Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).
Mawaziri waliokuwa washauri wakuu wa Firauni wakataka wakusanywe magwiji waliobobea katika uchawi nchi nzima, kisha wapambanishwe na Nabii Musa(as).
Basi walipofika wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira tukiwa sisi ndio tutakaoshinda. Akasema: Naam, na pia mtakuwa miongoni mwa wale wanaowekwa mbele katika (Serikali) (26:41-42)
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni sisi tutakuwa ndio wenye kushinda (26:44)
Kisha Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza(vyote) walivyozusha wachawi (26:45)
Wachawi walipoona vitu vyao vya kichawi(viini macho) walivyovitupa uwanjani vimemezwa vyote na nyoka(wa muujiza), walisalimu amri na kutoa shahada:
Hapo wachawi walipinduka wakasujudu. Wakasema: Tumemuamini Mola wa walimwengu wote. Mola wa Musa na Harun (26:46-48)
Firaun aliwatishia wachawi kuwapa adhabu kubwa kwa kusilimu kwao pasina idhini yake (Qurβan 26:49). Inabainika hapa kuwa uchawi si sawa na muujiza,na ndio maana wachawi walishindwa. Hakika uliwadhihirikia ukweli kwamba Musa(a.s) ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Ndio maana Firauni alipotangaza kuwa atawasulubu kwa kuwakata miguu na mikono yao kwa sababu wamesilimu pasina ridhaa yake; hawakuyumba katika imani yao.
Wakasema: Haidhuru, hakika sisi sote tutarejea kwa Mola wetu. Kwa yakini sisi tunatumai ya kwamba Mola wetu atatusamehe makosa yetu, maana sisi tumekuwa wa kwanza wa wenye kusilimu hapa (26:50-51)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu.
Soma Zaidi...Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma.
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7
Soma Zaidi...