image

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)


Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.s), alijitahidi kutumia mbinu mbali mbali ili wapate kumuelewa vizuri na kufuata ipasavyo ujumbe aliowaletea. Miongoni mwa mbinu alizozitumia ni hizi zifuatazo:



Kwanza alitoa hoja kwa watu wake za kuonesha haja na umuhimu wa kumuamini Allah(s.w) na kumuabudu ipasavyo. Aliwatanabahisha:


Mumekuwaje hamuweki hishima ya Mwenyezi Mungu. Na hali yeye amekuumbeni namna baada ya namna? Je hamuoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyoziumba mbingu saba tabaka- tabaka(moja juu ya moja). Na Akakaufanya mwezi ndani yake uwe nuru na Akalifanya jua kuwa taa? Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi, mimea. Kisha atakurudisheni humo na atakutoeni tena.Na Mwenyezi Mungu amekufanyieni ardhi kuwa busati (kitu kizuri mlichotandikiwa). Ili mtembee humo katika njia zilizo pana. (71:13-20)



Pili aliwabashiria malipo au jaza watakayopata endapo watamwamini na kumtii Allah(s.w) ipasavyo. Kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:



Akasema (Nuhu) Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji niliyedhahiri kwenu. Ya kuwa mwabuduni Allah na mcheni na mnitii.(71:2-3)



Atakusameheni madhambi yenu na atakuakhirisheni (bila ya balaa) mpaka muda uliowekwa...........(71:4)




Atakuleteeni mawingu yanyeshayo mvua nyingi. Na atakupeni mali na watoto, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.” (71:11-12)



Tatu aliwakhofisha watu wake na adhabu ya Allah(s.w) ya hapa duniani na huko akhera, endapo watakataa kumuamini Allah (s.w) na kumuabudu ipasavyo:



Na sisi tulimpeleka (tulimtuma) Nuhu kwa watu wake, (akawaambia): “Mimi kwenu ni Muonyaji anayebainisha (kila kitu). Ya kwamba msimuabudu yoyote isipokuwa Mwenyezi Mungu tu; hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya siku (kubwa hiyo) inayoumiza.” (11:25-26)



“Hakika sisi tulimtuma Nuhu kwa watu wake, ya kwamba waonye watu wako kabla ya kuwajia adhabu iumizayo.” (71:1)

Nne aliwalingania usiku na mchana:

“Akasema (Nuhu): Ee Mola wangu: Kwa hakika nimewalingalia watu wangu usiku na mchana, lakini wito wangu haukuwazidishia ila kukimbia” (71:5-6)



Tano, aliwalingania kwa njia ya muhadhara kwa sauti: Tena niliwaita kwa jahari. (71:8)



Sita, aliwalingania kwa siri kwa kumuendea mmoja mmoja:



“Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri’. (71:9)



Saba,aliwaweka watu wake wazi kuwa hakuwa anawalingania kwenye Dini ya Allah(s.w) kwa kutaraji malipo yoyote kutoka kwao bali alifanya hivyo kwa manufaa yao wenyewe.




“Na sikutakini juu yake ujira, ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.” (26:109)



Nane,alisubiri na kudumu kuwalingania kwa mbinu zilizoainishwa kwa muda wa miaka elfu kasoro hamsini (950).



“Na bila shaka tulimtuma Nuhu kwa watu wake na akakaa nao miyaka elfu kasoro hamsini, (wasikubali kumfuata), basi tufani liliwafika, (wakaghariki), na hali walikuwa madhalimu (29:14)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 638


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Zakaria(a.s) na Yahya(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Zakaria (a. Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11 Soma Zaidi...

historia na maisha ya Mtume IS-HAQ(A.S.) NA YA‘AQUUB(A.S.)
Is-haq(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII LUTI
Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ujumbe wa Nabii Ibrahiim(a.s) kwa Mfalme Namrudh
Soma Zaidi...

Mafunzo kutokana na vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Waliomshambulia na kumuuwa Ali, makhawariji na si muawiya
Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)
KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani. Soma Zaidi...