Shi’b Abu Talib, Abu Talib na Bibi Khadijah walifariki ikiwa ni mwaka wa 10 baada ya Utume sawa na mwaka 620 A.D. Umuhimu wa wawili hawa kwa Mtume na Waislamu unafahamika. Japo kuwa Abu-Talib hakusilimu, alijitoa muhanga kumlinda na kumhifadhi Mtume(s.a.w) kutokana na shari za Makafiri wa Makka. Mchango wa bibi Khadijah, mke wa kwanza wa Mtume(s.a.w), unafahamika. Tangu mwanzo wa Utume, bibi Khadijah alikuwa kiliwazo kikubwa cha Mtume(s.a.w). Alimfariji Mtume(s.a.w) kwa kila gumu lililomfika na alijitahidi kwa hali na mali kumsaidia Mtume(s.a.w) katika kazi yake. Kutokana na kipigo cha vifo hivi, Mtume(s.a.w) aliuita mwaka ule wa 10 B.U (620 A.D) “Ani al- Huzn” – mwaka wa huzuni.



Baada ya kufariki Abu-Talib na Bi Khadijah Maquraish walizidisha jeuri zao dhidi ya Mtume(s.a.w) na Waislamu kanakwamba wanamuambia Mtume(s.a.w), “Ni nani atakayekusaidia sasa”. Mtume(s.a.w) alipoona kuwa Makka imechafuka kiasi hicho, aliamua kwenda mji wa Taif kuwalingania Uislamu watu wa huko, Banu Thaqif na Banu Khawaizin, kabila la Bibi Halima, mama yake Mtume(s.a.w) wa kunyonya. Alitarajia kuwa kutokana na uhusiano wake na watu wa kabila hilo, watampokea vizuri atakapokwenda huko. Baada ya siku 10 kupita tangu afariki Bibi Khadijah, Mtume(s.a.w) alifunga safari ya kwenda Taif akiongozana na Zaid bin Harith. Alipowasili Taif aliwaendea wakuu wa mji ule na kuwafahamisha lengo la safari yake. Wakuu hawa walimpuuza na kumvunja sana moyo. Aliamua kuwaendea watu wa kawaida lakini nao pia walimpuuza. Hata hivyo, Mtume(s.a.w) hakukata tamaa, bali aliendelea kuwalingania Uislamu watu wa mji ule.



Walipoona Mtume(s.a.w) haondoki pamoja na kumkatisha tamaa kiasi hicho, wakuu wa mji ule walitoa amri kuwa watu wampige mawe popote watakapomuona mpaka aende zake. Watu walipopata amri ile, waliwaelekeza watoto na wahuni wa mji wampige Mtume(s.a.w) mawe mpaka aondoke. Bila ya huruma walimpopoa Mtume(s.a.w) mawe na kumsindikiza nayo kwa umbali wa maili mbili. Zaid alijitahidi sana kumkinga Mtume kwa mwili wake lakini haikusaidia kitu kwani wote walibubujikwa na damu mwili mzima kuanzia kichwani hadi miguuni.



Wale watoto na wahuni wa mji walipoacha kuwapiga na kurudi zao, Mtume(s.a.w) na Zaid walikaa kujipumzisha katika shamba la
‘Utbah bin Rabi’ah. ‘Utbah na ndugu yake walipomuona Mtume katika hali ile walimhurumia na wakamtuma mtumwa wao kuwaletea Mtume vishada vya zabibu na vyakula vingine. Yule mtumwa alimsaidia Mtume(s.a.w) juu ya safari yake na juu ya ujumbe wake. Yule mtumwa alisilimu baada ya kupata maelekezo yale kutoka kwa Mtume(s.a.w) na Bwana wake alijuta sana kwa nini alimtuma pale. Katika hali ile ya udhaifu, Mtume(s.a.w) alimuomba mola wake dua ifuatayo:



“Ya Allah! Kwako nashitakia udhaifu wa nguvu zangu na udhalilifu wangu katika macho ya watu. Ewe mwingi wa Rehema na Huruma kuliko wote wenye huruma! Wewe ndiye Bwana wa wanyonge na wewe ndiye Bwana wangu. Ni kwa watu gani umenipeleka? Kwa adui asiye na huruma anayenikunjia uso au kwa mgeni uliyempa uwezo juu ya jambo langu hili? Sijali lolote kunitokezea isipokuwa naomba ulinzi wako. Naomba hifadhi ya nuru ya uso wako – nuru iangazayo mbinguni na kuondosha aina zote za giza na nuru iongozayo na kudhibiti mambo yote ya hapa duniani na akhera. Naomba uninusuru na ghadhabu zako au kutokuwa radhi na mimi. Sina budi kuondosha Sababu ya wewe kutokuwa radhi na mimi ili hatimaye uwe radhi na mimi. Hapana nguvu wala uwezo ila kutoka kwako” (Sahihi – Muslim).



Mara baada ya dua yake alimjia Jibril (a.s) na baada ya kumpa salamu alisema:

“Allah anajua yote yaliyotokea kati yako na watu hawa. Anamtuma Malaika wa milima kuwa chini ya amri yako”.10

Mara tu baada ya Jibril(a.s) kumaliza ujumbe ule, Malaika muhusika alisimama mbele ya Mtume na kusema:

“Ee Mtume wa Allah, niko chini ya utumishi wako (niko tayari kukutumikia utakavyonituma). Kama unataka naweza kuvigonganisha vilima viwili vilivyoutazama mji huu na watu wote ndani yake wahiliki au unaweza kuamua adhabu yoyote unayotaka wapate.” 11

Mtume(s.a.w) aliye rehema kwa viumbe alijibu:

Hata kama watu hawa hawatakubali Uislamu, ninategemea kwa Allah kuwa watatokea watu katika kizazi hiki watakaomuabudu Allah na kupigania Dini yake”.12

T

ukio hili la Taif linatuonesha jinsi Mtume(s.a.w) alivyokuwa Rehema kwa viumbe na mvumilivu katika kazi yake. Pamoja na kufanyiwa ukatili mkubwa kiasi kile na watu wa mji wa Taif, bado hakuwalaani au kuwataka waangamizwe, bali bado alikuwa na tamaa kuwa watatokea watu wazuri katika kizazi chao watakaokuwa Waislamu na kuipigania Dini ya Allah(s.w) inavyostahiki.



Mafunzo Yatokanayo na Kufariki Bibi Khadija, Abu Twalib na Tukio la Taif
Kufariki kwa Bibi Khadija na Abu Twalib na tukio la Taif tunajifunza yafuatayo:

(i) Hatuna budi kutambua na kulipa fadhila angalau ya kihali (appreciation) kwa kila mtu aliyetoa mchango wa kuusukuma mbele Uislamu.



- Mtume(s.a.w) katika maisha yake yote hakusahau mchango wa Bibi Khadijah na pia hakusahau mchango wa ami yake katika kuuhami Uislamu pamoja na kwamba hakusilimu. Kwa kuwaenzi mwaka walio fariki akauita “Amul-al-Huzn”(mwaka wa huzuni)



(ii)Hatuna budi kutafuta fursa zitakazo pelekea kuulingania Uislamu kwa wepesi, Mtume(s.a.w) alienda Taif kutumia fursa ya udugu wa kunyonya. Mtume(s.a.w) alinyonyeshwa na Bibi Halima wa ukoo wa Saad kutoka mji wa Taif katika kabila la Bani Khawaizin.



(iii)Tuwe na subira na kumuelekee Allah(s.w) tunapokumbana na misukosuko katika mchakato wa kulingania na kusimamisha Uislamu katika jamii. Mtume(s.a.w). Pamoja na madhila yaliyomfika hakukata tamaa bali alimuelekea Mola wake na kuleta dua ile.



(iv)Tujiepushe na kuwalaani watu na kutaka waangamizwe kutokana na jeuri zao dhidi ya Uislamu, kwani asaa baada ya muda wanaweza, kwa rehema za Allah(s.w) kubadilika na kuufia Uislamu au kizazi chao kikaibukia kuupenda Uislamu na kuusimamisha katika jamii.





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 504


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu
Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Soma Zaidi...

Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.
Mambo ya Msingi Aliyofanya Mtume(s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

Historia ya maimam Wanne wa fiqh
Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

Msafara wa vita vya Tabuk Dhidi ya Warumi
Ukombozi wa mji wa Makka (Fat-h Makka) mwaka 8 A. Soma Zaidi...

Allah(s.w) Amnusuru Ibrahim (a.s) na Hila za Makafiri
Pamoja na kudhihirikiwa na ukweli wa udhaifu wa miungu wa kisanamu, watu wa NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Kujengwa upya al Kabah baada ya kuwa na mipasuko.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 18. Hapa utajifunza kuhusu tukio la kujengwa upya kwa al kaaba 🕋 Soma Zaidi...