Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake

Nabii Lut(a.

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake


Nabii Lut(a.s), kama Mitume wengine walivyofanya aliwanasihi watu wake wamuamini Allah(s.w) na wamche ipasavyo na waogope adhabu yake ambayo ikimfika mtu hapana awezaye kuizuia au kuiondosha.



(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao, (Nabii) Lut: 'Je, hamuogopi?' 'Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.' 'Basi Mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini.(26:161-163)




'Wala sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa (Mwenyezi Mungu) Mola wa walimwengu wote.' 'Je, mnawaingilia wanaume katika viumbe (vyake Mwenyezi Mungu)!' 'Na mnawacha alichokuumbieni Mola wenu katika wake zenu? Kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka (mliyowekewa).'(26:164-166)



Na (wakumbushe) Lut alipowambia watu wake: 'Je, mnaufanya uchafu, na hali mnaona?' Mnawaingilia wanaume kwa matamanio mabaya badala ya wanawake? Hakika nyinyi ni watu mfanyao ya ujinga kabisa. (27:54-55)



Pamoja na nasaha hizi nzuri zilizoambatana na hoja madhubuti, hawakumuamini Lut(a.s) ila watu wachache tu. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu. (51:36)




Jawabu la Makafiri Dhidi ya Nasaha za Nabii Lut(a.s)


Pamoja na Nabii Lut(a.s) kuwanasihi kwa maneno ya hekima na hoja zilizo wazi, watu wake hawakuwa tayari kabisa kuacha maovu yale.



Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)
Walishakuwa walevi wa machafu hayo na walipania kumfukuza Nabii Lut na wale walioamini pamoja naye ambao huchukia ubaladhuli huo.



'Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: Wafukuzeni wafuasi wa Lut katika mji wenu, hao ni watu wanaojitakasa, (basi wasikae na sisi wachafu)' (27:56)



'Wakasema: Kama usipoacha, ee Lut (kutukataza haya), bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaofukuzwa (katika nchi hii).' (26:167)



                   

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 177

Post zifazofanana:-

1.0 NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)
1. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)
Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia. Soma Zaidi...

magonjwa na lishe
DARASA LA AFYA MAGOJWA YANAYOHUSIANA NA VYAKULA 1. Soma Zaidi...

swala ya witri na namna ya kuiswali
3. Soma Zaidi...

Taathira ya Imani ya Malaika katika maisha ya kila siku
Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini. Soma Zaidi...

mambo gani ni haramu kwa mwenye damu ya Hedhi na nifasi (damu ya uzazi)
Soma Zaidi...

MSHENGA WA ALADINI MBELE YA MFALME
Soma Zaidi...

Biashara haramu na njia zake katika uislamu
Soma Zaidi...

HUKUMU YA KUUWA MTU (KUMWAGA DAMU) KWENYE UISLAMU
' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' ' ' ' "' ' ' ' ' [ ' ' '?... Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISA
Soma Zaidi...

Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Salih(a.s)
Mafunzo tuyapatayo hayatofautiani na yale yatokanayo na Historia ya Nabii Hud(a. Soma Zaidi...