image

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Mafunzo yatokanayo na Maandalizi ya Mtume (s.a.w) Kimafunzo 

        (Ki-wahay).

  1. Elimu katika fani zote (isipokuwa uchawi) ndio nyenzo kuu katika maandalizi kuusimasha Uislamu katika jamii.

 

  1. Kisimamo cha usiku kufanya ibada, ni katika nyenzo kuu ya pili katika maandalizi ya kusimamisha Uislamu katika jamii.

 

  1. Kusoma Qur’an kwa mazingatio kwa lengo la kuifanya muongozo pekee wa maisha pia ni maandalizi ya kuutawalisha Uislamu katika jamii.

 

  1. Kumtaja na kumtukuza Allah (s.w) vilivyo, pia ni katika nyenzo na maandalizi katika kuusimamisha Uislamu ndani ya jamii.

 

  1. Kujitupa kwa Allah (s.w) kwa kweli – ni kumcha Allah (s.w) peke yake ukweli wa kumcha, nayo ni katika maandalizi ya kusimamisha Uislamu.

Rejea Qur’an (3:102).

 

  1. Kumfanya Allah (s.w) ndiye mlinzi pekee na kumtegemea, ni jambo la muhimu katika kusimamisha Uislamu katika jamii.

 

  1. Kusimama na kuonya (kulingania Uislamu), ni jambo muhimu sana linalowezesha Uislamu kufahamika kwa watu.

 

  1. Kutakasa (kutwaharisha) nguo ni amri ya Allah (s.w) inayomtaka kila mlinganiaji wa Uislamu kuwa safi wa kuigwa kimwili na kiroho pia.

Rejea Qur’an (41:33).

 

  1. Kupuuza na kujitenga na mabaya na wabaya ni jambo la muhimu ili kukataza kwake maovu kuwe na athari.

 

  1. Kufanya ihsani (wema) kwa ajili tu kwa ajili ya kutafuta radhi za Allah (s.w) ndio uhai wa ibada ya muislamu.

 

  1. Kufanya subira kwa ajili ya Allah (s.w) ni katika nyenzo kuu katika kupelekea kuusimamisha Uislamu katika jamii.

 

  1. Utekelezaji wa ujumbe wa Qur’an ni kazi nzito na yenye kila aina ya misukosuko, hivyo kuwa na subira ndio nyenzo pekee.


 

  1. Mtume (s.a.w) Kuulingania Uislamu Makkah kwa siri.

-    Mtume (s.a.w) alianza kulingania familia yake, kisha rafiki zake na jamaa zake wa karibu walio rafiki.

 

-    Mtume (s.a.w) alianza kulingania Uislamu kwa siri kwa muda wa miaka mitatu kwa kukutana na waislamu waliosilimu mwanzo kabisa katika nyumba ya bwana Arqam bin Arqam – maarufu kama Darul-Arqam.

 

 

-    Baada ya miaka mitatu ya kuulingania Uislamu kwa siri, aliamrishwa kuutangaza sasa hadharani kwa jamii yote inayomzunguka. 

 

-    Mara tu baada ya Mtume (s.a.w) kuutangaza ujumbe wa Uislamu hadharani, alikumbana na Upinzani dhidi ya ujumbe wake huo kutoka kwa Makafiri wa Kiqureish wa Makkah.



           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/01/08/Saturday - 01:20:24 am     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1249


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Sulaiman(a.s)
Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

MASWALI MUHIMU KUHUSU HISTORIA NA MAISHA YA MTUME (S.A.W)
1. Soma Zaidi...

Kuandaliwa Mtume (s.a.w) Kulingania Uislamu katika mji wa Makkah
7. Soma Zaidi...

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu
Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Soma Zaidi...

Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nabii Isa(a.s) Alitumwa kwa Wana wa Israil
Mtume Isa(a. Soma Zaidi...

Taasisi za kisiasa za msingi alizotumia mtume (s.a.w) katika kuanzisha dola ya kiislamu madinah
Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 02
Soma Zaidi...