image

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana


Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.s) na walikuwa viongozi waandamizi wa Firaun. Walikuwa ni watu maarufu katika jamii yao na walikuwa mstari wa mbele katika kumpinga Mtume Musa(a.s).



“Na kwa yakini tulimtuma Musa pamoja na miujiza yetu na hoja (dalili) zilizo dhahiri. (Tulimpeleka) kwa Firauni na Hamana na Karun, wakasema: “(Huyu ni) Mchawi, muongo mkubwa” (40:23-24).

Katika aya nyingine Mwenyezi Mungu anatufahamisha kuwa aliwaangamiza Firaun, Hamana na Qarun kwa sababu waliyakanusha mafundisho ya Mtume Musa na wakatakabari:



Na (vile vile) Qarun na Firauni na Hamana (waliangamizwa); na hakika aliwajia Musa kwa miujiza waziwazi, lakini walijivuna katika ardhi, lakini hawakuweza kumshinda Mwenyezi Mungu. Basi kila mmoja tulimtesa kwa sababu ya dhambi zake. Miongoni mwao wako tuliowapelekea kimbunga cha changarawe; na miongoni mwao wako waliotolewa roho kwa ukulele mkubwa, na miongoni mwao wako tuliowadidimiza ardhini na miongoni mwao wako tuliowagharikisha na hakuwa Mwenyezi Mungu Mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wakijidhulumu (wenyewe) nafsi zao” (29:39-40).



Qarun alijaaliwa kuwa na mali nyingi sana. Lakini alilisahau lengo la maisha akatakabari. Watu walio karibu naye walimnasihi lakini hakuzinduka. Alijivuna na kuona kuwa utajiri aliokuwa nao kaupata kwa juhudi na elimu yake. Alisahau kuwa hiyo ni neema kutoka kwa Allah(s.w).




Hakika Qarun alikuwa katika watu wa Musa, lakini aliwafanyia dhulma. Na tulimpa hazina ambazo funguo zake zinawatopeza watu wenye nguvu (kuzichukua). Walimwambia watu wake: “Usijione (usijigambe), hakika Mwenyezi Mungu hawapendi wanaojigamba” (28:76).




Akasema: “Hakika nimepewa haya kwa sababu ya ilimu niliyo nayo”. Je, hakujua ya kwamba Mwenyezi Mungu amewaangamiza kabla yake watu waliokuwa wenye nguvu zaidi kuliko yeye na wenye mkusanyo mwingi zaidi (kuliko wake yeye)?” (28:78).

Kwa kutakabari kwake huko, Qarun aliangamizwa kwa kudidimizwa ardhini yeye na nyumba yake.




“Basi tukamdidimiza yeye (Qarun) na nyumba yake ardhini, wala hapakuwa na kundi lolote la kumsaidia kinyume na Mwenyezi Mungu, wala hakuwa miongoni mwa walioweza kujisaidia” (28:81).



Mafunzo:


Yapo mafunzo mengi kutokana na maisha ya Qarun. Funzo la kwanza ni kuwa kama utajiri hautatumiwa vyema, waweza kuzaa maovu yafuatayo:


(i) Humfanya mwenye mali kujisahau na kutakabari.

(ii) Humfanya mwenye mali kuwasahau wenye shida na wahitaji. Hali hii huzaa jamii ya wenye mali ambao hula na kusaza wakati wengine hubaki ombaomba wasio na msaada wowote.


Funzo la pili linalolandana na maisha ya Qaruni ni kuwa mali, cheo na mamlaka ya mtu hayawezi kumsaidia chochote Mwenyezi Mungu anapopitisha hukumu yake. Qaruni alitamba kwa mali yake, lakini hukumu ya Allah(s.w) ilipofika alididimizwa yeye na mali yake ardhini.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 846


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu
Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

tarekh 07
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...

Historia ya bi Khadija na familia yake na chanzo cha utajiri wake.
Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake. Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 03
Soma Zaidi...

Yusufu(a.s) Atupwa afungwa Gerezani
Mkewe Al-Aziz hakumkatia tamaa Yusufu(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Imam Tirmidh na Jami'u At-Tirmidh
Soma Zaidi...

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)
Kwa tabia zake njema Yusufu(a. Soma Zaidi...

Imam Malik Ibn Anas
Soma Zaidi...

Kisa cha Malkia wa Sabaa.
Sabaa ulikuwa mji katika nchi inayojulikana leo kama Yemen. Soma Zaidi...