Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina.
Nabii Musa na Harun walikuwa na kazi kubwa mbili; kwanza, kuwakomboa Bani Israil kutokana na dhuluma waliyokuwa wakifanyiwa na Firaun na Serikali yake, na pili, kuwarudisha kwenye nchi yao takatifu ya Palestina. Nchi hii imeitwa takatifu kwa sababu ilikuwa nchi iliyo kaliwa na Mitume watukufu, Ibrahim(a.s),Is-haq(a.s) na Ya‘aquub(a.s). Palestina pamoja na kuwa nchi iliyokaliwa na Mitume maarufu kama hao, watu waliofuatia baadaye waliacha mafunzo yao na kuanzisha mifumo ya maisha ya kishirikina. Hivyo Bani Israil walitakiwa warudi nchini mwao wakautawalishe Uislamu juu ya mfumo ya kishirikina uliokuwemo mle.
Kutoka Misr walienda hadi Mlima Sinai. Hapa walikaa kwa muda wa mwaka mmoja ambapo Nabii Musa(a.s) alishushiwa karibu hukumu zote za Taurat.
Musa(a.s) Kupewa Taurati
Musa(a.s) aliitwa na Allah(s.w) katika Mlima Sinai ili apewe sharia kwa ajili ya wana wa Israili. Siku arubaini ziliteuliwa ili Mtume aweze kujiandaa mwenyewe kwa kufunga na kuswali kwa ajili ya kazi ngumu inayomsubiri ya kuwaongoza Bani Israil wakasimamishe ufalme wa Allah(s.w) katika nchi ya Palestina. Wakati huu Mtume Musa aliwaacha Bani Israil (Mayahudi) katika sehemu ambayo sasa huitwa Wadiy-Shaikh ambayo ipo kati ya Nubi Salih na Mlima Sinai. Mlima Sinai una urefu wa futi 7,359 toka usawa wa bahari na mara nyingi huwa umefunikwa na mawingu. Kileleni mwa mlima huu lipo pango ambapo Nabii Musa (a.s) alikaa siku arobaini. Leo hii karibu na pango hilo pana msikiti na kanisa.
Habari ya kuitwa Musa katika Mlima Sinai inatajwa katika aya zifuatazo:
Na tulimuahidi Musa siku thalathini (afanye ibada, kisha tumpe Taurati) na tukazitimiza kwa kumi ikatimia miadi ya Mola wake siku arubaini. Na Musa akamwambia ndugu yake Haruni: "Shika mahali pangu katika (kuwaangalia) watu wangu na utengeneze wala usifuate njia ya waharibifu" (7:142).
Kama aya inavyobainisha, ilipotimia miadi Musa alikwenda kupokeasheria.
Akasema (Mwenyezi Mungu): "Ewe Musa! Mimi nimekuchagua juu ya watu wote kwa ujumbe wangu na kusema nawe kwangu. Basi pokea haya niliyokupa, na uwe miongoni mwa wanaoshukuru". "Na tulimwandikia katika mbao kila kitu - mawaidha (ya kila namna) na maelezo ya kila jambo. "Basi yashike kwa imara na uwaamrishe watu wako wayashike vema haya. Karibuni nitakuonyesheni miji ya wavunjao amri (zetu namna ilivyoharibika)" (7:144-145).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Musa alipotimiza muda, alifunga safari na ahali zake kurejea Misri.
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7
Soma Zaidi...Fat-h Makkah (Kukombolewa Makkah).
Soma Zaidi...Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.
Soma Zaidi...Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...