image

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA

Mtume Lut(a.

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA


Mtume Lut(a.s) ni mpwawe Ibrahiim(a.s) waliohama pamoja yeye kutokea Iraq. Lut(a.s) alitumwa kuulingania Uislamu katika miji miwili ya Sodoma na Gomora katika nchi ya Transjodan.



Tabia ya Watu wa Miji ya Sodoma na Gomora
Jamii aliyoikuta Mtume Lut(a.s) ilikuwa imeanguka sana kimaadili. Walifikia hali ya kuwa waovu zaidi ya wanyama licha ya kuwa maumbile yao yalikuwa ya binaadamu. Walizama kwenye kufanya maovu matatu mazito kama yanavyotajwa katika Qur-an:



Na (wakumbushe Nabii) Lut; alipowaambia watu wake: “Bila shaka nyinyi mnafanya uovu (ambao) hakuna yoyote aliyekutangulieni kwa (uovu) huo katika walimwengu.(29:28)




“Je, mnawaendea wanaume, na mnawakatia njia (watu kwa kuwaua na kuwanyang’anya njiani) na mnafanya maovu katika mikusanyiko yenu?” basi halikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: “Tuletee adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa umiongoni mwa wasemao kweli!” (29:29)”



Katika aya hizi tunafahamishwa kuwa watu wa jamii ya Lut (a.s) walikuwa wakifanya maovu mazito yafuatayo:


1) Walikuwa wakiwaendea wanaume wenzao katika kutosheleza matamanio yao ya ngono.

2) Walikuwa wakifanya uharamia na uporaji wa mali za watu.

3) Walikuwa wakifanya maovu haya hadharani na kwa ufahari.

Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)



Je, jamii yetu hivi leo haifanyi haya na zaidi ya haya tena kwa ufahari. Hivi leo kuna mashindano ya U-miss ambayo wasichana vigoli hujitokeza jukwaani mbele ya hadhara ya watazamaji wanaume kwa wanawake wakiwa wamevaa viguo visivyo sitiri mwili. Hali ni hiyo hiyo kwenye kumbi za dansi, disko na hata kwenye sherehe za kiserikali. Na wengine wameenda mbele zaidi hata kufikia wanawake kusoma taarifa za habari katika television wakiwa uchi wa mnyama na kufikia wengine kucheza sinema za wanawake na wanaume wakifanya ngono hadharani.



Leo hii baadhi ya nchi za magharibi zimepitisha sheria yakuruhusu ndoa baina ya wanaume kwa wanaume wakifanya ushenzi ule ule wa mabaradhuli wa miji ya Sodoma na Gomora.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1088


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Waliomuamini Nabii Nuhu(a.s)
Waliomuamini Nuhu(a. Soma Zaidi...

KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S. Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Mafunzo kutokana na vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuangamizwa kwa Watu wa Lut(a.s) watu wa Sodoma na Gomora
Watu wa Lut(a. Soma Zaidi...

Kupotoshwa Mafundisho ya Nabii Isa(a.s)
Pamoja na Isa(a. Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

Kuangamizwa kwa jeshi la tembo mwaka alizaliwa Mtume Muhammad s.a. w
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w sehemu ya 4. Hapa utajifunza kuhusu historia ya kuangamiza kwa jeshi la tembo. Soma Zaidi...

Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...