Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake

Baada ya NabiiIbrahiim(a.

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake


Baada ya NabiiIbrahiim(a.s) kutoa shahada ya kweli alipomuahidi Mola wake: “Nimejisalimisha kwa Bwana Mlezi wa Walimwengu Wote” alianza kulingania Tawhiid kwa watu wa jamii yake. Kwa hekima aliona aanze kumlingania baba yake, aliyekuwa mchonga masanamu na kiongozi wa Ibada ya masanamu. Alianza kumlingania kwa kutumia hoja zenye mashiko katika akili ya mwanaadamu kama ifuatavyo:



(Wakumbushe) alipomwambia baba yake: “Ewe baba yangu! Kwa nini unaabudu visivyosikia na visivyoona na visivyofaa chochote?” (19:42)



“Ewe baba yangu! Kwa yakini imenijia ilimu isiyokujia. Basi nifuate nitakuongoza njia iliyo sawa.(19:43)



Ewe baba yangu! Usimuabudu Shetani, hakika Shetani ni mwenye kumuasi (Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema.(19:44)



“Ewe baba yangu! Hakika naogopa kukupata adhabu inayotoka kwa Mwingi wa rehema (Mwenyezi Mungu), (ukifanya hivyo) utakuwa mwenziwe shetani.” (19:45)



Babu yake, badala ya kuyatia akilini aliyofikishiwa na mwanawe, alimkemea, kumtisha na badaye kumfukuzilia mbali nyumbani kwake.



“Akasema (yule baba yake) “Je! Unaichukia miungu yangu, ewe Ibrahim? Kama huachi (haya unayosema) lazima nitakupiga mawe. Na niondokelee mbali kwa muda mchache (huu).” (19:46)



Nabii Ibrahim(a.s)hakutetereka na kurudi nyuma alipofukuzwa nyumbani mwa baba yake. Alibakia na msimamo wake wa kulingania Dini ya Allah(s.w) kwa moyo mkunjufu huku akitarajia msaada kutoka kwake Allah(s.w) pekee.



“Na mimi nakuondokeeni (na kujiepusha) na mnayoyaabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu. Hakika sitakuwa mwenye kukhibu (kukosa ninalotaka) kwa kumuomba Mola wangu.” (19:48).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1151

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Yusufu(a.s)

“Kwa yakini katika (kisa cha) Yusufu na ndugu zake yako mazingatio mengi kwa wanaouliza (mambo wapate kujua)”.

Soma Zaidi...
Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
tarekh 02

FAMILIA YA MTUME (S.

Soma Zaidi...
MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)

KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara.

Soma Zaidi...
Kuchimbwa upya kwa kisima cha Zamzam

Sura na historia ya mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 3.Hapa utajifunza kuhusu kufukuliwa kwa kisima cha Zamzam baada ya kufukiwa muda mrefu.

Soma Zaidi...