Wakati Mtume(s.
Wakati Mtume(s.a.w) anazaliwa katika karne ya Sita (570 A.D) dunia ilikuwa katika giza totoro la ujahili. Wakazi wa Bara Arab, katika kipindi hicho walikuwa chini sana katika maadili. Ubabe, unyang’anyi na uporaji mali ya misafara ya biashara yalionekana matendo ya kishujaa na ya kujivunia. Wanyonge hawakuwa na haki, wanawake walinyanyaswa na kudhalilishwa hadi kufikia watoto wa kike kuzikwa wangali hai na wanawake kurithiwa kwa nguvu kama ilivyorithiwa mali.
Kwa muhtasari hali ya Bara Arab wakati huo ilikuwa kama alivyoeleza Jaffari bin Abu Twalib mbele ya Mfalme Najash wa Uhabesh:
“Ewe Mfalme, sisi tulikuwa waovu na majahili, tukiabudia masanamu na kula nyamafu hata mizoga ya wanyama waliokufa wenyewe.Tulifanya kila aina ya matendo machafu na ya aibu. Hatukuwa wenye kuwajibika kwa jirani na jamaa zetu. Wenye nguvu miongoni mwetu waliwakandamiza wanyonge. Kisha Allah akamleta Mtume miongoni mwetu ambaye tulimfahamu vema kwa nasaba yake, utukufu wake na uzuri wa tabia yake adhimu. Alituita tumuabudu Mungu mmoja tu na akatukataza kuabudia masanamu na mawe. Alitufundisha kusema ukweli kutunza amana, kuwaangalia ndugu na jamaa na kuwafanyia wema na kuacha maovu. Alituamrisha kusimamisha swala na kutoa Zakat. Alituamrisha kujiepusha na maovu na kujiepusha na umwagaji damu. Alitukataza zinaa, kusema uwongo, kula mali ya yatima na kuwasingizia uovu wanawake watwaharifu.
Alitufundisha Qur-an...” 4 (A Guillaume – The life of Muhammad).
Hali hii ya ujahili haikutawala Bara Arab peke yake, bali katika karne hii ya 6 A.D ulimwengu wote, Mashariki na Magharibi, ulizama katika giza totoro la uovu na ujahili. Ulimwengu katika zama hizo, wanyonge na watu wa chini walikandamizwa na kudhulumiwa pasina chembe ya huruma na wenye uwezo na watukufu miongoni mwao.
Katika kipindi hicho, hata wale waliodai kufuata mafundisho ya Mitume wa Mwenyezi Mungu, Mayahudi na Wakristo, walikuwa katika giza hilo hilo la uovu na ujahili. Mayahudi waliacha mafundisho ya Mtume wao na wakaamua kuishi kulingana na matamanio ya nafsi zao. Walipotokea Mitume waliwafanyia maovu mengi kama ilivyobainishwa katika Qur-an. Wakristo nao waliacha mafundisho sahihi ya Nabii Isa(a.s) badala yake wakafuata ushirikina wa Warumi. Walileta uzushi mwingi juu ya Dini ya Allah(s.w) kama tunavyojifunza katika Qur-an:
“Na Mayahudi wanasema: ‘Uzeiri ni Mwana wa Mwenyezi Mungu’ na Wakristo wanasema; ‘Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu’; haya ndiyo wayasemayo kwa vinywa vyao. Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! (9:30)
Wamewafanya Wanavyuoni wao na Watawa wao kuwa ni miungu badala ya Mwenyezi Mungu, na wamemfanya Masihii Mwana wa Maryamu (pia Mungu) hali hawakuamrishwa isipokuwa kumuabudu Mungu mmoja, hakuna anayestahiki kuabudiwa ila Yeye. Ametakasika na yale wanayomshirikisha nayo.” (9:31).
“Enyi Mlioamini! Wengi katika Makasisi (Wanavyuoni wa Mayahudi na wakristo) na Watawa (wao) wanakula mali za watu kwa batili na kuwazuilia njia ya Mwenyezi Mungu..........” (9:34)
Katika kipindi hicho cha historia utawala wa Kikristo Ulaya Magharibi uliwakandamiza na kuwanyonya wanyonge kama utawala wa kishirikina ulivyokuwa ukifanya huko Mashariki ya Kati na Mashariki ya mbali. Katika kipindi hiki wanasayansi walioibuka na ugunduzi ulio kinyume na maelezo ya Wakuu wa Kanisa walisulubiwa na kuuliwa kinyama miongoni mwao ni mwanasayansi maarufu, Galileo.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1079
Sponsored links
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Kitau cha Fiqh
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
kitabu cha Simulizi
👉6
Madrasa kiganjani
Chanzo cha vita vya Siffin na matokeo yake: Vita vya Ally na Muawia
Soma Zaidi...
NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE
Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a. Soma Zaidi...
Imam Tirmidh na Jami'u At-Tirmidh
Soma Zaidi...
Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Hud(a.s)
(i) Tuanze kulingania kwa kuonesha upweke wa Allah(s. Soma Zaidi...
KUCHIMBWA UPYA KWA KISIMA CHA ZAMZAMA NA KUNYWA MAJI YA ZAMZAMA KISIMA KILICHO BARIKIWA
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...
UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...
Kifo cha Nabii Sulaiman
Pamoja na utukufu na umadhubuti wa ufalme wake Nabii Sulaiman muda wake wa kuishi ulipokwisha aliondoka kama walivyoondoka Mitume,wafalme na wanaadamu wengine. Soma Zaidi...
Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga
Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba. Soma Zaidi...
Hadhi na haki za Mwanamke Ulaya Wakati wa mapinduzi ya viwnda
Soma Zaidi...