Navigation Menu



Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani

Yusufu(a.

Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani

Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani


Yusufu(a.s) alisahauliwa gerezani kwa muda mrefu. Kilichopelekea akumbukwe ni ndoto aliyoota Mfalme. Alipoamka aliwaita makuhani na kuwahadithia:

.............Hakika mimi nimeona ng’ombe Saba wanene wanaliwa na ng’ombe Saba ving’onda. Na nimeona mashuke Saba mabichi na mengine yaliyokauka. Enyi wakubwa nitafsirieni ndoto yangu ikiwa ninyi mnaweza kutafsiri ndoto(12:43)

Wakasema: ni ndoto iliyovurugika wala sisi hatujui tafsiri ya ndoto hizi(12:44)

Yule mfungwa aliyefasiriwa ndoto na Yusufu(a.s) kuwa atatolewa gerezani alimkumbuka Yusufu na akawaambia:

........Mimi nitakwambieni tafsiri yake. basi nitumeni (12:45)



Alipofika gerezani, akamwita:

Yusufu! Ewe mkweli! Tueleze hakika ya ng’ombe Saba wanene kuliwa na ng’ombe Saba dhaifu. Na mashuke Sabaa mabichi na mashuke makavu, ili nirejee kwa watu wapate kujua. (12:46)

Akasema: Mtalima miaka Saba mfululizo kwa juhudi. Na mtakavyovivuna viacheni katika mashuke yake isipokuwa kidogo mnavyokula.(12:47)

Kisha itakuja baadaye miaka Saba ya shida itakayokula vile mlivyolima, isipokuwa kidogo mtakachohifadhi (12:48)

Walipopata taawili ya ndoto hii, Mfalme kwa furaha kubwa kabisa alisema


Mleteni kwangu nimchague awe mtu wangu mwenyewe. Basi alipozungumza naye (Mfalme) alisema, Hakika wewe leo kwetu umekwishakuwa ni mwenye hishima na muaminiwa.(12:54)



Yusufu alimuagiza mjumbe wa mfalme kuwa kabla hajotoka gerezani lijulikane lile shauri la wanawake waliomtaka kwa nguvu na kumchochea aingie katika maasi - Qur’an (12:50). Yusufu(a.s) alitaka hilo lifanyike ili apate kusafika kwa Al-Aziz na kwa jamii nzima kuwa hakumfanyia dhuluma ile aliyosingiziwa.


Mfalme aliwakusanya wanawake na kuwauliza

“...............Nini jambo lenu lilikuwa mlipomtamani Yusufu kinyume cha matamanio yake? wakasema ‘Hasha lillahi! Sisi hatukujua ubaya wowote kwake. Mkewe Al-Aziz naye akasema: Sasa haki imedhihirika, mimi ndiye niliyemtamani kinyume cha nafsi yake, na bila shaka yeye yu miongoni mwa wa kweli (kabisa)” (12:51)



Baada ya hapo ndipo Yusufu(a.s) alipokubali heshima ile aliyopewa na kupendekeza awe msimamizi wa hazina ya nchi.

Akasema nifanye niwe mtazamaji wa hazina ya nchi; hakika mimi ni mlinzi mzuri na mjuzi hodari (12:55)



Tendo hili la Yusufu(a.s) kudai kesi yake na wanawake iangaliwe na Mfalme na haki itolewe, lilinyanyua sana hadhi yake. Kwanza aliifasiri ndoto ngumu ya Mfalme ambayo iliwashinda wachawi, wanganga na watabiri wote wa kutegemewa katika nchi. Pili alipotakiwa na Mfalme atoke gerezani, alikataa mpaka kesi ifikishwe mahakamani, mkosaji abainishwe. Matokeo ya kesi yakawa wanawake kukiri mbele ya hadhara ya Mfalme kuwa Yusufu(a.s) hakuwa na hatia bali wao ndio waliokuwa waovu.



Ilidhihiri kwa kila mtu kuwa hakuna yeyote miongoni mwao, ila amezidiwa na Yusufu(a.s) kwa uadilifu na tabia njema kwa ujumla. Haiwi ni kitu cha ajabu basi tunapoona Yusufu anapewa dhamana ya kuangalia hazina yote ya nchi. Huu ni wadhifa unaohitajia mtu aliyepea kwa uadilifu na hakuwepo aliyemzidi Yusufu(a.s).



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 728


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA
Historia ya harakati za Mtume(s. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Kulingania watu wake na Miujiza Aliyoonyesha Nabii Isa(a.s)
Mwenyezi Mungu pekee ndiye aliyewawezesha Mitume na Manabii kufanya miujiza. Soma Zaidi...

Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...

MASWALI MUHIMU KUHUSU HISTORIA NA MAISHA YA MTUME (S.A.W)
1. Soma Zaidi...

Kisa cha Israa na Miraji na kufaradhishwa swala tano
Safari ya Mi'rajKatika mwaka wa 12 B. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na Historia ya Nabii Yunus(a.s)
(i) Allah(s. Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...