picha

HISTORIA YA BANI ISRAIL

Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina.

HISTORIA YA BANI ISRAIL

HISTORIA YA BANI ISRAIL

Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina. Nchi hii imeitwa takatifu kwa sababu ilikuwa nchi iliyo kaliwa na Mitume watukufu, Ibrahim(a.s),Is-haq(a.s) na Yaβ€˜aquub(a.s). Palestina pamoja na kuwa nchi iliyokaliwa na Mitume maarufu kama hao, watu waliofuatia baadaye waliacha mafunzo yao na kuanzisha mifumo ya maisha ya kishirikina. Hivyo Bani Israil walitakiwa warudi nchini mwao wakautawalishe Uislamu juu ya mfumo ya kishirikina uliokuwemo mle.



Kutoka Misr walienda hadi Mlima Sinai. Hapa walikaa kwa muda wa mwaka mmoja ambapo Nabii Musa(a.s) alishushiwa karibu hukumu zote za Taurat.


Musa(a.s) Kupewa Taurati


Musa(a.s) aliitwa na Allah(s.w) katika Mlima Sinai ili apewe sharia kwa ajili ya wana wa Israili. Siku arubaini ziliteuliwa ili Mtume aweze kujiandaa mwenyewe kwa kufunga na kuswali kwa ajili ya kazi ngumu inayomsubiri ya kuwaongoza Bani Israil wakasimamishe ufalme wa Allah(s.w) katika nchi ya Palestina. Wakati huu Mtume Musa aliwaacha Bani Israil (Mayahudi) katika sehemu ambayo sasa huitwa Wadiy-Shaikh ambayo ipo kati ya Nubi Salih na Mlima Sinai. Mlima Sinai una urefu wa futi 7,359 toka usawa wa bahari na mara nyingi huwa umefunikwa na mawingu. Kileleni mwa mlima huu lipo pango ambapo Nabii Musa (a.s) alikaa siku arobaini. Leo hii karibu na pango hilo pana msikiti na kanisa.



Habari ya kuitwa Musa katika Mlima Sinai inatajwa katika aya zifuatazo:

Na tulimuahidi Musa siku thalathini (afanye ibada, kisha tumpe Taurati) na tukazitimiza kwa kumi ikatimia miadi ya Mola wake siku arubaini. Na Musa akamwambia ndugu yake Haruni: "Shika mahali pangu katika (kuwaangalia) watu wangu na utengeneze wala usifuate njia ya waharibifu" (7:142).

Kama aya inavyobainisha, ilipotimia miadi Musa alikwenda kupokeasheria.



Akasema (Mwenyezi Mungu): "Ewe Musa! Mimi nimekuchagua juu ya watu wote kwa ujumbe wangu na kusema nawe kwangu. Basi pokea haya niliyokupa, na uwe miongoni mwa wanaoshukuru". "Na tulimwandikia katika mbao kila kitu - mawaidha (ya kila namna) na maelezo ya kila jambo. "Basi yashike kwa imara na uwaamrishe watu wako wayashike vema haya. Karibuni nitakuonyesheni miji ya wavunjao amri (zetu namna ilivyoharibika)" (7:144-145).



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 3816

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 web hosting     πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...